Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Azimio la Bunge la Kuridhia Itifaki ya Jumuiya ya Afrika Mashariki ya Viwango vya Afya ya Mimea, Wanyama na Usalama wa Chakula

Hon. Athumani Almas Maige

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Azimio la Bunge la Kuridhia Itifaki ya Jumuiya ya Afrika Mashariki ya Viwango vya Afya ya Mimea, Wanyama na Usalama wa Chakula

MHE. ATHUMAN A. MAIGE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kunruhusu na mimi nichangie hoja hii kuhusu Azimio la Bunge la Kuridhia Itifaki ya Jumuiya ya Afrika Mashariki Kuhusu Viwango vya Afya ya Mimea, Wanyama na Usalama wa Chakula.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nianze kuunga mkono hoja hii; na kwa kweli Tanzania imechelewa sana karibu miaka nane imepita tangu wenzetu waliposaini Azimio hili na Itifaki hii kusainiwa na viongozi wa nchi zote za Afrika Mashariki ikabakia Tanzania. Tumepewa sasa mpaka mwezi wa 12 mwisho tuwe tumesaini Itifaki hii. Leo, ni siku ambayo tutajitahidi sana katika kupitisha Azimio hili. Naomba Bunge hili lipitishe Azimio hili kwa sababu lina manufaa sana kwetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, kawaida, huwezi kuongea itu ambacho uko nje. Tulipata matatizo, mahindi yetu yalikwama pale mpakana na tumepata taabu kujadili na wenzetu kwa sababu sisi hatujasaini Itifaki. Lakini, Itifaki hii inapendekezwa na kuridhiwa na Bunge lako Tukufu, na kwa kweli ni muhimu, na tafadhali, Itifaki hii ina maana kubwa sana kwetu sisi.

Mheshimiwa Naibu Spika, mimi nimejipanga kuongelea sehemu mbili. Ibara mbili tu muhimu katika Itifaki hii na ni Ibara ya 6 inayohusu usalama wa chakula na jinsi ya kudhibiti usalama huo hasa udhibiti wa chakula kinachotokana na mazao ya GMO.

Mheshimiwa Naibu Spika, tumesikia Serikali ikionge mara nyingi kwamba Tanzania haitaki GMO lakini hatuna sera hiyo. Sera inayoeleza kwamba Serikali haitaki au sheria inayosema Serikali haitaki GMO. Katika Itifaki hii GMO ni sehemu itakayodhibitiwa na Itifaki hii lakini sasa kama sisi huku hatuna instrument inayoweza kutusaidia kwenda kujadiliana kule itatupa taabu. Kwa hiyo, naiomba Serikali sasa ije na sheria au sera au kanuni instrument bora ya kupeleka kule kwenye usajili wa itifaki hii kwa katibu Mkuu wa Afrika Mashariki ili mazao ya chakula yanayotokana na Genetic Modified Organisms (GMO’s) yaweze kudhibitiwa kuingia nchini kwetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, Ibara nyingine ambayo ningependa kuiongelea ni ile Ibara ya 17 kuhusu Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki kuweza kutunza na kuhifadhi certified ya nyaraka na sheria na Kanuni ambazo Tanzania inaziwasilisha kule. Hili ni jambo muhimu sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, tumeona sababu ya Serikali iliyotoa kwanini kwa miaka nane hatukusaini Itifaki. Sababu kubwa ilikuwa ni kujiandaa, na tumeona maandalizi mazuri sana. Zimetungwa sheria na zimewekwa mamlaka mbali mbali kuhusu usalama wa chakula, mazao ya wanyama pia kuhusu mimea. Upande wa mimea, sheria kadhaa zimewekwa na mpaka mamlaka imewekwa lakini pia upande wa wanyama na mazao yake tumeweka sheria hizo na kuweka vile vile mamlaka au taasisi za kusimamia.

Mheshimiwa Naibu Spika, na hizi ndizo instrument zinazosemwa katika Azimio na zinasemwa katika article ya 17 ya itifaki hii inayosema na naomba noisome, ya kiingereza kifupi tu, mstari mmoja. Inasema “The Secretary General shall register the protocol with all Regional and International Organizations responsible for the implication of this” lakini pia inasema, “this protocol and all instruments of rectified shall be deposited with the Secretary General who shall transmit certified true copies of the protocol and instruments of the rectification to all partner states”.

Mheshimiwa Naibu Spika, ni muhimu Serikali sasa ijiandae na instrument hizi, vitendea kazi hivi ambavyo vitatusaidia kwenda kujadili kule wakati tunapoona kwamba Serikali sasa imesimama na msimamo wake kwamba jamani tuli-rectify/kukubaliana/ridhia mkataba/Itifaki hii tulikuja na vitu hivi. Hizo ndizo nyaraka muhimu ambazo Serikali inapaswa kuziunganisha nazo wakati wa kupeleka itifaki hii ambayo sisi tumeridhia.

Mheshimiwa Naibu Spika, nilitaka kuchangia hilo tu. Kuitaka Serikali iwe Imara katika kuandaa nyaraka hizi na instrument za kufanyia kazi. Ahsante sana. (Makofi)