Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Azimio la Bunge la kuridhia Mkataba wa Uanzishwaji wa Eneo Huru la Biashara la Afrika

Hon. Kavejuru Eliadory Felix

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buhigwe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Azimio la Bunge la kuridhia Mkataba wa Uanzishwaji wa Eneo Huru la Biashara la Afrika

MHE. KAVEJURU E. FELIX: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nikushukuru kwa upekee kabisa kwa kupata nafasi hii ili niweze kuchangia hoja kwenye Azimio la uanzishwaji wa Soko Huru katika Bara la Afrika.

Mheshimiwa Naibu Spika, azimio hili ni azimio zuri sana, linafaida nyingi sana, ningeomba kila Mbunge aweze kuridhia mkataba huu, una faida nyingi sana. Kwanza ukiangalia nchi yetu kijiografia Tanzania mahali ilipo tumebahatika kuwa sehemu nzuri kijiografia, tuna maliasili, tuna ardhi nzuri. Kwa hiyo ni suala tu la kujipanga.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuridhia mkataba huu utafungua masoko mapya kwa mazao yetu ya kilimo. Tunachangamoto ya mazao kama tulivyoona kwenye mahindi, lakini litafungua masoko mapya kwa mazao mengine madogo madogo kama alizeti na choroko.

Mheshimiwa Naibu Spika, pia mkataba huu utaimarisha mnyororo wa thamani utakuwepo na nini na ushindani, ushindani wa uzalishaji ambao tunaenda kushindana katika soko hilo huru utaboresha ubora wa mazao yetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, hivyo mimi ninashauri sana, ninashauri Serikali ijipange kwa kuelimisha kwa kutoa elimu kwa mapana na kwa marefu kwa wazalishaji wetu. Kama ni kilimo sasa twende kwenye kilimo cha biashara, tulime kilimo cha kibiashara. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini vilevile taasisi za kifedha zijipange kupunguza riba na ziwe tayari kusaidia wazalishaji kwa maana ya wakulima na wajasiriamali wapate mitaji ili tuweze kusogea kwenda kwenye masoko ya mbali. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa takwimu ambazo zipo sasa hivi nchi ambayo ina uchumi mzuri kwenye hili soko ambalo tunaenda kwenye wale wanachama ambao wamekwisha saini ambao ni 42. Nchi ambayo ina uchumi mzuri sasa hivi ni Nigeria ikifuatiwa na Egypt, ikifuatiwa na Afrika Kusini, sisi hatupo mbali sana tupo kama namba 10.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo sisi tuna nafasi nzuri kama Serikali ikijipanga ikahakikisha, ikaboresha miundo mbinu ili wakulima wetu huko wanako zalisha barabara zikafika, kukawepo na gharama ndogo za usafirishaji wa mazao yetu tutafaidika zaidi, zaidi na zaidi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo azimio hili ni zuri, litatusogeza mbele, litaenda kuzalisha mabilionea wengi katika Tanzania yetu na litaenda kuleta mabadiliko makubwa sana katika sekta mbalimbali; sekta ya kilimo na biashara pia kutokana na ushindani utakaotokea.

Mheshimiwa Naibu Spika, ninaomba kuunga hoja Azimio hili la Mkataba wa Uundwaji wa Soko Huru la Afrika. (Makofi)