Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Azimio la Bunge la Kuridhia Itifaki ya Jumuiya ya Afrika Mashariki ya Viwango vya Afya ya Mimea, Wanyama na Usalama wa Chakula

Hon. Ramadhan Suleiman Ramadhan

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chake Chake

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Azimio la Bunge la Kuridhia Itifaki ya Jumuiya ya Afrika Mashariki ya Viwango vya Afya ya Mimea, Wanyama na Usalama wa Chakula

MHE. RAMADHAN SULEIMAN RAMADHAN: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana nami kupata fursa ya kuchangia kwenye itifaki au azimio hili la Jumuiya ya Afrika Mashariki linalohusiana na usalama wa mimea, wanyama pamoja na usalama wa chakula. Kutokana na maelezo ambayo yametolewa mbele yetu na Mheshimiwa Waziri pamoja na taarifa ya Kamati, kitu ambacho nimejifunza, ni kwamba hii SPS Measure ina component mbili. Component ya kwanza inahusiana na Sanitary Major na component ya pili inahusiana na Phytosanitary Measure.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa kwenye component ya kwanza ya sanitary major ni kwamba msisitizo uwekwe kwenye kuweka measures au maana yake ni hatua au vitu vinavyoweza kum-protect binadamu kutokana na maradhi yanayotokana na vyakula. Maana yake ni measure to protect human from born disease. Ndiyo kitu ambacho nimekisoma.

Mheshimiwa Naibu Spika, mchango wangu na ushauri wangu kwa Serikali utajikita kwenye kwenye usalama wa chakula (food safety) kwenye hii component ya kwanza ya sanitary measure. Ili twende sambamba na itifaki, ni kwamba lazima measures zetu tunazozichukua kama Taifa, moja kati ya vitu vinavyotakiwa tujitahidi ni kuhakikisha chakula tunachokila sisi na Watanzania wote kipo salama. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kulikuwa na hoja hapa za baadhi ya wachangiaji kwamba tumechelewa kwa muda wa miaka nane. Kuchelewa siyo tatizo, lakini tunapokiendea kitu, tuwe na uhakika wa asilimia mia moja kwamba tunakwenda kutekeleza itifaki ikiwa sisi ndani bado tuko salama na tutaji-protect kuingiza chakula kutoka nje ambacho hakiko salama na tutakuwa tuna ulinzi wa vyakula vyetu tunavyokula. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa ushauri wangu ni kwamba ili hizi measures zichukuliwe na zifanye kazi, mchangiaji aliyepita amezungumzia kwenye aspect moja ya sheria, lakini tunahitaji kuwa na sera ya usalama wa chakula (policy) ambayo haipo. Tukitaka tuende sambamba na wenzetu ni lazima tujitahidi tuwe na Sera ya Usalama wa Chakula. The main and first thing kwenye ile component ya sanitary measure, halafu sera ndiyo ifuatiwe na sheria pamoja na kanuni na miongozo itakayotufanya sisi tuwe salama zaidi kwenye vyakula vyetu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwenye Ibara ya 11 ya itifaki hii ambayo inasema, itahusu nchi wanachama kuainisha, yaani kufanya harmonization sera, sheria, kanuni na program ili kufanikisha madhumuni ya itifaki hii, ni ibara imo ndani ya itifaki. Imesema, katika utekelezaji wa itifaki hii, ni lazima nchi wanachama kama blocks za Afrika Mashariki, tuwe au tume-harmonize sera zetu, sheria zetu, kanuni zetu na miongozo yetu kwenye wanyama, kwenye mimea na kwenye usalama wa chakula.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa tuna-harmonize vipi wakati hata hiyo sera hatuna; na sheria zetu bado ziko scattered zinazohusiana na usalama wa chakula? Hizi zetu za ndani, hazijawa harmonized. Huwezi kupata sheria moja ambayo imesimama kulinda usalama wa chakula. Usalama wa chakula upo kwenye sheria tofauti tofauti, ndogo ndogo; unakuta iko kidogo kidogo kila mahali; kwenye uvuvi kidogo, kwenye kilimo kidogo, kwenye vipodozi kidogo, lakini hatuna sheria mama ambayo inasimama kufanya protections ya aina ya vyakula tunavyokula. Huo ndiyo wasiwasi wetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, kama walivyosema wachangiaji, kuridhiwa kwa itifaki hii iwe ni wake-up call kwa Wizara na Serikali kwamba tunahitaji tuchukue hatua za haraka, tena haraka sana ili kama nchi tuwe na sera, sheria na kanuni zitakazotulinda sisi kama nchi kwanza, halafu litakaloilinda block yote ya Afrika Mashariki kutokana na vyakula tunavyozalisha na tunavyotumia kila siku kwenye maisha yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, huo ndiyo ulikuwa mchango wangu kwa ujumla. Naomba kuunga mkono hoja. (Makofi)