Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo kuhusu Uchambuzi wa Sheria Ndogo Zilizowasilishwa katika Mkutano wa Pili wa Bunge

Hon. Amour Khamis Mbarouk

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tumbe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo kuhusu Uchambuzi wa Sheria Ndogo Zilizowasilishwa katika Mkutano wa Pili wa Bunge

MHE. AMOUR KHAMIS MBAROUK: Mheshimiwa Spika, nikushukuru kwa kunipa nafasi hii, lakini kwanza nianze kwa kuwashukuru viongozi wetu wakuu wa nchi ambao ni Mama Samia, mwanamke pekee katika Afrika Mashariki anayetuongoza kwa wema sana na kwa heri sana. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini pia nishukuru na nimpongeze Makamu wetu wa Rais Dkt. Philip Mpango kwa kumshauri vizuri mama na leo mafanikio yake tunayaona sana. Lakini nimshukuru pia na kumpongeza Waziri Mkuu kwa namna anavyosimamia Serikali hii ya Mama Samia nikushukuru wewe Mheshimiwa Spika na Naibu Spika kwa namna ambavyo mnavyotuongoza na katika muongozo ambao naushukuru sana ni kwamba leo mimi nipo kwenye Kamati hii ya Sheria Ndogo, najisifia kujua mambo mengi sana katika nchi hii ya Tanzania ambayo nilikuwa siyajui ni kwa sababu tu umechukua jukumu la kunipanga katika Kamati ya Sheria Ndogo, nakushukuru sana, Mwenyezi Mungu akupe uhai mrefu wenye manufaa hapa duniani na akhera, lakini akupe busara na hekima za kuliongoza Bunge hili mpaka pale Mwenyezi Mungu atakaposema basi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sheria ndiyo kitu muhimu sana katika hii dunia na kila kinachofanikiwa katika dunia ni kwa sababu kimewekewa sheria madhubuti, lakini pia kusimamiwa sheria hiyo, ndiyo maana hata dini zetu uislamu, ukristo na dini nyingine zinaendelea vizuri au zinafanikiwa kwa sababu ya sheria. Kwa hiyo, tunashukuru sana leo kwamba sisi tupo kwenye Kamati ya Sheria Ndogo na tunasimamia sheria hizi ili nchi iende vizuri, tunashukuru sana na tunawaomba wanaohusika sasa na sheria wazitekeleze kwa wema sana.

Mheshimiwa Spika, mimi ninamambo machache sana yaani ninayoyaomba katika mchango wangu huu; kwanza katika mijadala yetu mingi sana tulikuwa tunashuhudia kwamba ushirikishwaji wa wadau ulikuwa mdogo sana au ulikuwa hakuna katika kila sheria iliyotungwa, kwa sababu unapomshirikisha mdau maana yake anatoa zile concern zake, zile hisia zako anazitoa kwako kwamba mkituambia hivi tutakuwa kuna tatizo hili, tatizo hili litajitokeza, lakini kwa vyovyote vile ukimshirikisha mdau utapunguza changamoto katika sheria, utapunguza makali katika sheria, lakini jambo hili limekosekana, unakuta kwamba sasa badala ya kwamba tunatunga sheria ili Serikali ipate mapato, lakini iende vizuri unakuta sasa kuna malalamiko ndani ya nchi. Jambo hili tunawaomba sana wale waliokasimiwa madaraka ya kutunga sheria na hasa hizi sheria ndogo ambazo sisi ndiyo tunazisimamia tunawaomba sana waweze kuwashirikisha wadau ipasavyo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, jambo la pili, ambalo mimi ninapenda nishauri na niombe ni kuweka uwiano baina ya sheria mama kwa sababu sheria zote zinazoitwa ndogo maana yake kuna sheria kubwa ambayo tunaita sheria mama, ni muhimu sana tunavyoamini ni kwamba wale wanaotunga sheria ndogo wameaminiwa na tunaamini kwamba wamesomea zile sheria, kwa nini wasifanye ile sisi tunaita murajaa, kwa nini wasirudie kwenye zile sheria mama wakajua kwamba hiki ninachokifanya kinalingana na sheria mama. Sheria mama inasema adhabu ni shilingi 20,000 wao wanasema shilingi 200,000; haiendani kabisa yaani kama kwamba hawakusoma kabisa kwenye ile Katiba au sheria mama, sasa hii inapelekea kuleta image mbaya kufikiria kwamba waliotunga hii sheria walikuwa wana-interest gani kwenye hiyo sheria. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, jambo la tatu, ni kukomoana yaani kuna sheria unahisi hasa kwamba hii sheria imetungwa kwa kuwakomoa watu Fulani, sasa mimi nilikuwa naomba sana wanaotunga hizi sheria wasitunge kwa kukomoa au kwa sababu mtu fulani tu tunataka kumlinda kwenye hiyo sheria. Kwa mfano, hata Mheshimiwa Ramadhani alikuwa anasema hapa anatoa mfano wa shilingi 1,000 lakini hata bajaji wakati mwingine hata, kila ikiingia itoe kwa mfano shilingi 500 au shilingi 3,000 sawa sina gari, ila basi wanatoa 40 sasa hii inapelekea kujiona wale wengine kwamba ni inferiority na hawana haki katika nchi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sasa mimi nilikuwa naomba sana wale wanaopewa madaraka haya ya kukasimu/ waliokasimiwa madaraka kwa ajili ya kutunga sheria ndogo wajitahidi sana watu wengine wasione kwamba tunawakomoa kwa sababu kazi hii waliyopewa, wamepewa na Bunge, wanaliwakilisha Bunge na sisi Wabunge tumechaguliwa na wananchi hao hao ambao wao ndiyo wanawatungia sheria. (Makofi)

Sasa ikionekana sisi leo tumechaguliwa na wananchi, halafu Wabunge wanakuja kupitisha sheria ambayo imewakandamiza wao, wao watatuonaje. Kwa hiyo, nilikuwa naomba sana wanaokasimiwa madaraka wajitahidi sana kuangalia kutokuwakomoa wananchi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kupata fursa hii, naunga mkono hoja. (Makofi)