Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2020 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 pamoja na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022

Hon. Judith Salvio Kapinga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2020 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 pamoja na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022

MHE. JUDITH S. KAPINGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama tunavyofahamu vijana katika Taifa lolote duniani ndiyo wadhamini wa Maendeleo wa Taifa hilo yaani they are the trustees of prosperity in the nation. Lakini vilevile vijana katika Taifa lolote ni zawadi kwa Taifa hilo na ndiyo maana kuna msemo unaosema wazee watatangaza vita, lakini ni vijana watakaoenda mbele kupigana au kufariki yaani all the men declare war, but it is the youth must fight and die. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nusu ya watu wote duniani yaani asilimia 50.5 ni vijana chini ya miaka 30; nasema haya kwa sababu Rais wetu Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan siyo Rais wa wastani hata kidogo, she is not an average president anafahamu na anatambua vijana wa Taifa hili ndiyo waliobeba mustakabali wa Taifa hili kwa namna moja ama nyingine. (Makofi)

Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan anatambua makali yetu ya Taifa ya kesho yatazimwa na vijana wa Taifa hili na ndiyo maana juzi katika mkutano wake wa vijana aliahidi mkeka utakaokuja utasheheni na kupambwa na vijana wa Taifa hili. Ila sasa hapa tunamuomba Mheshimiwa Rais aharakishe kwa sababu wananchi mtaani wanalalamika kwamba nazi zimepanda bei (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nasema maneno haya kwa sababu Rais anafahamu nguvu ya vijana na ndiyo maana tarehe 15 alituita pale Mwanza kuongea na sisi na kutupa moyo na kutupa muelekeo wa Taifa hili. Ndiyo maana nasema kwamba Rais wetu Samia Suluhu Hassan she is not an average president at all, anatambua kwamba vijana ndiyo walioikamata dunia hii, kwa hiyo, kwa mantiki hiyo tunamshukuru sana Mheshimiwa Rais kwa mkutano ule, tunasema kwamba sisi kama vijana ametuthamini kweli kweli, sisi kama vijana ametupenda kweli kweli na sisi kama vijana ametujali kweli kweli. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sisi kama vijana tunamuahidi kufanya kazi kwa kuwa ametupa ari ya kufanya kazi, ametupa nguvu, lakini vilevile ametupa hamasa ya kuendelea kum-support kwa kila jambo atakalolifanya kwa sababu mambo anayotufanyia sisi vijana wa Taifa hili ni ya mfano na tunatiwa moyo kweli kweli. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni wazi kwamba kwa bajeti hii ya Serikali ambayo ipo mbele yetu Rais wetu Samia Suluhu Hassan anaupiga mwingi kweli kweli na ninataka niseme hapa kwamba Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan anaenda na trend za dunia inavyoenda. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, yaani kwa lugha moja ama nyingine anaongea lugha moja na ulimwengu wote kwa ujumla na ningependa niwape mfano mmoja; wakati sasa hivi dunia inaenda kwenye deployment ya mtandao wa 5G ambao unaenda kuongeza global economic value ya USD trilioni 13.1 lakini inaenda kuongeza ajira takribani milioni 22.1. Juzi Mkurugenzi wa TCRA alifanya mkutano akatuambia Tanzania kwa mara ya kwanza tunaenda kwenye majaribio ya 5G; mtandao ambao kama leo ulikuwa una-download movie yako ya 20GB kwa zaidi ya lisaa limoja unaenda kui- download kwa sekunde moja mambo ambayo sisi kama Taifa tulikuwa hatufikirii kama tutafika huko, lakini Mheshimiwa Rais wetu Samia Suluhu Hassan anatuonesha mfano wa namna ambavyo tunapaswa kuongea lugha moja na ulimwengu wote kwa ujumla. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, wakati naongea haya Mheshimiwa Rais pia alijiuliza itawezekana vipi tukafikia malengo haya makubwa ya kimtandao kama Watanzania wengi kwa kiwango kikubwa hawana smartphone. Kodi ambayo imefutwa ya VAT labda kwa ambao hawafahamu ukileta simu hapa nchini kulikuwa kuna kodi tatu ambazo simu ilikuwa inatozwa; ya kwanza - custom processing fee; ya pili - railway development fee na ya tatu - VAT ambapo custom processing fee ilikuwa ni 0.6 percent, railway development fee ilikuwa ni 1.5 percent na VAT ilikuwa 18 percent. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, yaani leo ukiingiza mzigo wako wa milioni 10 kodi ambayo ulikuwa unalipia ni asimilia 20.1, kodi ambayo imeondolewa ni asilimia 18 kwa hiyo, kodi ambayo imebaki kwenye simu ni asilimia 2.1 yaani labda niongee kwa lugha rahisi, ukiwa una mzigo wa milioni 10 kodi yako ilikuwa ni 2,010,000 yaani asilimia 20.1, lakini leo hii una mzigo wa milioni 10 kodi ambayo unachajiwa badala ya milioni 2,100,000 ni shilingi 210,000 ni zaidi ya asilimia 97 ya kodi katika hizi simu ambazo zinaingizwa yaani simu janja, vishikwambi na modem imeondolewa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ndiyo maana nasema kufikia asilimia 80 ya watanzania wanaotumia mitandao ifikapo 2025 siyo ndoto ni suala ambalo linatekelezeka na litatekelezeka kabla ya 2025 na sisi kama vijana wa Taifa hili tunamshukuru Mheshimiwa Samia kwa sababu hapa ndipo ambapo tumejiajiri kwa kiasi kikubwa sana. Kwa kweli ndiyo maana naendelea kusema bajeti hii Mheshimiwa Rais anaupiga mwingi kwelikweli. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na kwamba tunashukuru kwa haya yote tungependa tuishauri Serikali masuala machache ambayo inabidi ifanyie kazi; moja, tunaomba Serikali ifuatilie masuala ya fedha za mtandao za simu kwa watu ambao wanafariki, yaani Tigo Pesa, M-Pesa, Halotel Money, Zantel Pesa zote hizo naona kwamba utaratibu haujakaa vizuri na tunaona kwamba kuna fedha zinapotea za watu waliofariki kwenye mitandao ya simu ambazo haziwi claimed. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, utaratibu uliopo sasa hivi tunatambua sheria inasema kwamba, ili uweze ku-claim fedha either katika mitandao ya simu au benki kuna utaratibu wa kufuata ule wa wasimamizi wa mirathi, lakini kwa dunia tunavyoenda sasa hivi tunaona huu utaratibu upo very complex kwa sababu ili uweze ku-claim hela za ndugu zako; kwanza huwezi kuambiwa salio mpaka uende na barua ya kuthibitishwa kama msimamizi wa mirathi na uende na viambatisho vingine ambavyo pamoja na hivyo. Lakini utaratibu huu wa kimahakama unachukua zaidi ya miezi mitatu au sita na sheria inasema kwenye mitandao ya simu line inafungwa baada ya miezi mitatu baada ya hapo hela inawekwa kwenye holding fee. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, siku hizi dunia inapoenda kwa nchi za wenzetu kama Uganda kuna mitandao ya simu ambayo mtu akienda next of kin wake yaani mnufaika wake pamoja na uthibitisho wa marehemu kwamba amefariki na cheti cha kufariki anapatiwa hizi fedha. Tunaomba kwenye suala hili utaratibu uimarishwe ili kuweza kuwalinda walaji, lakini vilevile kuhakikisha fedha hizi hazipotei na wanufaika wa makampuni ya simu hawanufaiki wao peke yao. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu pia hata line ikifungwa ndani ya miezi mitatu kuna fedha zinabaki kule, lakini hakuna utaratibu wa ku-claim fedha hizi kwa walaji ama kwa Serikali. Kwa hiyo, tunaomba suala hili fedha za watu wanaofariki kwa sababu siyo wote ambao wana-claim iangaliwe kwa namna moja ama nyingine ili hata Serikali iweze kuongeza fedha hapo ili makampuni ya simu wasinufaike wao peke yao. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunatambua Mheshimiwa Waziri alisema itakuja sheria ya Data Privacy and Protection Act, lakini tunaona suala hili ni la muhimu sana kuna fedha nyingi sana zinapotea hapa za waliofariki, tunaomba Serikali ifuatilie. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini suala lingine ambalo ningependa nishauri kuhusiana na charge za kwenye mitandao ya simu. Sasa hivi ukiwa unatoka kwenye simu unataka kuchukua hela benki yaani unatumia zile USSD codeā€¦

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MHE. JUDITH S. KAPINGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, samahani naomba nimalizie kwa dakika moja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mfano NMB *150*66# makampuni mengine yote ya simu una-dial nyota hiyo, yaani charge yako inaenda benki yaani uhitaji kuwa na salio ili uweze ku-access benki yako, lakini kwa Vodacom huwezi ku-access mpaka uweke salio la kawaida hata kama ukiwa na bundle hata kama ukiwa na bundle haikubali. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaomba Serikali itusaidie Vodacom wabadilishe utaratibu huu ili sisi tuweze ku-access benki zetu na kama kuna ma-charge waende kwenye benki. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono kwa asilimia 100 bajeti hii na ninakushukuru sana. (Makofi)