Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo kuhusu Uchambuzi wa Sheria Ndogo Zilizowasilishwa katika Mkutano wa Pili wa Bunge

Hon. Edward Olelekaita Kisau

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kiteto

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo kuhusu Uchambuzi wa Sheria Ndogo Zilizowasilishwa katika Mkutano wa Pili wa Bunge

MHE. EDWARD O. KISAU: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa nafasi hii na mimi niweze kuchangia kwenye hotuba hii ya Kamati ya Sheria Ndogo na kwanza kabisa niwapongeze Wajumbe wote wa Kamati ya Sheria Ndogo, wakiongozwa na Dkt. Wakili Msomi Mheshimiwa Rweikiza; Makamu Mwenyekiti rafiki yangu Wakili Msomi Ridhiwani Kikwete, Wakili Msomi Ramadhani, Wakili Msomi Edwin na Wajumbe wote wa Kamati hii, kwa kweli wamefanya kazi kubwa sana na wamefanya kazi kubwa ambayo kama walivyosema kwenye taarifa yao, kazi ya kutunga sheria ni ya Bunge la Jamhuri la Muungano wa Tanzania, lakini kwa mujibu wa Ibara ya 97(5) ya Katiba imelipa Bunge mamlaka ya kukasimu madaraka haya kwa mamlaka zingine ndogo zinazotunga sheria.

Mheshimiwa Spika, lakini ni vyema tukafahamu kwamba ikitokea dosari kwenye sheria ndogo, anayepata lawama ni Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa hiyo kazi inayofanywa na hii Kamati ya Sheria Ndogo ni kazi kubwa sana wanafanya kwa niaba yetu wote kwa hiyo niwapoongeze sana. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, na nilikuwa nasoma taarifa yao wanasema mpaka Februari, 2021 sheria ndogo zilizofanyiwa kazi na kuletwa ripoti hapa ni karibu sheria ndogo 915. Ni kazi kubwa sana na wamechambua vizuri sana wakaonyesha dosari mbalimbali zilizoko kwenye sheria nyingi ndogo zinazotungwa na mamlaka hizi za chini. Kwa mfano kwenye ukurasa wa 14 wanasema kuna sheria zaidi ya 15 ilikuwa na shida ya uandishi na ni kweli uandishi wa sheria sio kazi ndogo sana legal drafting ni soma kabisa linafundishwa na watu wengine wanachukua degree zao, kwa hiyo, sio kazi ndogo sana.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo ndio maana Bunge liendelee kufanya hiyo oversight, kuangalia sheria ndogo hizi, ili zisiwe na dosari ya aina yoyote. Lakini ukisoma pia taarifa yao wanasema kuna sheria zaidi ya 10 utekelezaji wake ni mgumu sana kwa jinsi ilivyotungwa na wakati mwingine zinaleta kero nyingi sana kwa wananchi, lakini nyingine hata kuna sheria ndogo baada ya wao kufanya uchambuzi, yanapingana na masharti ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Kwa hiyo sio zile sheria mama tu, lakini hata zinakwenda mpaka zinakinzana na sheria mama, which is very....

Mheshimiwa Spika, nashukuru na Kamati nimesikia kuna sheria ndogo ya Halmashauri ya Kiteto hapa ambaye inatoza watu shilingi 20,000 kwa kweli ni sheria imepitishwa Disemba hapa kwa mujibu wa GN hiyo, hata mimi Mbunge wa Kiteto bado sihifahamu hii sheria vizuri, lakini nitaangalia hii kwa ukaribu zaidi kwa sababu sasa sijui…

SPIKA: Yaani Mheshimiwa hiyo sheria ni kwamba sasa mmegeuza majando yale kuwa ni chanzo cha mapato ya Halmashauri; yaani ndio mantiki yake. Kwa hiyo sasa matokeo yake watu wanakuja kuweka majando Kongwa. (Kicheko)

MHE. EDWARD O. KISAU: Mheshimiwa Spika ahsante sana na jirani yangu unajua mimi na wewe vitu vingi tunashirikiana pamoja na wananchi wetu wa pande zote mbili wanafanya shughuli hizi, lakini lazima tuangalie ili isilete kero kwa wananchi kwa sababu inawezekana wale wanafanya shughuli hiyo labda wanatoza hela nyingi zaidi mpaka Halmashauri labda imefikiria labda ni chanzo cha mapato, lakini ni kweli nakubaliana na kamati tutaangalia vizuri sana ili isilete kero kwa wananchi.

Mheshimiwa Spika, lakini zipo sheria nyingi sana hapa mimi wakati nachangia kwenye bajeti ya Wizara ya Maliasili na Utalii ile kero ile ya kutoza ng’ombe shilingi 100,000 kwa kichwa, nilisema hapa inakinzana na Sheria ya Wanyamapori na nilishamwambia Mwanasheria Mkuu wa Serikali na kwanza hawafahamu kuna ng’ombe unaweza kununua kwa shilingi 100,000. Sasa kama faini inaweza kutozwa kwa shilingi 100,000 sasa si afadhali nikuachie huyo ng’ombe mimi nikanunue mwingine huko sokoni.

Mheshimiwa Spika, lakini kwa kuwa inakinzana na sheria mama tusikubali kabisa madaraka ya Bunge hili na mamlaka hizi za chini zituletee kero za namna hiyo na kutufanya watu waichukie Serikali kumbe mtu mmoja tu ndio ametunga sheria hizo, lakini sheria nyingine ya shoroba au marafiki zangu wa wanyamapori ilitungwa sheria na Bunge wakaambiwa wakatunge regulation kwa ajili ya shoroba hizi.

Mheshimiwa Spika, lakini Bunge likasema muoneshe haki za wananchi kwenye sheria hiyo yaani ndio obligation ya kwanza wao wakaweka masharti kwamba hawaruhusiwi kufanya moja, mbili, tatu wakati interest ya Bunge ilikuwa ni kuona haki gani wananchi wanazo kwenye sheria hizi.

Mheshimiwa Spika, mijadala ya sheria ndogo hizi na naendelea kupongeza Kamati hii na muendelee kutufanyia hii kazi wananchi wengi wanaumia kwa sababu ya sheria hizi ndogo ndogo ambazo zinatungwa na mamlaka za chini bila kuangalia sheria mama ama Katiba ama na sheria nyingine za nchi.

Mheshimiwa Spika, nilikuwa naangalia hotuba hii na kama ulivyosema Sheria ya Tafsiri (The Interpretation Act) kifungu cha 36 kama alivyosema hapa inasema; “Subsidiary legislation shall not be inconsistent with the provisions of the written law under which it is made, or of any Act, and subsidiary legislation shall be void to the extent of any such inconsistency,” inapatikana kwenye sheria hiyo. Kwa hiyo, ni clear kwamba sheria ndogo hairuhusiwi hata kisheria tu infact haitakiwa iwe operational kama itakuwa inconsistency na sheria mama.

Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana na huo ndio mchango wangu kwa leo, ahsante sana. (Makofi)