Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Azimio la Bunge la Kuridhia Itifaki ya Jumuiya ya Afrika Mashariki ya Viwango vya Afya ya Mimea, Wanyama na Usalama wa Chakula

Hon. Yustina Arcadius Rahhi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Azimio la Bunge la Kuridhia Itifaki ya Jumuiya ya Afrika Mashariki ya Viwango vya Afya ya Mimea, Wanyama na Usalama wa Chakula

MHE. YUSTINA A. RAHHI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi hii ili kuweza kuchangia hoja hii ya Azimio la Kuridhia Itifaki ya viwango vya Afya ya Mimea, Usalama wa Wanyama pamoja na vyakula vya Jumuiya ya Afrika Mashariki (The East African Community Sanitary and Phytosanitary Protocol).

Mheshimiwa Naibu Spika, Tanzania ni miongoni mwa nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki na tumeingia kwenye Jumuiya hii tukakubaliana mikataba, tukasaini mkataba toka mwaka 1999. Kati ya Mikataba hii inataka tushirikiane Nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki katika mambo mbalimbali kwa usawa na haki kwa ajili ya manufaa ya nchi wanachama.

Mheshimiwa Naibu Spika, kipengele kimojawapo ambacho kipo kwenye mikataba hii ni kipengele namba 151 ambacho kinataka Nchi Wanachama kutengeneza Itifaki ya Kuridhia Afya ya Mimea na Usalama wa Wanyama pamoja na chakula na sisi Tanzania tulisha iandaa hii na kuitayarisha toka mwaka 2013.

Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na kwamba sisi ni Wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki vile vile sisi ni Wanachama wa Shirika la Biashara la Dunia (World Trade Organization), sisi kuwa wanachama wa Jumuiya ya World Trade Organization imetulazimu vile vile kutekeleza baadhi ya makubaliano ambayo mojawapo ndio hii Itifaki ya Afya ya Mimea na Usalama wa Wanyama pamoja na Usalama wa Chakula, imebidi tutekeleze kwa sababu na sisi ni wanachama ambapo sasa makubaliano haya yanaitwa The Agreement on the Application of Sanitary and Phytosanitary Protocol. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Itifaki hizi lengo lake kubwa ni kulinda afya ya mlaji popote pale. Ndio maana sisi sasa tunatekeleza makubaliano mbalimbali ya kimataifa yakiwemo makubaliano ya usalama wa chakula ambayo inaitwa the Codex Alimentarius Commission na vilevile ya usalama wa mimea ambayo ni International Plant Protection Convention na pamoja na hii ya usalama wa wanyama World Organization for Animal Health.

Mheshimiwa Naibu Spika, sisi kwa kuingia au kuridhia Itifaki key ya Jumuiya ya Afrika Mashariki kwa vyovyote vile tuna faida mbalimbali ambazo kama Nchi Tanzania tutaweza kuzifuata na moja wapo ni kukua kwa biashara ya mazao, mifugo pamoja na uvuvi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kama tunavyoona kwamba kijiografia sisi tuko vizuri, sisi ni wazalishaji wakubwa wa mazao ya chakula. Kwa hiyo kuwa na document ya pamoja, Itifaki itatusaidia sisi kuweza kuingia kwenye biashara ya Jumuiya ya Afrika Mashariki. Tunafahamu kwamba sisi soko letu kubwa la mahindi lilikuwa Kenya lakini hivi karibuni tumeona vizuizi kwamba mahindi yetu walisema yana sumu kuvu. Sasa tungekuwa tayari tuna hii Itifaki inayokubali kiwango gani cha sumu kuvu ambayo tumekubaliana katika Itifaki hii pengine hiki kizuizi kisingekuwepo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, vile vile sisi Tanzania ndio wafugaji wakubwa, ndio tuna mifugo mingi katika nchi hizi za Jumuiya ya Afrika Mashariki. Kwa hiyo moja kwa moja hii inatupa fursa sisi Watanzania, kwamba sasa tunaweza tukaingia kwenye soko la Afrika Mashariki. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, faida nyingine kubwa ni kwamba sasa Itifaki hii itatoa hamasa kwa wakulima, wafugaji na wavuvi pamoja na taasisi mbalimbali kwamba sasa wakazalishe kwa viwango vinavyotakiwa ku-win biashara hii ya Jumuiya ya Afrika Mashariki pamoja na Kimataifa. Kwa mfano tu, wafugaji wanapaswa kuogesha mifugo yao pamoja na kuwapa chanjo pengine labda ya ugonjwa wa midomo na kwato, kwa sababu hii mara nyingi imekuwa kizuizi ili kwamba mifugo yao pamoja na mazao ya mifugo kama nyama na maziwa iweze kupata soko katika Jumuiya ya Afrika Mashariki. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja, nawashauri na Wabunge wenzangu kwa sababu kuna round table kuweza ku-harmonize mambo fulani kama GMO ambayo sisi kwa kisera tulishayakataa, Itifaki hii ipite na tuweze kufanya biashara katika Jumuiya ya Afrika Mashariki pamoja na biashara ya Kimataifa.

Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja. (Makofi)