Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2020 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 pamoja na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022

Hon. Anatropia Lwehikila Theonest

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2020 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 pamoja na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022

MHE. ANATROPIA L. THEONEST: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru lakini pia nishukuru kwa kupata nafasi ya kuchangia hotuba ya bajeti. Ninachangia hotuba hii ikiwa inaingia kwenye rekodi. Hotuba ambayo kwa mara ya kwanza tunapata Rais Mwanamke. Nadhani imekuwa ni ndoto ya zaidi ya miaka 50 kwa Taifa letu, kwa wanawake lakini kwa watu wote wanaoamini katika mabadiliko na kwa watu wanaoamini katika 50/50. Kwa hiyo, ninamshukuru Mungu leo ninakuwa sehemu ya historia. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimpongeze Mama yetu, ameanza vizuri. Ameanza vizuri nadhani ni kazi yetu Wabunge kumshauri, ni kazi yetu Wabunge kumtia moyo, na ni kazi yetu kumuelekeza pale tukiona mambo hayaendi vizuri. Hiyo, niseme ni moja kati ya commitment yangu mimi pia kama Mwanamke kuelekeza, kutumia mamlaka niliyopewa ya Katiba kama Mbunge kuishauri na kuielekeza Serikali na mimi niseme nitamshauri Mama yangu kama alivyosema kwa staha kuhakikisha anafanya vizuri. Akifanya vizuri, wanawake tutafanya vizuri. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nitaanza kwa kusema malengo tuliyokuwa nayo ya kuwa na Tanzania ya Uchumi wa Kati, malengo tuliyokuwa nayo ya mipango ya miaka mitano, miaka 25 yanaweza yasifikiwe kwa sababu uchumi wetu hauendi kwa namna ambavyo tulikuwa tunatarajia. Uchumi ambao ulitarajiwa katika mwaka 2021 uwe unaenda kwa asilimia Nane mpaka asilimia kumi leo unaenda kwa asilimia Nne (4). Kwa hiyo, matumaini yetu hayawezi kufika kama watu wanavyotaraji. Kama matumaini hayawezi kufika yale ni lazima tuyabadilishe au tuone namna gani tunaweza kubadilika ili tuendane na mabadiliko yaliyoko. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tulikuwa na mpango wa kuhakikisha kipato cha Mtanzania kinafikia at least by 2021 dola 1,500 ambayo ni shilingi 3,469 lakini in reality ni kwamba haiwezekani. Leo kipato cha kawaida ni sawa na shilingi 2,557 ambayo ni dola 1,080. Kwa hiyo malengo hayawezi kufikiwa na sababu zimeelezwa ni kutokana na ugonjwa wa corona. Lakini, nitarudi kusema hatuwezi kuwa na mabadiliko ya msingi kama idadi kubwa ambayo tunapaswa kuwaleta on board ambao ni wakulima hawajafikiwa kwa kiwango kikubwa. Wote tutakubaliana idadi kubwa ya Watanzania ni wakulima ambao ni zaidi ya asilimia 64 lakini ni kiwango gani tumewekeza kwenye kilimo? Ukiwasikiliza Wabunge wanaongea mara nyingi na tuseme maeneo mengi wengi tunatokea kwenye mashamba, kwenye vijiji, watalalamikia namna ambavyo kilimo kinaendeshwa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna baadhi ya maeneo ambayo tunafanya vizuri kutegemea na asili zetu kwamba tuna mvua za kutosha na kadhalika lakini bado hatufanyi vizuri. Kuna watu wanalalamikia mahindi kukosa soko. Kuna watu wanalalamikia kahawa kukosa soko. Kuna watu wanalalamikia alizeti na mambo mengine. Ni kwa kiwango gani sasa wakati ambapo tunaona uchumi kwa trend ya Dunia hauendi vizuri tumejiandaa katika ku-exhaust kwenye masoko ili at least mazao ya kiuchumi ambayo tuliyonayo, mazao ya kilimo yaweze kufanya vizuri kwenye soko. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimekuwa msemaji mzuri sana katika zao la kahawa na ninaamini kama nchi tukiwekeza vizuri kwenye zao la kahawa tutaweza kufanya vizuri kama kilimo kwenye Pato la Taifa. Leo mchango wa kilimo kwenye Pato la Taifa ni asilimia 27, it’s just a peanuts. Ukiwa na watu wa zaidi ya asilimia 64 wanachangia asilimia 27 kwenye Pato la Taifa then you have failed. Nadhani bado tuna kazi yak uji-stretch ili tuweze kuongeza mapato. Kama tunataka kufanya transformation ya uchumi wa Kati na Watanzania wa-feel kwamba wako kwenye uchumi wa kati tunapaswa kuwekeza kwa watu ambao ni wengi zaidi. Takwimu zinaonesha export ya kilimo ni asilimia 24. Narudia, t’s just a peanut, tunahitaji kufanya vizuri na tuna nafasi ya kufanya vizuri tukiamua kufanya hivyo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimeshaongelea suala la kahawa na niseme leo ninavyoongea leo nimeongea na wakulima wa Kagera wa Kahawa, Uganda kilo ya kahawa ni zaidi ya shilingi 2,500 lakini waliouza kahawa Tanzania kule Kagera wanauza shilingi 1,200, siyo sawa! Ni lazima tuangalie ni namna gani tunaweza ku-trade katika hii biashara ya kahawa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Uganda wanauza wapi ambapo sisi hatupaoni? Nchi nyingine zinauza wapi? Lakini siyo hiyo tu, nimeeleza humu ndani nikasema Uhganda na udogo wa Uganda wanalazisha tani zaidi ya 200,000 kwa mwaka lakini sisi tunazalisha tani 65,000 siyo sahihi! Wakulima wa kahawa wamekuwa frustrated wameacha kulima kahawa kwa sababu ya soko ambalo haliko promising. Lengo hapa ninalolisemea ni namna gani wale waliokuwa wengi wanaweza kuchangia kwenye Pato la Taifa na tutaona mabadiliko drastically kimsingi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, wakulima wa mahindi wanalalamika, wakulima wa maharage wanalalamika, tunakosea wapi kama Taifa? Kwa hiyo, mimi niiombe Serikali i-exhaust namna ambavyo tunaweza kutumia masoko ya nje, i-exhaust namna ambavyo tunaweza ku-penetrate kwenye soko na nimeeleza mara moja hapa Bungeni, nikasema Duniani au Afrika Kahawa ya Tanzania inashika namba mbili kwa ubora. Kwa hiyo, bado tuna nafasi ya ku-compete kwa sababu tunazalisha kahawa iliyokuwa bora. Wakulima ambao nimeongelea ni zaidi ya asilimia 64 wanapata changamoto gani? Wakulima hawakopesheki kwa sababu ya aina ya kilimo wanachokifanya na hawakopesheki kwa sababu kilimo chenyewe kiko unpredictable, mtu amekopa fedha zake amewekeza kwenye kilimo lakini huwezi kupata soko huwezi kuuza, kwa hiyo automatic uta-default. Kwa hiyo ninafikiria ni lazima tuangalie namna gani tutaweza kuwasaidia wakulima waweze kukopesheka. Mmeanzisha Benki ya Kilimo lakini ni kwa kiwango gani Benki ya Kilimo imewezeshwa? Ni kwa kiwango gani Benki ya Kilimo inaweza kumkopesha hata mkulima wa kawaida? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukija wale mnaowasema asilimia 64 ya wakulima lakini unakuta wanaokopesheka ni less than three percent kwa hiyo hatuwezi hata ku-achieve tunachokitaka.

Mheshimiwa Mwenyekiti, siyo hiyo tu ya mikopo na nieleze, mfano kama Kagera, bado tuna fursa ya kufanya biashara. Nimekuwa nikiongelea masoko ya kibiashara ya Mrongo na Nkwenda. Hilo ni eneo jingine ambalo budget na niseme bajeti mwanzoni nilifikiria kwamba inategemea walipa kodi asilimia 20 lakini reality ni walipa kodi asilimia tano. Imagine walipa kodi asilimia tano kutegemeza nchi, ina maana the 95 percent wanaangalia asilimia tano, it’s not fair and the vice versa. Kama tuki-convert the 95 percent ambao ni wakulima na wengine tukawawezesha kufanya biashara kuwapa mikopo wakaweza kuzalisha wakalipa kodi hata mzigo wa wale five percent hautakuwa mkubwa. Kwa hiyo, masoko ya kitega uchumi ambayo yapo Murongo na Nkwenda yakiboreshwa tutaweza kufanya biashara vizuri na watu wa Uganda. Hiyo ni concern nyingine naileta ambayo sasa tunapaswa kuangalia katika sekta ya kilimo ili tuweze kuongeza tija. Hilo ni suala la kwanza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia wale wakulima wa kawaida tunawasaidiaje waondoke kwenye umaskini? Nimeona takwimu, kuanzia 2016 takwimu za Serikali zinaonesha umaskini ulikuwa asilimia 28 point something na mliahidi kwamba by 2021 tutakuwa tumefika asilimia 16 lakini reality mabadiliko yamekuwa ni asilimia mbili tu, yaani umaskini umepungua kwa asilimia mbili tu. Hatuwezi kupata mabadiliko tunayoyategemea. Tunawezaje kusaidia kupunguza umaskini, mmefanya kazi ya kupeleka umeme vijijini kupitia REA, ni kitu kizuri na ni namna moja ya ku- stimulate uchumi wa vijijini kwa sababu umeme kama umeme bado unakuwa na impact kwa sababu hata wafanyabiashara watafanya mambo mengine ya kipato.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nijiulize, ni kwa kiwango gani tumejiandaa miradi ya leo iwe sustainable. Leo tumepeleka umeme kwa kasi vijijini lakini huo umeme utakuwa na cost implication baadaye. Kuna nguzo zitadondoka, kuna mafuriko na vitu vingine. Kwa hiyo, tunavyopeleka umeme ni lazima tuangalie to what extent huo umeme utaendelea kuwepo pale vijijini. Lakini tukijiandaa na emergency zinazotokana na umeme, kunaweza kuwepo na radi zikaharibu miundombinu, lakini kunaweza kuwepo na shoti kutegemea na mazingira ya vijijini. Ni kwa kiwango gani tumejiandaa miradi hii ya umeme hairudi nyuma? Hilo ni swali la pili ambalo kama tutaweza ku-sustain tutakuwa tumeweza kupunguza umaskini katika maeneo yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kitu kingine ambacho Mheshimiwa Waziri umeongea kwenye bajeti yako unafutaje msamaha kwenye vifaa vya umeme vinavyotumia umeme wa jua? Leo ukienda kwenye vijiji miradi ya REA ambayo inaelezwa imeenda vijiji zaidi ya 8,000 wakienda kwenye kijiji kimoja wanafunga umeme katika nyumba 20 tu na nyumba zilizosalia zinatumia umeme wa nishati ya jua - sola. Unavyoenda kuongeza kodi maana yake unawarudisha wale watu kutumia vibatari. Unawarudisha wale watu kununua mafuta ya taa. Unawarudisha kwenye maisha yale ambayo wakati tunazaliwa tuliyaona yako hivyo. Mimi ninashauri
Serikali, hebu tafuteni vyanzo vingine vya mapato hiki cha misamaha ya kodi msikiondoe. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. (Makofi)