Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Bernadeta Kasabago Mushashu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. BERNADETHA K. MUSHASHU: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kumpongeza Waziri, Naibu Waziri, Katibu Mkuu na Watendaji wote wa Wizara ya Maliasili na Utalii kwa hotuba nzuri ya bajeti na kazi nzuri inayotekelezwa na Wizara. Ukiondoa kipindi hiki ambapo dunia nzima imeathiriwa na Covid 19, sekta hii ni kati ya sekta zinazofanya kazi nzuri sana Tanzania. Hongera.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mkoa wa Kagera kuna mapori matano yaliyopandishwa hadhi na kuwa Hifadhi za Taifa za Burigi - Chato, Ibanda -Kyerwa na Rumanyika -Karagwe. Hifadhi hizi ni mpya, bado zinahitaji uwekezaji mkubwa ili kuweza kufikia lengo lililokusudiwa ya kuimarisha sekta hii na kuongeza pato la Taifa. Hivyo ili kuchochea ukuaji huu katika Hifadhi Mkoani Kagera napendekeza:-

(1) Tuletewe wanyama wengi zaidi ili waongezeke, wazaliane hifadhi zivutie watalii;

(2) Hifadhi hizi zijengewe miundombinu ya barabara na mageti yaongezwe, ili zipitike wakati wote;

(3) Tujenge Hoteli nzuri, makambi na Lodge za kudumu.

(4) Hifadhi zilipoanzishwa vijiji jirani hawakupatiwa elimu ya kutosha. Napendekeza viongozi na wanavijiji wapewe elimu ya Uhifadhi, Ulinzi shirikishi, ni faida gani wao watazipata kutokana na hifadhi hizi wa mkoani Kagera?

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna tatizo kubwa la wanyamapori kama tembo, ngedere kuingia kwenye maeneo ya wananchi, wanaharibu mazao na kuua wanadamu. Wakulima wanapata hasara na vifo vinatokea mara kwa mara. Serikali ifanye yafuatayo: watafute njia ya kuzuia tembo kuingia katika maeneo ya wakulima ya kudumu; tutumie technologies za kilo kuwaondoa tembo hawa; wanyama waharibifu kama ngedele nyani wamezaliana sana, ni wengi vijijini, wanaharibu sana mazao ya wakulima. Napendekeza wavunwe, wapunguzwe ili kupunguza hizi athari. Tufufue kitengo cha Vermin Control Unit.

Mheshimiwa Mwenyekiti, viwango vya fidia na vya kifuta machozi ni vya siku nyingi, ni vidogo sana, havina uhalisia, virekebishwe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sekta hii ya utalii ni sekta ya kipaumbele ya Serikali mbayo inachangia kwa kiasi kikubwa pato la Taifa. Sekta hii imeathiriwa sana na Covid 19. Serikali ichukue hatua za haraka kunusuru sekta hii. Tunaiomba Serikali ianzishe Stimulus Package ili kunusuru haraka sekta hii. Serikali itoe fedha kuwasaidia wafanyabiashara wenye hoteli, wasafirishaji na Wizara ili kunususuru sekta hii haraka sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashauri, kama nchi tuwe na Mfuko wa Dharura kuweza kutatua matatizo kama haya yakijitokeza. Mfuko uwe wa Kudumu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Wizara iwe na mipango kabambe ya kuchochea utalii wa ndani. Kutoka viwandani, mashuleni, wakulima, wavuvi, watumishi na kadhalika, wote wahamasishwe na kuwekewa utaratibu ili washiriki. Itasaidia kuongeza namba ya watalii nchini na pato la Taifa.