Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Esther Lukago Midimu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. ESTHER L. MIDIMU: Mheshimiwa Mwenyekiti, Mkoa wetu wa Simiyu una mito miwili muhimu sana. Mito hiyo ni Mto Simiyu na Mto Duma. Kwa miaka ya hivi karibuni mito hiyo imekuwa inakauka muda mfupi tu baada ya mvua za masika kwisha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tatizo kubwa, miti mingi imekatwa ili kutengeneza mkaa na kuni kwa ajili ya kupikia na hii ni kwa sababu hakuna chanzo kingine cha nishati. Imefika hatua akina mama wanatumia kinyesi kupikia, kitu ambacho kinasababisha macho yao kuwa mekundu. Hii ni sababu ya lawama na kusingiziwa ni wachawi na hatimaye kuuawa kwa kukatwa na mapanga.

Je, Serikali ina mpango gani mahususi na wa dharula ili kuleta nishati mbadala na wenye gharama nafuu ili kuwanusuru akina mama wenzetu wa Mkoa wa Simiyu?

Mheshimiwa Mwenyekiti, watalii wengi wanatokea Arusha kuelekea Serengeti, lakini sisi Mkoa wa Simiyu hatuna barabara wala mlango wa kuingilia Hifadhi ya Serengeti. Je, ni lini sasa barabara hiyo itajengwa ili wananchi wa Mkoa wa Simiyu nao wapate fursa ya kuitumia hifadhi ya Serengeti na kufurahia urithi wa Taifa letu?

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa upande wa Mkoa wa Simiyu miradi ya barabara hatuioni na wakati kuna Hifadhi ya Taifa ya Serengeti na Pori la Akiba la Maswa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mazao yatokananyo na nyuki yana mchango mkubwa sana katika uchumi wa nchi yetu, pia kuna nchi hapa Afrika, kwa mfano Ethiopia, mazao ya nyuki yana mchango mkubwa sana katika GDP. Tanzania ina mazingira mazuri sana kwa ufugaji wa nyuki kwa mfano Mikoa ya Katavi, Rukwa, Tabora na Kigoma pamoja na Singida, lakini hata hivyo sioni mpango mkakati wa kuliendeleza jambo hilo. Vilevile hakuna watalaam wa nyuki kwa sababu hata chuo kilichopo Tabora ni kidogo utadhani ni chuo cha mtu binafsi. Tunaomba chuo hicho kiongezewe miundombinu ili kiongeze udahili. Serikali iendelee kuchukua hutua madhubuti ya kuwezesha chuo hiki na kutengeneza ajira kwa vijana na kuliwezesha zao hili kuongoza Kimataifa.