Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2020 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 pamoja na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022

Hon. Priscus Jacob Tarimo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Moshi Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2020 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 pamoja na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022

MHE. PRISCUS J. TARIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa nafasi ya kuchangia hutuba hii ya Wizara yetu ya Fedha. Nianze kwa kumpongeza sana Mheshimiwa Waziri, Naibu Waziri, wote ni ndugu zangu. Nawashukuru Katibu Mkuu, Naibu Makatibu Wakuu pamoja na Watendaji wote kwa shughuli hii nzito. Naipongeza Serikali kwa kweli, tayari tumeshaona mwanga mbele, tunawashukuru sana, tunawapongeza. Kazi ya muhimili huu huwa ni kuwakumbiza nyie, lakini ninyi wenyewe mmetuonesha njia na tutawaunga mkono. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nitaanza na miradi ya kimkakati. Nimeshawahi kuteta na Mheshimiwa Waziri. Kule Moshi katika miradi ile ya kimkakati, Halmashauri yetu tulipewa Stendi ya Kimataifa pale. Stendi ile imeshameza shilingi bilioni saba za Serikali Kuu. Serikali ya Halmashauri imetengeneza barabara za kuzunguka na kutokea eneo lile na kuzamisha pale zaidi ya shilingi milioni 500, lakini miradi ile imesimama, mwenzangu juzi alitoa mpaka takwimu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naiomba Serikali tumeishaianza kazi, ile fedha tusiifukie. Nasi tuna maombi mawili; tunaomba aidha Serikali itusaidie tumalizie, mradi ule una kama shilingi bilioni 17 au 19, lakini kama Serikali itaona imebanwa, itusaidie kusaini kibali cha kuturuhusu sisi Halmashauri iweze kukopa. Original plan ndiyo hiyo. Kwa hiyo, tunaomba hayo yaweze kufanyika. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusiana na madhara ya UVIKO-19. Dunia nzima hayo madhara yameonekana na kumekuwa na utaratibu wa kutoa kitu kinaitwa stimulus na kiukweli katika nchi yetu, kila mahali wamedhurika, lakini zaidi kwenye utalii na usafirishaji na hoteli. Sasa naiomba Serikali, kama itashindwa kutoa stimulus kwa maana ya kupeleka fedha, maana naona baada ya ile Kamati aliyoiunda mama yetu, naona Benki ya Dunia kama siyo IMF wamesema watatoa dola milioni 400 na kitu. Sijajua mpango wa Serikali na hizo fedha ni vipi kama tutapewa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba stimulus iwe katika maeneo haya. Kama Serikali itashindwa kabisa kutusaidia fedha, basi itusaidie hata kwenye kuhuisha zile leseni bila gharama, lakini ikishindikana hiyo, basi kuna zile charges ambazo zimepanda ndugu yangu wa Arusha jana alilalamika sana, basi zibaki zile za mwaka jana na zile nyingine mpya hasa zile za ardhi zisimamishwe kabisa mpaka hao watu watakapo-recover kwa sababu kuna muda mrefu sana mpaka wa-recover. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa upande huo huo, wafanyabiashara wengi hasa wakubwa na wa kati wanafanya biashara kwa mikopo na wengi wamekopa kwenye mabenki ya ndani. Sasa hatua za mwanzo, zile benki zimepunguza au zimeondoa principal, zimebakiza interest. Sasa kwa kawaida unajua, ile interest ikiendelea kuchajiwa ni umesogeza tu na mzigo mbele unazidi kuwa mkubwa. Naomba Benki Kuu kama inaweza, kama njia ya stimulus, iondoe interest pamoja na principal mpaka angalau mwakani mwezi wa Sita au mwezi wa Kumi na Mbili, hali hii ikishatulia, basi wale wafanyabishara waweze kurudi kwenye biashara zao. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nina lingine la kuishauri Serikali, hasa kwenye sera za uwekezaji. Hatujawa na sera za wazi kabisa ambazo zinaweza kum-support mtu anayetaka kuja kuwekeza hapa. Kwa majarida ya Kimataifa yanasema, katika nchi ambazo hazitabiriki ni pamoja na Tanzania.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa nitatoa mifano michache tu, moja ya sera ambazo zinaweza kuvutia watu ni pamoja na interest za benki na watu wengi wameziongelea. Hiyo ni positive, lakini negative ya sera ambazo zinatukosti ni kipindi ambacho Serikali ilizivamia biashara zenye leseni, tena leseni kutoka za mamlaka tofauti tofauti, viwanda na biashara na BoT zile bureau de change na kuzifunga bila ya maelezo mengi na kunyang’anya zile hela. Sasa hizo sera za namna hiyo ndio zinasababisha tunakuwa nchi ambayo haivutii sana wawekezaji. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba sana kuishauri Serikali. Na sehemu nyengine ambazo tunaweza kusaidia kwenye sera za uwekezaji ni kwenye kodi, sheria zetu za kodi zinamatatizo kidogo. Nilishawahi kutoa mfano hapa kuhusiana na kodi kwenye ile Tanzania Revenue Appeals Act. Ile sura ya saba inatoa haki ya ku-appeal, sura ya 16 wanaku- limit kwamba mambo haya na haya na haya, yaani kwamba ni kama tu ukiwa umeonewa na Kamishna na una-appeal kwenye board. Lakini hiyo pia inaenda kinyume pia na Tanzania Appeal Act sura ya 53 ambayo inatoa haki ya appeal kwa lolote. Sasa hizi ni moja ya vitu vichache ambavyo vinasababisha tuwe hatuna mazingira mazuri ya kuwekeza, kwa hiyo, ningeshauri hilo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, niipongeze Serikali, imetenga fedha nyingi kwa ajili ya kuangalia na kupandisha madaraja kwa watumishi wa Serikali, lakini kwenye hili peke yake halitoshi, lazima tukumbeke wale watumishi ule mshahara wao ni factor ya kodi ya Serikali kwa sababu inakatwa pale.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, ningeshauri, pamoja na hizo juhudi zilizofanyika zote kipo kitu amabacho inabidi tukiangalie, watanzania wote walioajiriwa na waliojiajiri tunajenga nyumba zetu kwa cash hii ni gharama kubwa ukija kuangalia, yaani unapokuta barabarani mtu anaendesha mkokoteni amepakia geti ni mjasiriamali anapambana, ninajua Serikali imeweka mazingira mazuri kupita Watumishi Housing lakini bado. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tuangalie uwezekano wa kuitumia benki kama TIB, maana sitaki kurudi nyuma tuiofufue Tanzania Housing Bank, lakini TIB iwe na mfumo wa kuhakikisha tunawezesha wafanyakazi kujenga nyumba zao, iwe ni security kwao na ni security pia kwenye maeneo yetu ya kazi. Haya mambo ya uwajibikaji na rushwa hayataweza kuisha kwa sababu kila mtu atataka kujenga na nyumba leo imeonekana ni moja ya vitu vitakavyo msaidia kama retirement. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na hayo mazuri ningeshauri hilo, pia kwa Polisi wamekuwa wakihoji, Polisi peke yao ndio ambao hasa kuanzia Inspector, wanatakiwa kustaafu wakiwa na miaka 55, Magereza na Immigration wao wanaenda mpaka miaka 60, sasa wanasema kunini, na wao ni watu wanaofanya mazoezi wako fiti, wanaomba liangaliwe hilo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye eneo la viwanja vya michezo, mimi nina mambo mawili pale, kwanza niipongeze Serikali pamoja na masuala ya nyasi bandia, kwa mfano wa viwanja vya Halmashauri, tunavitumia kama chanzo cha mapato na mambo mengine mengi yanafanyika pale, vikiwekwa viwanja vya nyasi kidogo vinakuwa haviwezi kutumika kwa michezo mengine na vitu vyengine. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye ile mliyosema kwa majiji sita haya majiji ndio yenye viwanja. Hebu tuangalieni halmashauri zenye maeneo kama Moshi, tunauwanja wa majengo, Waziri Mkuu alifika pale akasema atatusaidia, sisi tuko tayari tumeshachimba maji na tumshafanya grading na tumeshaanza juhudi za kuweka majani na tumetenda milioni 300, hebu njooni muanze na sisi, na sisi wenyewe tutakuwa jiji karibuni. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, niwapongeze sana eneo la madini wamefanya vizuri sana, na nimeona kuondoa VAT kwenye kwenye yale madini ambayo yatakuja kubusti viwanda vyetu vile vya uchenjuaji ni hatua nzuri sana. Niongezee tu Serikali iunde kamati ya kwenda kushawishi sasa zile nchi ambazo hayo madini yapo ili yeje yachenjuliwe hapa, ili kubust export yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni wazo ambalo nimeona litatusaidia kuhakikisha vile viwanda vya uchenjuaji vinafanya kazi vizuri. Mwisho kabisa nilishaongelea tena suala la kuangalia kuunganisha bandari, reli na yale maeneo ya muhimu ya kiuchumi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naona mda umeisha nashkuru sana naunga mkoni hoja. (Makofi)