Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2020 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 pamoja na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022

Hon. Edward Olelekaita Kisau

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kiteto

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2020 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 pamoja na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022

MHE. EDWARD O. KISAU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa nafasi hii. Leo sauti yangu siyo nzuri sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa kama walivyosema Wabunge wengine, kweli bajeti hii ni ya wananchi. Kwa hiyo, pongezi za kwanza ziende kwa Mheshimiwa Rais wetu Mheshimiwa Mama Samia Suluhu Hassan na za pili ziende kwa Waziri wa Fedha, mzee wa wananchi. Unajua timu ya wananchi lazima pia upende wananchi, si ndiyo bwana! Hongera sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nampongeza pia rafiki yangu Naibu Waziri. Hii timu imejipanga vizuri sana. Zaidi nampongeza Mwenyekiti wa Kamati ya Bajeti ya Bunge na Makamu Mwenyekiti na timu yote ya bajeti. Hii bajeti tunayoisifia bila shaka imepita kwenye mikono mingi sana kuanzia kwa Kamati ya Bunge, wataalam na timu nzima ya Wizara. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, niseme tu, mimi naichukulia Wizara ya Fedha kama ndiyo financiers, ni kama benki hivi. Kwa hiyo, lazima m-scrutinize miradi yote inayoletwa, halafu mwangalie ile ambayo ina tija. Wakati mwingine nikiangalia watafiti, ningefurahi sana kama Wizara hii ingekuwa na thinktanks wa nchi hii wote wawekwe kwenye Wizara ya Fedha. Kwa sababu kila kitu at the end kinakuja kwenu; ili kuangalia baadhi ya miradi mingine na kujua kwamba baada ya miaka mitano ijayo tutaweza kutekeleza ilani ambayo tumeinadi kwa Watanzania.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ya pili, pesa hizi za Watendaji Kata, Maafisa Tarafa, zimefurahisha sana wananchi kule majimboni, big up! Hata hivyo wakati niko kwenye shughuli za mwenge, akaninong’oneza Mtendaji wa Kata, akaniambia, waambie watukumbuke na pikipiki pia na sisi kama walivyofanya kwa Maafisa Tarafa. Hii itasaidia sana. Ni ujumbe tunawapa. Vile vile kupunguza faini kwa boda boda imewafurahisha sana wananchi, big up! (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna hoja nyingine nataka niweke sawa hapa. Kuna Waheshimiwa Wabunge wamekuwa kila wakisimama hapa, wanasema walipa kodi ni milioni mbili na nusu mpaka milioni tatu kati ya milioni 60, is not true. Shilingi milioni 60 unajua ni pamoja na Watoto! Sasa is a bit unfair kusema walipa kodi ni milioni mbili au milioni tatu eti kwa milioni 60 ya Watanzania.

Mheshimiwa Mwenyekiti, data zetu zinasema, watu asilimia 68 ya population ya nchi hii hawalipi kodi kwa sababu ni below age na wengine ni wastaafu. Kwa hiyo, wakati mnasema wanaolipa kodi, I think is good to be fair; tunaongelea watu kama milioni 20 hivi, lakini ni kweli kama ni watu milioni mbili au milioni tatu wanalipa, tujitahidi.

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa.

MWENYEKITI: Mheshimiwa Olelekaita taarifa.

Mheshimiwa Esther matiko.

T A A R I F A

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kumpa taarifa mzungumzaji kwamba ni juzi tu tulipewa semina na wataalam na hata akipitia zile power point walisema wanaolipa kodi ni chini ya 5% of the population. Sasa population ina-include na watoto wadogo hata waliozaliwa leo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kumpa tu hiyo taarifa.

MWENYEKITI: Mheshimiwa Olelekaita.

MHE. EDWARD O. KISAU: Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa taarifa nyingine za kuambiwa na wewe unaangalia. Si ndiyo bwana! Kwa sababu na sisi ni wataalam, watoto hawawezi kulipa kodi, wale waliostaafu hawawezi kulipa kodi. Sasa mimi nasema, kwa wale Waheshimiwa Wabunge wanaosema asilimia ya watu wanaolipa kodi ni milioni mbili kati ya milioni 60, this is what I want to correct. Mimi sizungumzii ile 5% waliyosema hawalipi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ushauri wangu tena, hili Bunge tumeshazungumza hapa, tukasema hili Bunge baada ya miaka mitano, tunataka tujulikane kwamba ni Bunge la wakulima, wafugaji na wavuvi, kwa sababu asilimia 65 ya Watanzania wako huko. Mimi ninachoomba, kwa bajeti zijazo tujipange. Asilimia 10 ya mapato yetu tuwekeze kwenye kilimo. Natarajia huko mbele, tufanye hivyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine Ilani ya Chama cha Mapinduzi tunafurahi sana mmeongeza hela kwenye TARURA, big up! Nasi wengine tumeshafanya hata mikutano na tumeshakubaliana hiyo hela inaenda wapi? Kwa kweli tutasimamia ili hizi pesa zisipotee. Vile vile Ilani ya Chama cha Mapinduzi huko mbele huko tulishakubaliana, tukasema ukurasa wa 71 wa Ilani hii na naomba ninukuu: “kufanya mrejeo wa mgawanyo wa fedha za Mfuko wa Barabara kati ya TANROAD na TARURA.” Ili tupate pesa nyingi kwa TARURA ni lazima tu-revisit hii formula ambayo tulikubaliana isiwe 30 kwa 70 tena, hapana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tukubaliane kwa bajeti nyingine zijazo huko; na kwa kuwa ni commitment iko kwa kwenye ilani, tusema ni asilimia kama ni 50 kwa 50 ama 60 hata iende TARURA na TANROADS kwa sababu tulishakubaliana hivyo. Hii itaongeza chanzo kikubwa kwa barabara zetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna watu wamezungumza kuhusu tozo za utalii. Mheshimiwa Waziri, wenzetu jirani hapa baada ya Covid wao wametengeneza kitu kinaitwa Covid- 19 and Tourism in Kenya; Impact, Measures Taken, Recovery and Pathways. Yaani wanaangalia baada ya janga hili, tukakwama, kwa sababu ni kweli hii Covid-19 imepeleka hii sekta ya tourism down to its knees.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, walitakiwa – na ninyi sasa muangalie from that eye – na hiyo document nitakuletea, wataalam wetu waangalie ili na ninyi muweze kutengeneza a stimulus package, recovery package, ili huko mbeleni tuweze kunufaika. Kwa sababu ni kweli imepelekwa chini zaidi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ushauri mwingine; tumezungumza hapa sana kuhusu mambo ya umwagiliaji. Na tunajua ni kweli ardhi tunayo, mvua tunapata; tusipowekeza kwenye umwagiliaji hatutaweza kumkwamua mkulima. Tuwekeze.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu bajeti hizi, nilikuwa naangalia Wizara ya Mifugo kwa mujibu wa ilani wanatakiwa wajenge mabwawa karibu 95, lakini kwa sababu ya uchache wa bajeti yao, wamepewa mabwawa matano tu. Sasa kwa miaka mitano tukiendelea na trend hii, baada ya miaka mitano tutakuwa tumetengeneza mabwawa 20, na tuli-commit kama 400 hivi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, wakati mwingine tunapotengeneza plans hizi tujaribu kuangalia. In fact, nilishasema wakati mwingine, na ninarudia, labda Wizara ya Fedha iangalie ilani hii projects zote zilizoko kwenye ilani, tufanye tathmini tujue in terms of figures, how much projects zote ambazo tumesema tutafanya baada ya miaka mitano tuzungumze in terms of money ili kila mwaka tujue kabisa tukipata bajeti hii ikaenda kwenye barabara tutaweza baada ya miaka mitano kufanya vizuri zaidi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mfano nilikuwa naangalia hapa kilometa za barabara kwa miaka mitano ni karibu 8,000. Sasa tusipotengeneza bajeti ya kujibu hizi 8,000 kila baada ya mwaka mmoja, tutajikuta baada ya miaka mitano tutashindwa kufanya barabara zote ambazo tumekubaliana. Lakini tuki-cost ilani yetu vizuri itatuongoza, itatoa mwongozo mzuri sana huko mbele tunakokwenda.

Mheshimiwa Mwenyekiti, bajeti hii ni kweli ni ya wananchi. Na hotuba ya mama Samia Suluhu Hassan mimi nawashauri sana Mawaziri muisome vizuri sana ile. Kuna miradi kabisa anataja anasema huu ndio moyo wangu – iko kwenye hotuba yake. Ni vizuri tujielekeze huko ili kiu ya mama yetu kwa Watanzania ikapate kupata suluhu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna hoja nyingine fupi sana nataka nizungumze. Imejitokeza huko mbele kuna mkanganyiko fulani; Wizara ya Ardhi wanawapa kijiji hati, TAMISEMI wanatambua, lakini anakuja bingwa mwingine kule kutoka Wizara ya Maliasili na Utalii anaanza kuwavuruga wananchi wale.

Mheshimiwa Mwenyekiti, concept ya Serikali moja anayozungumza mama yetu; msipeleke confusion kule kwa wananchi. Ninyi mkutane humu, mnyongane wenyewe kule maofisini halafu muelewane kabla hamjaenda kwa wananchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema haya nakushukuru sana na ninaunga mkono hoja. Ahsante sana. (Makofi)