Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Azimio la Bunge la Kuridhia Itifaki ya Jumuiya ya Afrika Mashariki ya Viwango vya Afya ya Mimea, Wanyama na Usalama wa Chakula

Hon. Amb. Dr. Pindi Hazara Chana

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Azimio la Bunge la Kuridhia Itifaki ya Jumuiya ya Afrika Mashariki ya Viwango vya Afya ya Mimea, Wanyama na Usalama wa Chakula

MHE. BALOZI DKT. PINDI H. CHANA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Nianze kwa kumpongeza Mheshimiwa Waziri, Naibu Waziri na Serikali bila kuisahau Kamati kwa kutuletea Itifaki ya Jumuiya ya Afrika Mashariki ya viwango vya afya ya mimea, usalama wa wanyama na chakula. Tunashukuru sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya wananchi wa Mkoa wa Njombe, hususan wakulima, specific wanawake, natoa shukrani za dhati kwa kutuletea itifaki hii. Wananchi wa Njombe wamekuwa wanasafirisha sana mazao yakiwemo viazi, mahindi, parachichi na mazao mengine mengi kama mbao na kadhalika, kwenda katika Jumuiya ya Afrika Mashariki. Wananchi wa Njombe na wengine kwa kweli walikuwa wanapata changamoto za aina mbalimbali.

Mheshimiwa Naibu Spika, nimeshuhudia watu wanapeleka mahindi nchi za jirani wakifika kwa wale wanaosaga mahindi millers inaweza ikawa ni maize or wheat wanaambiwa kwamba mzigo wako una sumu kavu. Mtu amekuja na semi-trailer mbili hana mahali pa kula, hana mahali pa kulala, tukisingizia aflatoxin na mzigo unakuwa ushaingia nchi za jirani.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, eneo hili imekuwa ni changamoto ya kutosha, na baadhi ya maeneo kumekuwa na madalali, mara mzigo unapofika nje ya boarder madalali wanakuwa wanawasumbua wakulima wetu kwamba wacha nichukue mzigo nitakutafutia soko, wanakuwa wanakosa pesa zao kwa wakati. Kwa heshima na taadhima niipongeze Serikali kwa kweli kwa kutuletea Itifaki hii, ku-ratify hii protocol kwa sababu sasa itaokoa.

Mheshimiwa Naibu Spika, na nikienda Ibara ya 2 kwenye malengo ni pamoja na kuhamasisha biashara ya kilimo. Asilimia 60 ya Watanzania tumejikita kwenye kilimo kwa hiyo hii Itifaki iko mahali sahihi kabisa na imekuja wakati muafaka. Kwa hiyo, kupitia Itifaki hii, Ibara ya 2 pale tunaambiwa promote trade in food and agriculture commodities. Niombe sana sasa tuendelee kuwa na masoko ya mipakani, mipaka yetu yote ya Tanzania, nchi zote tunazopakana nazo, wilaya muhimu tuweke haya masoko.

Mheshimiwa Naibu Spika, pia nizidi kupongeza Ibara ya 4(2)(a) kinasema katika masuala ya plant health, harmonize the inspection and certification procedure of plant and plant product. Yaani sasa tunakwenda kulinganisha, kufanya ukaguzi uwe unafanana. Sasa tunapoambiwa na nchi jirani kwamba hapa kuna sumu kuvu (aflatoxin) kwa sababu sasa viwango vinakwenda kulingana, hakuna kudanganyana na kubabaishana kwamba akipima TBS ndio sasa itatambulika certificate yake na Kenya Bureau of Standards (KBS); huku kuna TBS kule kuna KBS.

Mheshimiwa Naibu Spika, wakati mwingine tunachukua mfano kuna kampuni mbalimbali ambao wana counterpart wao…

MHE. NUSRAT S. HENJE: Mheshimiwa Naibu Spika, taarifa.

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Pindi Chana kuna taarifa.

T A A R I F A

MHE. NUSRAT S. HENJE: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimpe taarifa mzungumzaji kwamba aflatoxin ni sumu kuvu sio sumu kavu. (Makofi)

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Pindi Chana unapokea taarifa hiyo?

MHE. BALOZI DKT. PINDI H. CHANA: Mheshimiwa Naibu Spika, ninaendelea na hoja yangu kuhusiana na suala zima la aflatoxin na sipingani na tafsiri kwa hiyo, tunaendelea na hoja.

Mheshimiwa Naibu Spika, aflatoxin ni jambo ambalo linaleta changamoto na mara mizigo inapokwenda tunapoambiwa kwamba kuna aflatoxin au aina nyingine ya chemicals ambayo haifai/sumu inaleta changamoto sana kwa wakulima wetu.

Kwa hiyo, hili ni eneo ambalo Itifaki hii inakwenda kuboresha maana kuna watu wanyalukolo kuna namna yetu ya kutamka na watu wa maeneo mengine kila watu na namna yao, kwa hiyo, bora tutumie kiingereza ili kuweka muafaka. Kwa hiyo, nazungumzia suala zima la aflatoxin.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini pia kuna maeneo ya kubadilishana information. Katika Ibara ya 9 inazungumzia suala zima la sharing of information. Tumekuwa na changamoto nyingi sana kwenye masuala ya kilimo kwa mfano masuala mazima ya nzige namna gani tunakabiliana na changamoto ya nzige.

Mheshimiwa Naibu Spika, eneo lingine ambalo naunga mkono ni Ibara ya 11 harmonization of policies, laws and regulations; hili pia ni eneo ambalo muhimu sana tuka harmonize kwa mapema.

Mheshimiwa Naibu Spika, Ibara ya 8 inazungumzia boarder post control. Naomba kushauri kwamba katika suala zima la boarder post control sasa tuhakikishe boarder post zote ni one stop boarder post. Baadhi ya maeneo bado hatuna one stop boarder post, kunakuwa na boarder mbili; mtu ana-clear upande wa Tanzania na nchi inayofuata. Lakini tunapokuwa na one stop boarder post kwanza inapunguza kupoteza muda kwa hiyo, muda haupotei na mzigo unakuwa cleared kwa haraka na mara mzigo ukiwa cleared kwa haraka, maana yake ni kwamba time is money anaweza kwenda kuchukua mzigo mwingine kupata kupeleka kule kunakostahili.

Mheshimiwa Naibu Spika, eneo lingine ni suala zima la Ibara ya 16 ambayo inatueleza wazi kwamba this protocol shall enter into force upon ratification and deposit of instrument of ratification with the Secretary General by all the partner states. Mara leo baada ya kuridhia na tunaunga mkono wote hapa kuridhia Itifaki hii, niombe sana tusichelewe ku-deposit with the Secretary General wa East Africa Community. Secretary General who shall transmit certified true copies of the Protocol and Instruments of ratification to all the partner states.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, naunga mkono na nampongeza sana Waziri kutuletea Kamati naunga mkono na kwa kweli kwa niaba ya Wananchi wa Njombe naunga mkono hoja ya kuridhia Itifaki hii ya Jumuiya ya Afrika Mashariki, ahsante sana. (Makofi)