Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Azimio la Bunge la Kuridhia Itifaki ya Jumuiya ya Afrika Mashariki ya Viwango vya Afya ya Mimea, Wanyama na Usalama wa Chakula

Hon. Prof. Patrick Alois Ndakidemi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Moshi Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Azimio la Bunge la Kuridhia Itifaki ya Jumuiya ya Afrika Mashariki ya Viwango vya Afya ya Mimea, Wanyama na Usalama wa Chakula

MHE. PROF. PATRICK A. NDAKIDEMI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Nami nikushukuru mno kwa kunipa nafasi ya kuchangia katioka hoja hii muhimu.

Mheshimiwa Naibu Spika, Itifaki hii ambayo tunaijadili hapa ni makubaliano ambayo yameingiwa kati ya Tanzania na nchi wanachama wenzetu ikiwa na lengo moja kubwa ambalo ni kuhakikisha kwamba tuna-harmonize na kutumia sheria, kanuni ambazo zipo ili kumsaidia Mtanzania ashiriki kikamilifu katika biashara mbalimbali ambazo zinafanyika katika Jumuiya yetu ya Afrika Mashariki. Kwa hiyo, ni kitu muhimu na Wizara husika imefanya kazi kubwa sana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, tuliwa-summon wakatuletea maelezo mengi marefu tu kuanzia Wizara ya Kilimo, Waziri pamoja na wataalamu wake wamejitahidi sana, Waziri wa Mifugo naye alikuja. Tuliiita Wizara ya Mambo ya Nje nao wakaja wakatuelezea mambo ya ki-protokali na Wizara ya Biashara vilevile walikuja. Kwa hiyo, ni kitu muhimu ambacho tunaliomba Bunge kwa umoja wetu tupitishe Itifaki hii. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Itifaki hii ni muhimu sana na itatusaidia kwa kiasi kikubwa kufanya biashara na wenzetu kama ambavyo Waziri ameeleza. Sisi kama nchi ya Tanzania wote tunakubali kwamba kwa sekta ya kilimo tuko vizuri, tuna uwanda mpana sana wa kulima na bidhaa zetu kwenye Jumuiya ya Afrika Mashariki ni nyingi ukianzia mahindi, mbogamboga, maua, maparachichi, matunda, kila kitu tunacho hapa. Vilevile ukija upande wa Wanyama, tunao ng’ombe wengi sana kushinda wenzetu, tunao kuku na samaki wengi kabisa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, mbele ya safari Wabunge wenzangu nawahakikishia tukipitisha Itifaki hii sisi ndio tutakuwa wanufaika wakubwa kuliko hata wenzetu. Kwa hiyo, kwa umoja wetu naomba tukubaliane tuipitishe, ili tuende mbele, pesa ziingie kwenye mifuko ya raia wetu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nawaambia hivyo kwa sababu sisi kama nchi tumechukua muda mrefu sana kujiandaa kuingia kwenye Itifaki hii. Kwa hiyo, kwa mawasilisho waliyofanya Mawaziri ambao nimewataja tuko tayari kabisa. Niombe tu tuliwa-grill sana Mawaziri kuna wakati ambapo tulikuwa hatujajiridhisha na maelezo tulikuwa tunawaambia nendeni mkatuletee ili tujiridhishe tukawa- convince Wabunge wenzetu wakubali Itifaki hii na hilo limefanyika. Kwa hiyo, sisi kama wajumbe wa Kamati tumeridhika kabisa na maelezo ambayo yametoka Serikalini kwamba Itifaki hii ni muhimu na nawaomba tena kwa umoja wetu turidhie ili tuende mbele. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, faida ambazo zitapatikana kwa kuridhia Itifaki hii ni nyingi sana, wenzangu wameshataja na sipendi kurudia lakini mimi kama Mchaga nizungumzie ile ya biashara. Tukiridhia Itifaki hii biashara yetu itaongezeka vizuri, tutafanya biashara ya uhakika ya mazao, mifugo, samaki na tutapata kipato cha kutosha kabisa. (Makofi/ Kicheko)

Mheshimiwa Naibu Spika, Tanzania tuko tayari kusema ukweli kwa maelezo ambayo Waziri ametoa. Nitaeleza vitu vichache tu, tayari wamesha-identify taasisi nyeti ambazo zitasimamia afya ya mimea ambapo wameshaunda taasisi inayoitwa Tanzania Plant Health and Pesticide Authority, itakuwa inashiriki kikamilifu, tuta-compete vizuri na wenzetu wa nchi za jumuiya. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwenye afya ya wanyama kuna taasisi ambazo zipo, mfano Tanzania Veterinary Laboratory Agency, hawa wanashughulikia ng’ombe na wanyama wengine. Kuna TAFIRI kwenye mambo ya samaki na kwenye usalama wa chakula tuna Shirika letu la TBS, wapo tayari kuhakikisha kwamba viwango ambavyo vinahitajika kutekeleza itifaki hii vinatekelezwa vizuri kabisa.

Mheshimiwa Naibu Spika, pia, niseme kwamba sera mbalimbali zipo tayari. Tumemuelekeza Waziri pale ambapo sera hazipo waende chap watengeze sera ili tuendane na wenzetu na tuweze kutekeleza Itifaki hii. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kusema hayo, kuna ushauri ambao pia tuliutoa naomba nirudie; tunaiomba Serikali chondechonde wahakikishe kwamba tunawajengea uwezo wataalamu wetu ambao watashiriki kwenye Itifaki hii. Tuwe na watafiti waliosoma sawasawa watakaokuwa wanashiriki kwenye utekelezaji wa Itifaki hii. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, pia, tunaomba tuwe na uwekezaji wa kimkakati. Tuwe na maabara ambazo ni advanced zinazoweza kupima na kutoa majibu sahihi ambapo hatutakinzana na wenzetu wa nchi nyingine za Jumuiya ya Afrika Mashariki. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kitu kingine ule ugonjwa wa kutokuipatia Wizara pesa ya kutosha. Tunaomba kwenye utekelezaji wa Itifaki hii kwa sababu tutakuwa tunashirikiana na nchi nyingine, Serikali itenge pesa za kutosha ili Profesa Mkenda na wenzake wasikwame kwenye kutekeleza Itifaki hii. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kuna kitu kimoja kwenye udhibiti wa usalama wa chakula. Zamani tulikuwa na taasisi iliyokuwa inaitwa TFDA, haya ni maoni yangu hayajatoka kwenye Kamati; tulii-dissolve ile tukawa na TMDA na sasa hivi TBS ndiye anayekagua kuanzia ukaguzi wa magari kule Japan mpaka huku, ana kazi nyingi sana. Kwa hiyo, naomba sana Serikali ifikirie uwezekano wa kuwa na chombo ambacho kitakuwa kinaangalia usalama wa chakula. Ikiwezekana kwa mfumo mwingine tuwe na TFA nyingine ambayo itakuwa inashugulika na masuala ya kudhibiti ubora wa vyakula ambavyo vitakuwa vinauzwa huko nje. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kusema hayo, naomba kuunga mkono hoja. Naomba Wabunge wenzangu tu-support Azimio hili, ahsante sana. (Makofi)