Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2020 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 pamoja na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022

Hon. Dr. Charles Stephen Kimei

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vunjo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2020 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 pamoja na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022

MHE. DKT. CHARLES S. KIMEI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Nashukuru kwa nafasi hii. Mimi pia nimpongeze Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuweza kuja na bajeti yake ya kwanza nzuri sana. Nampongeze Mheshimiwa Waziri Mkuu, Mheshimiwa Waziri wa Fedha, Naibu wake na uongozi wa Wizara kwa ujumla kwa bajeti hii ambayo kusema kweli imezingatia maoni ya Wabunge pamoja na maoni ya wadau wengi na ninaamini kwamba imewafurahisha wananchi kwa ujumla katika nchi yetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, niseme tu makubwa ambayo siyo sana ya kutaka kuingia ndani in detail, lakini niseme mambo matatu makubwa ya kisera. Kwanza, nikiangalia bejeti hii, kusema ukweli ni contractionary budget. Yaani ni bajeti ambayo haitaweza kukuza uchumi kwa kiwango kile ambacho tungetarajia. Kwenye wasilisho la hali ya uchumi wa sasa hivi tumeambiwa kwamba tumekua kwa asilimia 4.8.

Mheshimiwa Naibu Spika, tunasema kwamba tutakua kwa asilimia 5.6 mwaka ujao, 2022. Kwa nini tufikie asilimia 5.6 badala ya kurudi asilimia saba ambapo ndiyo long term trajectory yetu kwa miaka mingi? Wakati tumeshashuka mwaka huu tukapunguza ile kasi, tutawaona kwamba kwenye nchi nyingine ambazo wametekeleza aina fulani ya sera, utaona kama Ulaya zinaanza kurudi na kuwa mara mbili ya ile waliyokuwa wamebajeti mwaka uliopita.

Mheshimiwa Naibu Spika, nafikiri tatizo ni kwamba ukiangalia bajeti, sera zilizomo humu ndani za fiscal na monetary utakuta zote ni contraction. Kwa nini? Kwa mfano, ukisoma bajeti ya mwaka jana, 2020 na ukisoma Monetary Policy Statement ya mwaka 2020 na ya miaka mitabo iliyopita kwa ujumla hutaona tofauti. Wanabaki pale pale kwamba tutakua kwa asilimia saba. Naamini kwamba ndiyo sababu tumebakia tunakua kwa asilimia saba kwa sababu hatubadilishi zile sera za ujumla, zinabakia ni zile. Kwa hiyo, kama hubadilishi ile sera uka-promote growth, ni kwamba hutaweza ku-break through out of your long term hiyo ambayo tumekuwa tunaiendeleza asilimia sita au saba kwa miaka zaidi ya 10 toka wakati wa awamu ya nne na ya tano. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, ninaamini ukweli ni kwamba ukiangalia sekta ya fedha, utakuta kwamba tatizo ni kwamba kama unashikilia inflation kwenye tarakimu kati ya tatu na tano kwa miaka 10 au 20, umejenga fiscal space kubwa sana ya kuweza kukopa na kuongeza fedha za kuendesha miradi katika nchi yetu; ya Serikali in this case, lakini pia inafungua fedha zile zilizo benki ziweze kwenda kwa sekta binafsi.

Mheshimiwa Naibu Spika, ukweli ni kwamba sera hii ya kushikilia inflation kwenye asilimia tatu, maana yake ni kwamba mikopo isikue. Kwa sababu the only way unavyoingiza fedha kwenye uchumi ni kwa mikopo au kwa kuuza fedha za kigeni. Sasa sisi mikopo yetu tumeishikilia, Serikali inakopa kidogo na sekta binafsi inakopa kidogo, kwa hiyo, kwenye uchumi kunakuwa na ukwasi mdogo sana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, unajua Marekani ni nchi ambayo the rate of employment kule Marekani ni 5% au 6% na wao inflation yao inakuwa ni tatu kwa sababu wakichochea kidogo uchumi tayari inflation mambo yatakuwa magumu, hawatapatikana watu wa kufanya kazi. Hapa kwetu tuna unemployment kubwa, kwa hiyo, tunaweza tukaweka mkopo kwa sekta binafsi, sekta binafsi ikaajiri na uchumi ukaanza kukua kwa 7%, 8%, 9% au 10%. Ni very easy. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ukweli ni kwamba utakuta kwamba riba ni zile zile miaka hii yote. Toka mimi nianze kusoma hii serious, riba zinazotokana na Sera ya Fedha ni zile zile za zaidi ya asilimia 10. Ukiangalia nakisi ya bajeti ambayo sasa ni budgetary policy ni nakisi ile. Ukiangalie, yaani kitu unapotaka kuangalia zaidi kwenye bajeti ni nakisi.

Mheshimiwa Naibu Spika, ukiangalia nakisi ya bajeti ambayo sasa ni Budgetary Policy, yenyewe Budgetary Policy ni nakisi ile. Uiangalie yaani kitu unavyotaka kuangalia zaidi kwenye bajeti nakisi. Ukiweka nakisi ndogo maana yake Serikali inajinyima kwenda kukopa fedha kwa sababu, maana yake ni kitu ambacho lazima ukipate nje ya mapato uweze kukiingiza kwenye uchumi wako. Na sasa hivi kwa sababu kuna fiscal space ya muda mrefu ya low inflation unaweza ukakopa hata kwenye Benki Kuu, tumeona sasa wameanza kukopa Benki Kuu kwa kasi kubwa kidogo na hiyo ni kitu kizuri kwa sababu, tunaingiza fedha kwenye uchumi, na watu wakishaleta bidhaa zao wanaweza wakaongezea mikopo yao wakazalisha. (Makofi).

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa hiyo nasema kwamba, bila kufanya marekebisho hapo na niwakumbushe wale waliosoma kidogo, kuna trade off kati ya inflation na growth. Trade off kati ya inflation na, unaongeza inflation unaongeza na rate of wealth growth mpaka a certain level hapo inflation inapokuwa kwamba, ina cause employment imeshafikia mwisho ndio unasema hapa sasa nikienda zaidi nitajikuta napata hasara kwa sababu hata labor cost inakuwa sasa ni structural inflation imejitokeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, nataka kusema kwamba, hii issue ya contraction monetary policy na fiscal policy tuiangalie, nakisi sasa imeshuka wameishusha kutoka asilimia 3 kwenda asilimia 1.5 maana yake Serikali isikope, isitafute fedha mahali pengine ikaingiza kwenye uchumi uchumi ukakua; uchumi hauwezi kukua bila kuwekeza, sasa hiyo ni moja. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, niseme pili,nasema kwamba, ukiangalia kwa upande wa mapato ijapokuwa wana-protect ifike kwenye 23 plus, lakini ukweli ukiangalia mapato ya mwaka huu hayatafikia trilioni 18. Mpaka sasa hivi ukichukua takwimu za mwezi Mei ziko itafikia, nimepiga hesabu haiwezi kuzidi trilioni 18, sasa trilioni tano utazipata wapi? Uongeze ufike 23 trillion?

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo una over estimate, tumesha-over estimate kwenye hii bajeti, lazima tuangalie ni wapi tupate au tuongeze vipato wanavyoshauri wengine kwenye simu, whatever. Japokuwa wanawema ukiweka kwenye simu au ukiweka kwenye miamala hii watu watarudi kule kwenye matawi ya benki, benki zitafurika watu. Watu watasema kwa nini nikachukue kwenye M-Pesa? Nitaenda kwenye benki kwenye matawi nichukue pesa yangu cash kwa kulekule hudai kwa hiyo, sasa tatizo utaongeza mpaka wapi?

Mheshimiwa Naibu Spika, kuna vitu hivi ambavyo vina alternative ways tukivishika tutapata matatizo. Kwa hiyo, nasema kwamba, ukweli ni kwamba, hilo ni tatizo na niseme hivi kuna hii issue kwa mfano kwenye upande wa mapato unpredictability, again mambo ya policy unpredictability yamejiingiza hapo. Kwamba, unaweka ushuru kwa mwaka mmoja, nasema tumeweka huu kwa mwaka mmoja, hii kwa mwaka mmoja, sasa wewe mtu utafanyaje maamuzi ya kuwekeza wakati wewe unajua kwamba, huu ushuru umepata unafuu wa mwaka mmoja tu? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, tunataka ushuru ukae kwa miaka mitatu, minne, kabla hujajigusa. Tatizo hapa tunasema tax current kuwe na tax current ya kwamba, nikipandisha mwaka huu nitakaa miaka mingine mitatu kabla sijapandisha. Kwa hiyo, mtu akitaka kutumia ile opportunity anawekeza kweli kama unpredictability tunazidi kuiongeza hapa haitasaidia sana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, halafu nasema hivi kodi hii ambayo wanakamati wa bajeti wameisema ya LUKU; LUKU, eehee, LUKU ni watumiaji wengi ni wapangaji. Sasa wewe ukaenda kutumia unamtoza mwenye property au unamtoza aliyepanga property?

Mheshimiwa Naibu Spika, tuangalie vizuri namna ya kukusanya. Ni kodi nzuri ni ubunifu, lakini tuiangalie namna ya kukusanya na kitu kama hicho. Lakini niseme hivi kwenye upande wa ku-allocate resources zetu tunaziweka sana kwenye miundombinu, sawa, lakini tujiulize ni kitu gani tunafanya ili watu waanze kuona opportunities kwenye central corridor kwa mfano kwa sababu sasa SGR is coming, lakini hebu niambie toka tuanze kujenga SGR mpaka Morogoro ni watu wangapi wameenda kuanza kuwekeza au hata kuulizia nijenge kiwanda gani? Niweke kitu gani? Niweke shamba gani? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, hamna watu wamekaa kimya tu kwa sababu, kuna vitu vingine ambavyo havijafanyika kuweza ku-motivate production na investment katika hii nchi. Mwisho, but not the last kwa sababu muda tu. Niseme execution, execution unakuja kuona mwisho wa mwaka, unaona hela nyingi zinaanza kutolewa quarter ya tatu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, issue ninayoomba ni kwamba, fedha hasa hizi za maendeleo tujaribu kuzipangilia kwa mpango kwamba, zile ambazo tunakopa tuzikope mapema, ili zianze kutekeleza miradi ya maendeleo tusingojee mpaka quarter ya nne ndio tuanze kupata pesa kwa sababu hizi zinakusanywa kwenye kodi mostly for the current purpose, lakini hizi za maendeleo ni fedha ambazo zinatakiwa zipatikane immediately. Tutafute wale watu wanaotukopesha watukopeshe, tutafute donors wazilete mapema tuanze kuzitumia kwenye miradi ya maendeleo, tuanze kuzi-disburse mara moja hasa kule kwenye wananchi zifike mara moja. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini cha mwisho ni issue hii ya ahadi za viongozi. Tuliahidiwa na Wabunge hapa tulipokuja tuliahidiwa kwamba, zile ahadi za viongozi kwa wananchi wetu kule kwenye majimbo zitaorodheshwa ziwekwe kwenye vipaumbele tuambiwe kwamba, hii ya kule Vunjo itatekelezwa mwaka wa tatu. Nikitajiwa hivyo nitasema haleluya, lakini kama hatujajua kwamba, zile ahadi zimewekewa mchakato gani wa kutekeleza itakuwa kwamba, tunabakia tunaenda kule wataanza kutupa mawe wewe ulizungumza hivi, tupeni tuende na hicho kitu. Nimesema hapa kwa sababu najua ni kwenye mambo ya execution. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba unisamehe kwa kuzidisha kidogo, lakini nataka kusema naunga mkono hoja hii vizuri sana. Na haya niliyosema ni mambo tu ya kuboresha tunaenda mbele, ahsante sana. (Makofi)