Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Azimio la Bunge la kuridhia Mkataba wa Uanzishwaji wa Eneo Huru la Biashara la Afrika

Hon. Issa Ally Mchungahela

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lulindi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Azimio la Bunge la kuridhia Mkataba wa Uanzishwaji wa Eneo Huru la Biashara la Afrika

MHE. ISSA A. MCHUNGAHELA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Awali ya yote kwanza nimshukuru Mwenyezi Mungu mwingi wa Rehema aliyeniweka hai na kuja kushiriki katika mjadala huu wa African Continental Free Trade Area.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza ni-declare kwamba mradi huu au itifaki hii ni itifaki nzuri ambayo itatuwezesha kufanikisha. Kwa hiyo, kwa mwanzo kabisa lazima niunge mkono hoja kwa sababu tunaenda kuliendea soko na takribani watu bilioni 1.2 ni watu wengi sana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini, baada ya kusema hivyo msimamo wangu mwingine wakutaka kuistua Serikali usichukulie kuwa kama nataka kuipinga Serikali au kutaka kuipinga hoja hii. Lakini ichukuliwe kwamba ni chachu ya kuisukuma Serikali kujielekeza katika kutatua changamoto muhimu hasa hizi za biashara ambazo zitatuwezesha sisi kunufaika sana na mkataba huu.

Mheshimiwa Naibu Spika, ukiniuliza kwamba, je? tumechelewa kwenye mkataba huu kama ambavyo watu wengine walivyojaribu kudai, ninaweza nikasema hapana hatujachelewa na hata wale waliokataa kusaini mwanzo mkataba huu walifanya jambo zuri kabisa kwa sababu gani? Kwa sababu Serikali iliweza kujiangalia kama Taifa na kuanza kutafakari njia bora za kuangalia changamoto ambazo zilitufanya tukaukataa mkakataba huu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini pia sisi kama nchi tulijitutumua mbele za nchi nyingine duniani na kujionyesha kwamba sisi ni watu huru, lakini tunauwezo wa kujiamulia maamuzi yetu ambayo yenye maslahi na nchi yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini ukiniuliza kwamba, je, tuendelee kukataa mkataba huu? Nitakuambia hapana, hatuwezi kufanya hivyo kwa sababu mazingira ya sasa hivi yamekuwa ni mazingira bora kuliko yale mazingira ya zamani. Lakini hali kadhalika pia mkataba huu una content nyingi sana ambazo ni positive ambazo kama Serikali itafanya jitihada kwa umakini kabisa kufuatilia maslahi gani ambayo tunayoyapata humu, tutanufaika na huu mkataba.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini kwa utendaji wa Serikali nianze kusema kwamba sina shaka kwa sababu kuna mambo mengi sana ambayo nafikiri kwa kukataa ule mkataba mwanzo kusaini Serikali ilienda ikajielekeza katika mazingira mazuri yakuanza kutafuta changamoto kama vile nilivyosema zile zilizosababisha watu kuukataa ule mkataba.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mfano ukiangalia, Serikali ilienda ikaweka mazingira mazuri ya mtandao wa barabara, imeweka mtandao mkubwa kabisa wa barabara ambao ni chachu kubwa katika suala la kiuchumi hasa hasa katika uzalishaji kule kwa mfano vijijini kwenye mazao ya kilimo. Mtandao wa barabara umekuwa ni muhimu sana naweza nikaishukuru sana Serikali na kuipongeza na kwamba iongeze bidii, iongeze zaidi ya hapo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini pia ukiangalia Serikali ilifanya kazi kubwa pia ya kutengeneza mtandao wa nishati mpaka sasa hivi tunazungumzia kwamba nchi nzima tumekuwa na umeme takribani kila kijiji kasoro vijiji vichache. Hii pia ni sehemu kubwa sana Serikali ambayo iliifanya kazi hii kwa kuangalia changamoto zile ambazo zilipelekea sisi kuukataa ule mkataba kwa mara ya kwanza.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo kwa namna moja au nyingine hatuna sababu ya sisi kujiona inferior kwa kukataa huu mkataba mwanzo haizidi haipungui ni kwamba tumepata nguvu sasa ya kuweza kupambana zaidi na wenzetu kwa sababu tayari tushapata vitu wezeshi vitakavyosaidia sisi kutusukuma kwenda mbele zaidi.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini kuna kitu ambacho najaribu kutaka kusisitiza kwa Serikali pamoja na mazuri yote ambayo nimeyasema hapa na mengi ambayo nakusudia kuyafanya ukiangalia kuna mambo mengi sana kwa mfano, ujenzi wa Stigler’s gauge, lakini kuna pia ujenzi wa EPZ, lakini kuna mambo mengi sana yaani kama vile vyanzo vya nishati nakadhalika.

Mheshimiwa Naibu Spika, bado tunaona kabisa kwamba Serikali ina nia nzuri, lakini pia nataka kuisisitizia Serikali kwamba iongeze kasi katika utekelezaji wa hizi adhima zake au nia zake, kwa sababu gani? Zenyewe ndizo zitakazotufanya sisi tuweze kuonekana mbele za wenzetu kwamba ni watu tupo superb na tuweze kuchangamkia hizi fursa tunazokwenda kuziendea vizuri zaidi.

Mheshimiwa Naibu Spika, kitu ambacho nilichotaka kusisitiza hapo ni kuiomba Serikali ifanye jitihada ya makusudi kabisa kuweka sub-seeds kwenye mazao au biashara mkakati vitu ambavyo tunaona sisi tunafanya vizuri zaidi basi tujaribu kuweka sub-seeds kuwezesha sisi kupata bei nzuri au kuwa na gharama ndogo ya uzalishaji, lakini wakati huo huo tukiweza kuweka bei nzuri ukilinganisha na bei za wenzetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, kitu kingine pia ni kuweza kutumia kodi au tariff vizuri katika maeneo ambayo tunaona kwamba tupo tunakaribia kupoteza, sehemu ambapo tukiona kwamba hapa tunakaribia kupoteza tunatakiwa tuweke tariff kwa ajili ya ku-protect. Kwa mfano, hizi product zetu tunazozalisha, lakini pia ku-protect wazalishaji wetu wa ndani na wafanyabiashara wa ndani.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa maana hiyo tukijaribu kufanya hivyo nafikiri sisi tutakuwa ni miongoni mwa watu wenye manufaa makubwa sana na huu mkataba kwa sababu hiyo inajieleza mpaka sasa hivi ukizingatia tupo katika ndani ya watu au nchi kumi ambazo ni bora sasa hivi Afrika katika masuala ya kiuchumi.

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kusema hivyo naomba kuunga mkono hoja asilimia mia moja. Ahsante. (Makofi)