Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Azimio la Bunge la Kuridhia Itifaki ya Jumuiya ya Afrika Mashariki ya Viwango vya Afya ya Mimea, Wanyama na Usalama wa Chakula

Hon. Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Azimio la Bunge la Kuridhia Itifaki ya Jumuiya ya Afrika Mashariki ya Viwango vya Afya ya Mimea, Wanyama na Usalama wa Chakula

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nikushukuru kwa nafasi, lakini pili nitumie nafasi hii kuwashukuru Wabunge waliotoa maoni, mengi ni ushauri ambao kama Wizara tutahakikisha tunauzingatia.(Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ninataka nichangie kwa ufupi sana. Kwanza sisi tunazalisha locally tuna trade globally kwa hiyo lazima zitakuwepo threat na tunai-consider threat waliyoitoa Waheshimiwa Wabunge hasa athari ya hofu ya suala la GMO.

Mheshimiwa Naibu Spika, nataka niwaambie kwamba mwaka jana tumepitisha sheria ndani ya Bunge lako Tukufu (The Plant Health Act, 2020) iliyopitishwa na ukisoma katika definition imesema wazi kabisa hii ni instrument moja tutakayoitumia ku-control vihatarishi vyote vya teknolojia za GMO. Imesema a plant means any living plant all the parts thereof, including seeds and gem plus. Sasa hivi ndiyo tunatengeneza Kanuni na mapendekezo ya Kamati tutaya- consider kwa kiwango kikubwa sana kuhakikisha kwamba tunaitumia sheria hii na mamlaka hii kuwa ni instrument muhimu ya control. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la pili ninataka tu niseme kwamba Tanzania Plant Health Authority inatujengea uwezo mkubwa wa kuwa na maabara zetu ambazo zitakuwa Internationally Certified ambazo mazao yote ya kilimo yanayotoka nje ya mipaka yetu yakipata hati ya uthibitisho kutoka katika maabara zetu hizi itakuwa ni moja kwa moja tunaweza kuingia katika soko la Kimataifa. Kwa hiyo, hili ni jambo ambalo nilitaka niwahakikishie Waheshimiwa Wabunge. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, suala jingine ni hoja ya Sera ya Kilimo, tuwahakikishie kwamba tutaihuisha iweze kuendana na mahitaji ambayo ni ya sasa na kuweza ku- accommodate mahitaji yote ya protocol hii. Protocol hii inazungumzia suala la harmonization.

Mheshimiwa Naibu Spika, protocol hii pamoja na kuwa tunaipitisha leo suala la harmonization mnapoenda kwenye meza kama ninyi hamna instrument ambazo zitawafanya m-harmonize na wenzenu hamuwezi ku- harmonize chochote utakuwa out of the game.

Kwa hiyo, kwa kuipitisha leo protocol na sisi kwenda kuhuisha Sera yetu ya Kilimo na uwepo wa hii sheria ambayo imepitishwa na Bunge lako Tukufu na uanzishwaji wa hizi maabara itatujengea uwezo mkubwa wa ku-compete na wenzetu katika soko la Jumuiya Afrika Mashariki, lakini vilevile soko la Kimataifa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kuna hoja wamesema Waheshimiwa Wabunge kuhusu maabara ambazo zipo katika baadhi ya maeneo yaani isiwe kwamba center ya maabara ni moja. Labda tuseme Nyanda za Juu Kusini tuna maabara yetu ya treat ambayo ni ya chai kama Wizara, tumeanza kuiwezesha maabara ile ili iweze kuhudumia na mazao mengine ambayo siyo specifically ya chai mfano, parachichi na mahindi. Maabara zetu za Uyole na maabara zingine tutazijengea capacity ili ziweze ku-meet mahitaji yanayotukabili. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nimalizie tu kuwahakikishia Waheshimiwa Wabunge kwamba kama Wizara tunajua threat zinazotukabili katika protocol hii, lakini tunazo mitigation solution ambazo tunaweza kupambana nazo na tutakuwa salama huko mbele tunakokwenda.

Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja, nashukuru. (Makofi)