Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2020 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 pamoja na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022

Hon. Lucy Thomas Mayenga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2020 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 pamoja na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022

MHE. LUCY T. MAYENGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipatia nafasi ya kutoa na mimi mchango wangu.

Meshimiwa Naibu Spika, kwanza kabisa nianze kwa kumshukuru sana Mheshimiwa Rais wetu na kumpongeza kwa kazi nzuri ambazo anaendelea nazo, na kwa kweli kimsingi kwenye hili nimpongeze sana kwa hatua ambao Mheshimiwa Rais ameichukua ya kuteua wakuu wa Wilaya kutoka kwenye makundi mbali mbali, hongera sana. (Makofi)

Meshimiwa Naibu Spika, hizi siasa wakati mwengine huwa zinatufanya kama vile tunakuwa na hamaki hamaki halafu baadaye tunarudi kwenye mstari. Nilikuwa naomba tu kumwambia ndugu yangu Mheshimiwa Halima Mdee, kwamba kati ya mambo licha ya kwamba Serikali ya Awamu ya Tano ilikuwa anaelezea kwamba si mambo yote yalikuwa perfect kwamba mambo mengine yalikuwa na dosari, mimi nakubaliana nae. Lakini nataka nimwambie kubwa zaidi ambalo hatakiwi kulisahau, kwamba perfect kuliko yote ni wao kuendelea kuwepo hapa Bungeni. (Makofi)

Meshimiwa Naibu Spika, ninaomba kumpongeza Waziri huyu wa Fedha, kaka yangu Mwigulu, Naibu Waziri pamoja na watendaji wote wa wizara hii, kwa kweli wanafanya kazi nzuri sana. Bajeti hii ni bajeti ambayo kwa kweli wananchi wengi wanaipokea positive, ambacho wanakitaka na tatizo kubwa la wananchi; Mheshimiwa Waziri wa Fedha alisema kwamba Watanzania tufunge mikanda. Mimi nilikuwa naomba kumwambia Mheshimiwa Waziri, kwamba Watanzania hawana tatizo la kufunga mikanda, matatizo yao yapo kwenye maeneo mawilili tu. Ni kwamba wananchi wafunge mikanda lakini kinachopatikana kitumike kule ambako kunatakiwa kutumika. (Makofi)

Meshimiwa Naibu Spika, kwa upande mwengine wa pili, ni kwamba wananchi wanasema wapo tayari kufunga mikanda lakini kusiendelee kuwepo na mianya ya upotevu wa pesa katika maeneo mbali mbali. Kwa hiyo hayo yakienda sawa sawa kwa kweli Watanzania hawana wasi wasi na wapo tayari kufunga mikanda.

Mheshimiwa Naibu Spika, lingine ambalo mimi ningependa kushauri hapo, zipo njia ambazo Serikali imesema inataka kuongeza matumizi ikiwemo utaratibu mzima wa kupata fedha kwa njia ya kodi, kwenye simu, kwenye majengo na kadhalika. Sasa mimi naomba kuuliza, hivi tangu siku ile bajeti imesomwa hapa ni nini kinaendelea huko chini kwa watendaji wetu?

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sababu tusipoangalia, Mungu atajaalia, najua kesho bajeti hii itapita. Tusipoangalia tunaweza kujikuta hapa tumekaa tumepanga vizuri lakini baadaye kutakuwa na kero kubwa sana kule chini kwa wananchi. Nilikuwa naomba Wizara zote za Serikali katika maeneo yote ambayo Wizara zote zitaguswa, na hasa pia kwa wananchi wale ambao watakuwa ni wamiliki wa nyumba (wenye nyumba), Serikali iweze kuwa na utaratibu wa haraka na utaratibu mzito sana na wenye kutilia mkazo ili kwamba mambo kule yaweze kwenda sawa sawa.

Mheshimiwa Naibu Spika, ninasema hivyo kwa sababu, ninajua watendaji wetu walivyo. Mpaka sasa hivi kule chini baadhi ya watendaji kwenye baadhi ya maeneo kumeanza ile kama kuamka amka wameanza kukimbizana kimbizana, hatuna data base ya vitu vingi. Sasa hivi hata ukiuliza tuna nyumba ngapi kwenye maeneo fulani watu bado hawana. Sasa vitu kama hivyo kama huna data ya vitu ufuatiliaji wake na utekelezaji wake utakuwa ni ule wa kukamatana, kushikana na kadhalika, Itasababisha chaos nyingi sana. Ndiyo mana nasema kwamba wenye nyumba, na ndiyo mana nasema Wizara nyengine zote tufanye kazi kwa pamoja kuhakikisha mambo haya mengine hayawezi kutokea.

Meshimiwa Naibu Spika, lingine ambalo nataka niliseme, kwenye kurasa wa 117 wa hotuba unasema, kwamba nchi yetu baada ya kuingia kwenye nchi ya uchumi wa kati wa chini, itaifanya nchi yetu kutakiwa kujiendesha kiuchumi bila ya kutegemea kwa kiwango kikubwa misaada na mikopo yenye masharti nafuu, ambayo hupewa nchi zenye kipato cha chini.

Meshimiwa Naibu Spika, hili nilikuwa naomba niseme, kwamba humu ndani tangu watu wameanza kuchangia hakuna mbunge ambaye hajasimama au ambaye hawezi kusema kwamba kwake kuna matatizo ya maji. Hata kama hajasema maji, kwenye masuala ya pembejeo, na kama hatasema embejeo atazungumzia masuala ya barabara na kadhalika.

Mheshimiwa Naibu Spika, nchi yetu inahitaji pesa, sasa tunapataje pesa hizo? Mimi nilikuwa naomba tuwe na njia mbili. Mheshimiwa Rais wetu ameanza vizuri sana, kwamba tusijifungie, ameanza kufungua; na kwe kweli niwapeni Habari njema, hata sasa hivi baadhi ya wafanyabiashara Kariakoo wanasema tunamshukuru Rais wetu, mambo yamebadilika. (Makofi)

Meshimiwa Naibu Spika, sasa kwa kusema hivyo, kama nchi yetu inatakiwa pesa, ziko pesa ambazo zitapatikana, kwa maana ya Serikali kutafuta pesa kwa kutumia vyanzo mbalimbali, lakini ziko pesa nyengine ambazo zitapatikana kwa hizi nafasi ambazo Serikali imeachia ili watu waweze kufanya shughuli zao kama kawaida, kwa kuwawezesha wananchi. Sasa mimi nilikuwa naomba kuishauri Serikali. Yapo mashirika ya wenzetu hapa duniani ambayo yanatoa mikopo kwa riba nafuu.

Nilikuwa naomba Serikali yetu, najua sasa kwamba sasa hivi imejifungua, kuna mashirika ya kiarabu bila ya kujali masuala ya itikadi za dini, twende tukajaribu kuangalia huko kwa wenzetu wana mashirika ambayo yanatoa misaada kwa riba nafuu sana sana. Kwa sababu tunachokitaka, hata kama watu watasema kwa sababu nyengine zozote, tunachokitaka hatuangalii mambo mengine sisi tunaangalia ni jinsi gani tutaweza kuwasaidia wananchi wetu.

Meshimiwa Naibu Spika, lingine ni kuwawezesha wananchi kiuchumi. Mimi nilikuwa naomba Watanzania na watu wengine ndugu zangu tusiwachukie wanfanya biashara, tusiwachukie wafanyabiashara kwa sababu mfanya biashara au mtu mmoja akipata ile chain ikishuka mpaka chini watu wengi wananufaika na mfanyabiashara huyo na kwa hiyo uchumi wa watu utakuwa mzuri kuanzia chini mpaka juu.

Meshimiwa Naibu Spika, ninasema hivyo kwa sababu ninaomba sana Serikali tuweze kubadilisha utaratibu wetu wa jinsi ya kufanya kazi, tuwawezeshe Watanzania. Hivi kuna ubaya gani kwa Mtanzania mtu ametoka huko nje amekuja hapa kuwekeza, wakati wa tender evaluation, tukasema kwamba tunataka walau mtu akitoka nje awe walau na Mtanzania. Kwasababu kwa kufanya vile na tukiwapa masharti hayo yataweza kuwasaidia na Watanzania wenzetu. Kuna wakandarasi, kuna watu wanauwezo mkubwa sana wa kufanya hizo kazi.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini sasa hivi hebu niulize, Stiegler’s Gorge Mtanzania anafanya kazi pale? Najuwa watu watasema wapo lakini anafanya kazi gani? Huku kwenye daraja la Kigongo Busisi jiulizeni Mtanzania anafanya kazi gani? Tukiangalia kwenye maeneo mengine, hata hilo daraja la Tanzanite, pale Salender Bridge, tuangalie Watanzania wanafanya shughuli gani? (Makofi)

Meshimiwa Naibu Spika, tukiwawezesha wananchi kiuchumi, itasaidia Watanzania hao wakiingia huko kupata si tu fedha pia na ujuzi. Siku nyengine Serikali hata ikisema inataka kufanya mradi mkubwa watu wa kufanya kazi hizo watakuwa wameshaingia, wamepata uzoefu na wao wanashiki kuendeleza shughuli mbali mbali za uchumi wa nchi yetu.

Meshimiwa Naibu Spika, tukiendeleza kusema wawekezaji wanakuja mtu anakuja na mitambo yake na ucjuzi wake anafanya, Mtanzania kazi yake iwe kupeleka cement na kupeleka kokoto, hatuwezi kuwawezesha Watanzania kiuchimi.

Mheshimiwa Naibu Spika, niongelee suala linguine, kwa sababu ya muda, suala la ranch za taifa. Ninaomba kuishauri Serikali, ninafahamu kwamba kuna baadhi ya ranch za taifa, bado hatufanyi vizuri. Lakini na ninaomba niseme hivi, hata hizi dhahabu na madini mengine yote haya; kuna wakati Mwalimu Nyerere alisema tuache kwanza mpaka pale tutakapokuwa tayari. Si kila ardhi kwenye hii nchi ni lazima itumike kwa ajili ya matumizi mengine yeyote. Mimi nilikuwa naomba hata, kama hizi ranch hazifanyi vizuri lakini tuwe makini sana sana, hatuwezi kujua zitatusaidia lini na kwenye jambo gani. (Makofi)

Meshimiwa Naibu Spika, lingine nizungumzie suala zima la biashara. Kama ambavyo nimesema kwamba wananchi wawezeshwe kiuchumi; Wizara ya Viwanda na Biashara, unajua wakati mwengine kuna mambo yanakuwa yanafanyika watu wengine wanakaa wanapanga mambo makubwa halafu huku nje wapo ambao wanakuwa kama hawapo, yaani kama tunachokiongea wao hakiwahusu. Ninasema hivyo kwasababu, kama tumekaa tumesema kwamba tukae tujiandae kiuchumi tuwe na bajeti tutafute pesa, tupate pesa kwenye kodi na kadhalika.

Meshimiwa Naibu Spika, ninafahamu kaka yangu Waziri wa Viwanda na Bisahara unafanya kazi nzuri sana pamoja na Naibu wake. Wizara ya Kilimo kaka yangu Waziri wa kilimo pamoja na kaka yangu Bashe wanafanya kazi nzuri sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuna mashirika pale Wizara ya Viwanda, kama CAMARTEC, wapo pale, hivi mimi naomba kuuliza wanafanya nini? CAMARTEC kimsingi ukiangalia kwenye muundo wao, mimi nimeusoma, wanatakiwa waje na ubunifu kusaidia maendeleo katika sekta mbali mbali za kilimo na kadhalika.

Mheshimiwa Naibu Spika, kule vijijini wananchi mpaka leo wanatumia majembe ya mkono, na wao wapo, majembe ya mkono yapo, hata kuwasikia huwasikii. kuna TANTRADE ambao kimsingi wanatakiwa wawawezeshe wafanyabiashara wa ndani na nje, lakini leo hii TANTRADE Mama Samia au Waziri aende pale Kariakoo aende akaangali jinsi gani biashara zinafanyika, kwenda tu kuangalia hawaendi, wanafanya nini? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kuna TIRDO, kuna SIDO. Walau SIDO wanajitahidi, wanafanya kazi mambo yanaonekana, kuna TEMDO, lakini kuna hizi taasisi nyengine ambazo ukiwauliza mnafanya nini hawajui wanachokifanya na wapo wanapata mishahara kwa pesa za Serikali. Nilikuwa naomba Wizara hii ya Viwanda na Biashara, waweze kuamka, hivi vishirika shirika na viataasisi taasisi hivi, Serikali iweze kuviangalia waliundwa kwa sababu ya nini, ili tukijua waliundwa kwasababu ya nini tutajua kama wanafanya kazi na wanastahili kuwepo au wanakula kodi za Serikali.

Mheshimiwa Naibu Spika, sehemu nyingine ambayo naomba sana, Mheshimiwa Waziri wa Viwanda na Biashara aweze kuangalia ni BRELA. Waziri wa Viwanda na Biashara, katika kitu ambacho kitamfanya aonekane kwamba amefanya kazi kwenye Wizara hii au hajafanya kazi ni BRELA, naomba sana afungue macho aende akaangalie BRELA nje na ndani. Najua kama yupo atakuwa ananisikia au hata kama hayupo najua akipata hii habari atajua kwamba imekaakaaje.

Mheshimiwa Naibu Spika, la mwisho, ni kwenye Sekta nzima ya Maji. Pesa zote zinazokwenda kwenye Sekta ya Maji zaidi ya nusu hazifanyi kinachotakiwa.

Nampongeza sana Mheshimiwa Waziri wa Maji kwa kazi kubwa aliyoifanya ya kufumua ma-engineer wa maji kwenye Wizara ya Maji kwa sababu ambacho kilikuwa kinafanyika ni kitu ambacho kwa kweli kinasikitisha sana. Haiwezekani wewe ukawa huko Wizarani, halafu una mtandao wa wizi kuanzia kule juu Wizarani mpaka kule chini kabisa. Wananchi wanalalamika kuhusu upungufu wa maji, mabomba yamepasuka na kadhalika halafu wewe umekaa umepumzika tu.

Naomba sana Mawaziri hawa, Waziri wa Maji, Waziri wa Viwanda, Waziri wa Fedha, Waziri wa Kilimo waendelee kufanya kazi ya kuangalia watu ambao wanawazunguka Wizarani, kwa sababu inawezekana tunaweza tukakaa…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MHE. LUCY T. MAYENGA: Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja. Mambo ni mengi, muda mchache. (Makofi)