Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2020 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 pamoja na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022

Hon. Amb. Dr. Pindi Hazara Chana

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2020 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 pamoja na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022

MHE. BALOZI DKT. PINDI H. CHANA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Naomba kwanza kusema kwamba naunga mkono hoja. Nianze kwa kumpongeza sana Mheshimiwa Waziri wetu Mheshimiwa Dkt. Mwigulu Nchemba na Naibu Waziri Mheshimiwa Eng. Masauni. Kwa kweli nawapongeza sana. Ili itifaki iwe imezingatiwa, nampongeza sana Mheshimiwa Rais wetu, mama jembe, Mheshimiwa Mama Samia Suluhu Hassan. Hongera sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kweli bajeti hii ni bajeti ya mfano. Nina salamu nyingi kutokea katika Mkoa wetu wa Njombe. Wananchi wa Njombe wanashukuru sana, kwa kweli wanasema hii bajeti ni ya kuigwa, ya mfano, kwa sababu inakwenda kuweka pesa kwenye mifuko ya wananchi. Kumekuwa na maboresho makubwa sana upande wa kodi na sasa pesa zinakwenda kuwepo kwenye mifuko ya wananchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, moja kwa moja naanza na suala zima la Madiwani. Suala la Madiwani nimekuwa nikiliongelea sana hapa na ninashukuru Serikali kupitia Wizara imesikia kilio hiki cha posho za Madiwani na Serikali wamesema watalipa. Tunazo Halmashauri grade A, B na C. Hapa kuna point mbili; kuna suala la Serikali kuchukua dhamana ya kuwalipa Madiwani moja kwa moja kwenye accounts zao na vile vile kuna suala la kuongeza kiwango cha posho za Madiwani. Haya ni mambo mawili tofauti. Tutaomba wakati wa kutoa ufafanuzi, haya mambo mawili yaeleweke. Tunapochukua dhamana ya kuwalipa Madiwani moja kwa moja kupitia Serikali Kuu: Je, viwango vinakwenda kubadilika au viwango ni vile vile? Kupitia ALAT, maombi ya Madiwani ni kwamba viwango pia viboreshwe. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyeki, eneo lingine upande wa Serikali za Mitaa ni malipo ya haki ya madaraka kwa WEO na Makatibu Tarafa. Kwa upande watendaji wetu, unakuta mtendaji mmoja ana vijiji tuseme vitatu au vine, analipwa shilingi 100,000, posho hiyo, jambo ambalo nalipongeza sana na kuliunga mkono. Katibu Tarafa, ana vijiji takribani mara nne ya yule Mtendaji wa Kata. Sasa huyu katibu wa Tarafa naye tunamlipa shilingi 100,000 na huyu WEO naye shilingi 100,000.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, ombi kutoka kwa Makatibu Tarafa ni kwamba kile kiwango cha mafuta walichokuwa wanapewa kutoka kwa ma-DAS kibaki pale pale, waendelee kusaidiwa. Kwa hiyo, hii shilingi 100,000/=, wanayopewa Makatibu Tarafa, isiwe mbadala kwamba hawatapewa tena ile pesa waliyokuwa wanapewa kutoka Ofisi za ma-DAS, kwa sababu kazi za Makatibu Tarafa ni zaidi ya kazi ya Watendaji wa Kata. Sasa viwango hapo vinafanana. Kwa hiyo, ni ombi maalumu ambalo tunaweka mezani kwamba kuna kiwango walikuwa wanapewa kutoka ofisi ya DAS kiendelee kuzingatiwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kuboresha hilo, niendelee kuomba Wizara isaidie sana mashine za ki- electronic. Watendaji wetu wa kata wote wapewe zile mashine za kukusanyia mapato za ki-electronic ili mapato yasipotee, tunapojadili bajeti, mabato yaeleweke. Baadhi ya Watendaji wa Vijiji bado wanakusanya mapato kwa mkono (manually), siyo electronic.

Kwa hiyo, tunaomba sana mashine za kukusanyia mapato za ki-electronic ziende vijijini. Katika masoko bado tunakusanya mapato kienyeji. Katika stendi zetu bado tunakusanya mapato kienyeji bila mashine. Suala hili la mashine za ki-electronic tunaomba sana lizingatiwe. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, eneo lingine ambalo pia linaweza lika-boost mapato, tunayo mikoa mipya; Njombe ni miongoni mwa mikoa ambayo ilipatikana dakika za hivi karibuni; Simiyu, Geita, Katavi na mengine. Mikoa hii mipya makao makuu ya mikoa hii mipya, mpaka leo makao makuu mengi hayajawa Manispaa. Tuangalie Makao Makuu ya mikoa hii mipya kama inakidhi kuwa Manispaa. Naleta salam kutoka Mkoa wa Njombe. Njombe tunaomba iwe Manispaa. Halmashauri ya Mji wa Njombe tumeshakaa katika vikao vya DCC na tunakidhi. Tufanyie…

MHE. COSTANTINE J. KANYASU: Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa.

MWENYEKITI: Mheshimiwa Pindi Chana subiri.

Mheshimiwa Kanyasu Taarifa.

T A A R I F A

MHE. COSTANTINE J. KANYASU: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba tu kumpa taarifa mchangiaji. Kwanza anachangia vizuri sana na moja ya mikoa mipya anayozungumza Makao yake Makuu ni Geita Mjini, ambayo imekidhi viwango vya kuwa Manispaa tangu mwaka 2018. Nilikuwa nampa tu taarifa tu Mheshimiwa.

MHE. BALOZI DKT. PINDI H. CHANA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Naipokea taarifa hiyo na nadhani hizi salamu sasa zinazidi kukamilika kwa Serikali. Hii mikoa ni yetu, tunaweza tukasubiri vile vigezo kwamba kwa sababu tumeamua tuwe na mikoa mipya, mikoa hii mipya lazima viongozi wetu wa Kitaifa, Waziri Mkuu aende pale. Sasa mkoa mpya usipoweka airport, Waziri Mkuu anaendaje pale?

MHE. JACQUELINE N. MSONGOZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, Taarifa.

MWENYEKITI: Mheshimiwa Pindi, Taarifa kutoka kwa Mheshimiwa Jacqueline.

T A A R I F A

MHE. JACQUELINE N. MSONGOZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi hii. Nataka tu nimpe taarifa mchangiaji anayechangia sasa kwamba anapoendelea kuchangia, akizungumzia maslahi ya Mkoa wa Njombe asisahau kuzungumzia maslahi ya Mkoa wa Ruvuma jirani yake, kwamba Mkoa wa Ruvuma nao pia ni Mkubwa sana, unahitaji kugawika ili tuweze kupata Mkoa wa Ruvuma na Mkoa wa Selous. Ahsante. (Makofi)

MWENYEKITI: Mheshimiwa Pindi Chana, unaipokea hiyo taarifa?

MHE. BALOZI DKT. PINDI H. CHANA: Mheshimiwa Mwenyekiti, hii ni dalili kwamba upande wa Serikali za Mitaa tukiboresha mifumo mapato yanaongezeka; unapofanya Manispaa au mikoa miwili, miundombinu inaongezeka. Kama pale Njombe tunakuwa na uwanja wa ndege, bosi wetu Waziri Mkuu akija, ana-fly kutoka Dodoma. Ana-land pale, anatembelea mashamba ya parachichi, hatumtoshi by road, kwa sababu anakazi nyingi. Kwa hiyo, tunaoma Mkoa wa Njombe na mikoa ya mingine ambayo ni mipya ipewe Manispaa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, unapokuwa na Manispaa, kuna miradi ya kimkakati. Tuchukulie mfano stendi mpya ya mabasi, ile ya pale Dar es Salaam, Mbezi Luise. Sasa mradi kama ule utawekaje mahali ambapo ni Town Council, siyo Halmashauri ya Manispaa? Maana kuna miradi inaenda kwenye jiji, kuna miradi inakwenda Manispaa na miradi inayokidhi Town Council. Hii mikoa tuliamua sisi iwepo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, ni wakati muafaka sasa tuone namna gani Makao Makuu ya mikoa hii mipya yanakuwa Manispaa kwa maslahi ya Watanzania na kwa faida ya Watanzania. Tuchukulie mfano, pale Njombe ikiwa Manispaa, unakuta bidhaa zote za kilimo kutokea Makete lazima zipite Manispaa. Viazi, chai inayotoka Lupembe, lazima ipite pale Njombe Manispaa. Kule Ludewa kuna Ziwa Nyasa, samaki lazima zipite Manispaa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, inapokuwa manispaa miundombinu, barabara za lami, mabenki uwekezaji unakuwa mkubwa kule ziwani kule ni mbali na tuendelee kuwa wanachama wa maziwa makuu sisi kama nchi tuendelee kuwa wananachama wa great lakes network itatusaidia sana kuweza kufanikisha uwekezaji katika maeneo hayo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, eneo lingine ni suala zima la mchuchuma na Liganga kwa kweli nina salute Mheshimiwa Rais amezungumzia Lichuchuma na Liganga. Lichuchuma na Liganga wanasema kuna political will. Rais wetu mama yetu mpendwa amesema tatizo ni nini leo Waziri amejibu maswali vizuri sana hapa swali lililoulizwa na Mbunge wa Jimbo kuhusu Mchuchuma na Liganga. Tunapongeza sasa tuanze madiwani wanaongelea Wabunge Mchuchuma na Liganga Mheshimiwa Rais Mchuchuma la Liganga sasa shida iko wapi? Hapo sijaelewa kwa hiyo suala hili Mheshimiwa tuimairishe. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, TARURA naunga mkono, TARURA tumetenga hizo milioni 500 kila jimbo tukumbushane TARURA ilikuwepo ipo na itaendelea kuwepo sasa hizo pesa zinapoenda tunatoa shukrani nyingi lakini ionyeshe tofauti isiwe kama wakati ule wa mwanzo wanasema business as usually tuone namna gani pesa hizi zikienda zionyeshe tofauti.

Mheshimiwa Mwenyekiti, eneo lingine ambalo ni muhimu ni mapato yanayotokana na uchumi wa blue. Uchumi wa blue ndani yake kuna bahari, uchumi wa blue ndani yake kuna costal area zote, uchumi wa blue ndani yake kuna maziwa Tanzania peke yake tuna maziwa yasiyopungua tisa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, na haya maziwa lakes great lakes ni muhimu sana haya maziwa, Mungu ametuletea bahari atulipiii hiyo bahari ina samaki tunaweza tukavua kwa wakati wowote kwenye haya maziwa tunavua. Kwa hiyo, muhimu sana tuangalie uchumi wa blue.

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MHE. BALOZI DKT. PINDI H. CHANA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ya pili naunga mkono hoja; ahsante. (Makofi)