Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2020 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 pamoja na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022

Hon. Issa Jumanne Mtemvu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibamba

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2020 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 pamoja na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022

MHE. ISSA J. MTEMVU: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi na mimi nichangie kwa hizo dakika tano. Sitoacha kumpongeza sana Mheshimiwa Waziri mwenye dhamana ya wizara hii ya fedha na Mheshimiwa Naibu Waziri wake na watendaji wote wa wizara hii kwa kazi nzuri waliyofanya kutuletea taarifa hii ya hotuba ya bajeti na hali ya uchumi wa nchi yetu ambayo imeeleweka sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kweli nitajielekeza katika maeneo machache na hasa katika mazingira ya Sera ya Mapato pamoja na Sera ya Matumizi. Katika Sera ya Mapato pamoja na kuendelea kutekeleza mpango mzuri wa kuboresha mazingira ya biashara na uwekezaji wa viwango Mheshimiwa Waziri ametuelekeza eneo la mapato ataliangalia sana kwenye maeneo ya kodi, tozo na ada mbalimbali na hapa ndiyo nataka kusema, moja ikiwa ni kodi ya majengo sura 289.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa haraka sana nakubaliana sana, zilikuwepo option nyingi sana, lakini hii moja aliyoichukua Mheshimiwa Waziri yakutumia mifumo ya LUKU ni moja ya utaratibu mzuri sana kati ya taratibu nyingi ambazo zingeweza kuwepo. Na hii kwa sababu ameona uchumi wa sasa unakwenda na teknolojia ya TEHAMA kwa hiyo, akaona ni vizuri tuelekee na njia hiyo nami nampongeza sana. Lakini pia limesaidia wale ndugu zetu wa Chama chetu cha Mapinduzi walikuwa wanatumika vibaya sana katika eneo hili bila tija yoyote kwa hiyo sasa kwa njia hii wanaenda kupumzika na fedha nyingi tutazipata katika eneo hili.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini pia eneo la Ukaguzi wa Umma sura 418, Mheshimiwa Waziri ametuambia hapa nia ya Serikali kupeleka CAG akakague makampuni yetu yale ambayo Serikali ina HISA chache minority interest ni jambo zuri, lakini linachangamoto kwa haraka. Moja ya changamoto; linaweza likatuletea shida kwenye uwekezaji, hizi minority interest tulizonazo kwenye makampuni yale, yale makampuni yana utaratibu wake.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini jambo la pili ambalo ni changamoto; ni katika eneo la Bodi ya Directors, yale yanasimamiwa na bodi zao, bodi zao zina taratibu zake, kwa hiyo nia yetu nzuri kupeleka CAG akafanye kazi mle, lakini hebu tuone kama hizi bodi zao zina uwezo wa kupeleka KPMG na wengine wengi priest house Water, Beroke and Tuch na wengine hebu tuone katika maangalizo hayo ili tuweze kwenda sambamba. Lakini tunajua mpaka sasa CAG mwenyewe hajaweza kukamilisha asilimia 100 ya ukaguzi wa yale ambayo yanatakiwa kwa Mujibu wa Sheria. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nilitaka kusema pia maeneo mawili ya mwisho katika eneo la mapato, moja ni eneo hili la ushuru wa barabara na mafuta, jambo nzuri sana tumeelekeza shilingi mia kwa petrol na diesel sisi tunalifurahia kwa sababu tunaenda kuongeza fedha takribani bilioni za kutosha ambazo zitaenda kutusaidia kwenye barabara zetu za TARURA. Na hii lazima niwaambie wananchi wa Kibamba wafurahie hili walifurahiye jambo hili. Kwa sababu barabara za jimbo lile ndiyo barabara changamoto kwa Mkoa wa Dar es Salaam bilioni hizi zaidi ya 399 zikiongezwa mule maana yake TARURA watapata fedha na fedha zaidi ya bajeti waliokuwa wamewekewa awali, sasa wananchi wategemee barabara zao zitapitika kwa wakati wote. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ipo tozo ya posta na mawasiliano hii ni shilingi 10 hadi shilingi 200 hii nataka niwaambie wananchi wangu waielewe vizuri sana hii inatija na itatusaidia sana, itatusaidia kwa sababu fedha hizi zinaenda kuongeza bajeti ya maji na ndiyo Mkoa wa Dar es Salaam una asilimia 92 za mafanikio katika wizara, lakini asilimia 8 hakuna maji. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nimekuwa nikisema hapa hizi ni shida ambazo ziko ndani ya Kibamba, sasa wakikubali kulipa hizi shilingi 10 hadi 200 maana yake tunaenda kuongezewa zaidi ya bajeti iliyokuwa imepangwa katika wizara hii na maji yanaenda kupatikana vizuri ndani ya Kibamba. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini upande wa sera ya matumizi kwa haraka, nitasema kidogo hapa juu ya fedha zinazotumika mwisho wa mwaka kuzibakiza ndani ya Sekretari zetu za Mikoa kama tulivyokuwa tumeomba sisi wenyewe Waheshimiwa Wabunge jambo nzuri na mimi nalikubali, linamaangalizo. Sheria iko vizuri sheria ya fedha Ibara ya 29(1) hadi (5) inazungumzia unspent amount katika mwisho wa mwaka wa fedha ni vizuri zirudishwe katika mfuko mkuu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, sisi tunasema hazitorudi so zimekwenda kwa kuchelewa vizuri lakini regulation ikatueleze vizuri na ije hapa kwenye Bunge lako Tukufu ili tuweze kuweka vizuri muda sasa ambao itaendelea kubaki kule ili baada ya muda fulani ikishindwa maana ilikuwa tarehe 15 kabla ya mwaka kufungwa watoe taarifa kwa Pay Master General, sasa itaongezwa zaidi hata ya mwezi na kadhalika. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini pia inaleta sura ya kutumia vibaya hizi hela ndani ya deposit, vizuri regulation ikija hapa tuiunge mkono katika mazingira ambayo yatasaidia utimilifu wa nidhamu na maadili ya matumizi ya fedha za Serikali. Najua muda ni mdogo sana lakini niseme vizuri juu ya jambo la DMDP II Dar es Salaam nimeliona Mheshimiwa Waziri kalisemea vizuri ametenga dola za Kimarekani milioni 120. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru naomba niunge mkono hotuba ya Waziri na bajeti ya Serikali ahsante. (Makofi)

NAIBU SPIKA: Malizia sentensi ametenga milioni 120…

MHE. ISSA J MTEMVU: Mheshimiwa Naibu Spika, Dollar za Kimarekani kwa ajili ya Mto Msimbazi na kutengeneza guidon katika hili, lakini wajielekeze sasa kuna Mto Mbezi kuna shida sana Mheshimiwa Waziri katika bakaa utakayokuwa nayo najua re-allocation zinawezekana utusaidie na Mto Mbezi ndani ya Jimbo la Kimbamba nakushukuru sana kwa kuniongezea dakika moja hii ahsante. (Makofi)