Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Azimio la Bunge la kuridhia Mkataba wa Uanzishwaji wa Eneo Huru la Biashara la Afrika

Hon. Judith Salvio Kapinga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Azimio la Bunge la kuridhia Mkataba wa Uanzishwaji wa Eneo Huru la Biashara la Afrika

MHE. JUDITH S. KAPINGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi. Kwanza nianze kwa kuipongeza Wizara kwa kuja na mkataba huu, kwa kuwa naamini kwamba mkataba huu una manufaa makubwa sana kwa nchi yetu ya Tanzania na nchi nyingine za Bara la Afrika. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nianze kwa kusema kwamba uanzishwaji wa maeneo huru ya biashara siyo jambo jipya duniani, ni jambo ambalo limeanza miaka mingi nyuma tangu miaka ya 1950; na mfano mzuri ni European Economic Community ambayo ilianza mwaka 1957 na baadaye kubadilishwa jina pale ambapo European Union iliundwa mwaka 1993. Kwa hiyo, inawezekana kwa sisi kama Bara la Afrika tumechelewa kutokana na changamoto mbalimbali na kuja na mkataba huu 2019 kwa sababu ni wazi kabisa sisi kama Afrika tumekuwa wahanga wa masuala ya ukoloni. Kwa hiyo, inawezekana tulichelewa kama Bara. hata hivyo, changamoto tulizonazo na ambazo tulikuwa nazo kama bara haziwezi kutunyima fursa ya sisi kama waafrika kuja na mbinu mbalimbali za kutuinua kiuchumi ikiwemo kuwa na soko huru la biashara kuelekea kutimiza malengo yetu ya ajenda 2063. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nianze kwa kuchangia kwamba mojawapo ya hasara au changamoto ambazo tunaweza kuzipata kutokana na kuridhia mkataba huu ambao tumeelezwa na Serikali, moja ni kupungua kwa mapato ya kodi yanayotokana na ushuru wa forodha kwa bidhaa ambazo zitaondolewa kodi kwa takriban shilingi bilioni 41 ndani ya miaka 10, yaani wastani wa shilingi bilioni 4.1 kwa mwaka. Pia mojawapo ya changamoto nyingine ambazo tumeambiwa ni uwezekano wa kupoteza ajira kwa baadhi ya sekta hususan sekta za uzalishaji.

Mheshimiwa Naibu Spika, nachelea kusema kwamba changamoto hizi zinafikirisha ukilinganisha kwamba sisi kama Taifa bado tuna changamoto ya ajira, lakini niseme kwamba kuna baadhi ya masuala ambayo kama Taifa tukifanyia kazi, changamoto hizi ambazo tunaweza tukazipata kutokana na kuridhia mkataba huu, tunaweza tukazipunguza kwa kiasi kikubwa sana na njia mojawapo ni kuendelea kujenga uchumi shindani. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, uchumi shindani una variables mbalimbali, lakini sisi kama taifa tukiendelea kujijenga tunaweza tukapunguza changamoto hizi kwa sababu tayari tuliishaanza. Mojawapo ya masuala ambayo tunaweza tukayajenga ili kuweza kuongeza uchumi shindani mojawapo ni kuendelea kuwa na miundombinu imara na wezeshi lakini vilevile kuendelea kuwa na taasisi imara, kuendelea kuwa na elimu ya juu inayotoa vijana ama watu ambao wanaweza kupambana kwenye soko la ajira la biashara, kuenzi mabadiliko ya teknolojia, kuenzi mabadiliko ya ubunifu na kuwa na masoko yenye tija. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, naamini iwapo kama Taifa tutafanyia kazi masuala haya na kuwa na uchumi shindani, tunaweza tuka-penetrate kwenye masoko na vilevile athari ambazo tumeambiwa tunaweza tukawa nazo kama Taifa, tunaweza tukazipunguza ikiwemo suala la ajira. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mfano ukiangalia ripoti ya takwimu za biashara za benki yetu kuu kwenye kanda za kiuchumi kati ya Tanzania na nchi nyingine za jirani kwa mfano tukianzia biashara za bidhaa kati ya Tanzania na nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki, Tanzania tumekuwa tukifanya vizuri. Kwa mfano ukiangalia takwimu za miaka saba nyuma yaani kuanzia 2013 mpaka 2020 kwenye kuuza bidhaa tumekuwa tukifanya vizuri kwa sababu tumekuwa tukipanda, tulianza mwaka 2013 na US dola milioni 419, lakini mwaka jana 2020 tumeweza kupanda mpaka US dola milioni 812.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini kwenye kuuza bidhaa tumeweza ku- contained soko letu na kulinda soko letu kwa sababu tulianza na US dola milioni 394, lakini kwa mwaka jana tumeweza ku-contained na kushuka mpaka dola milioni 324. Kwa hiyo, inaonyesha kabisa sisi kama Watanzania tunafursa kwenye soko hili kwa sababu bidhaa zetu kwa uuzaji wa nje tumekuwa tukifanya vizuri sana na tumeweza kulinda soko letu la ndani kwa kiasi kikubwa sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini kwenye masuala ya ajira, ukweli ni kwamba ukipunguza kodi kwenye bidhaa unafanya makampuni yaweze kuzalisha zaidi, lakini generally hii ina-apply kote, ina-apply tu kwenye nchi ambazo gharama zao za maisha ni ndogo, ya kwamba kama gharama za maisha husika ni ndogo inamaana bidhaa zao zinaweza zika- penetrate kwenye masoko ya nchi nyingine kuliko nchi ambazo gharama za maisha ni kubwa mno.

Mheshimiwa Naibu Spika, tunaweza tukachukulia mfano, wamarekani wakati wamejiunga na mkataba wa North America na free trade area, wamarekani viwanda vyao vingi sana vilikosa ajira kwa sababu Mexico ilikuwa na gharama za chini ndogo kuliko Marekani, lakini sisi kama Tanzania cost of living inakuwa approximated kwa dola 0.32. ina maana tunafanya vizuri kuliko nchi nyingine za Afrika.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, tunaweza tukauza zaidi ni kuimarisha tu baadhi ya masuala ya kiuchumi ili tuweze kushindana zaidi na kufanya vizuri katika soko. Na hapa sasa inabidi tufanyie masuala ambayo ni ya msingi sana ikiwemo kujiongeza kiji-digital, yaani huduma ambazo zinatolewa kiji-digital sasa tunafanya kazi kwa uharaka na ziweze kuwa reliable. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nilizungumzia suala la taasisi imara liweze kutuvusha lazima taasisi zetu ziweze kubadilika.

NAIBU SPIKA: Dakika moja Mheshimiwa kengele imeshangongwa.

MHE. JUDITH S. KAPINGA: Mheshimiwa Naibu Spika, namalizia kwa mfano taasisi za kiserikali kama AFTC lazima zitoke kwenye kufanya kazi kwa mazoea ya finically na ziende kwenye biashara za mitandao kwenda kulinda walaji kwenye mitandao. Sasa hivi ukiwauliza hawana hata mkakati wa kulinda walaji kwenye mtandao ambapo biashara kubwa imeamia huko. kwa hiyo, mimi sina shaka kama Taifa tutafanya vizuri tukiendelea kufanya kazi tu kwa ajili ya variable sisi ambazo tukazifanyisha ukiwa na uchumi shindani basi tunaweza tukafanya kazi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja. (Makofi)