Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Dr. Oscar Ishengoma Kikoyo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muleba kusini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. DKT. OSCAR I. KIKOYO: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kupata nafasi hii kuchangia Wizara hii. Niungane na wenzangu Wabunge kuwapongeza Mheshimiwa Waziri, Naibu Waziri na watendaji wote wa Wizara hii. Kwenye hotuba ya Mheshimiwa Waziri ameongea mazao mapya ambayo wameyaongeza kwa ajili ya kuongeza chachu na ufanisi katika Wizara ya Utalii, nayo ni utalii wa uvuvi na kujiburudisha, utalii wa kula Wanyama pori, utalii wa kula chakula porini na utalii wa kupiga makasia. Nawapongeza sana kwa hilo.

Mheshimiwa Naibu Spika, nadhani wengi tumetembea katika nchi za wenzetu. Kwa mfano ukienda Misri, pamoja na kuangalia zile pyramids lakini jioni mkitoka kuangalia yale ma-pyramids mtakwenda Mto Nile, mtapiga ma-cruise, kuna ngoma za asili, mtakula chakula, inaongeza value kwenye package ya utalii.

Mheshimiwa Naibu Spika, sisi Tanzania tutumie na sisi akili zetu jamani, tusibakie kwenda kuangalia wanyama sijui wapi, kuangalia sijui Tarangire, sijui Serengeti, tuongeze value kwenye kuangalia wale Wanyama, jioni hawa watalii wanaangalia nini, wanafanya nini.

Mheshimiwa Naibu Spika, ukienda Hongkong pale ile Hongkong ilivyokaa ina vilima mithili ya Mji wa Mwanza, lakini vile vilima wamehakikisha wamevitunza na ni sehemu ya vichocheo vya utalii, ile jioni mnapanda kwenye mlima mnaangalia Hongkong pale chini. Angalia Mji wetu wa Mwanza tunautumiaje kwenye sekta ya utalii, tumebaki na sekta ya utalii ambayo hatujaijumuisha na mazingira ya maeneo ya utalii wetu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, tuna ziwa Victoria pale na maziwa mengine tunayaunganishaje kwenye sekta ya utalii kwa mfano Ziwa Victoria, Mheshimiwa Waziri wa Uchukuzi yupo pale, kuna kipindi pale Bukoba walikuwa wameandaa kuwa na cruising party kipindi cha mwisho wa mwaka, lakini ukienda kuazima meli ile ya Victoria wanakwambia hii siyo kazi yetu, siyo kazi ya utalii hii, ni kana kwamba Wizara ya Utalii inajitegemea, Sekta ya Uchukuzi inajitegemea lakini tunapaswa kuwa holistic approach tunapokuja kwenye sekta ya na masuala yote ya utalii. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Hifadhi ya Burigi Chato, nawashukuru Serikali ile hifadhi ilikuwa ni majanga miaka ya nyuma, tusingepita mle, lakini kwa kuanzisha hii hifadhi imetuongezea usalama watu wa kanda ya ziwa. Nimwombe Waziri Burigi ndiyo imebeba maana ya ile hifadhi. Tuna Ziwa Burigi pale ambalo kwa bahati nzuri kama hawajawahi kufika, lakini najua hawawezi kufika kwa sababu lile eneo la Burigi halifikiki, hakuna barabara nzuri, lakini pili kama mchangiaji mmoja alivyosema hakuna mawasiliano.

Mheshimiwa Naibu Spika, nimwombe Mheshimiwa Waziri, wakati anakuja ku-wind up atuambie wana mkakati gani kuhakikisha kwamba lile Ziwa Burigi linafikika. Watalii watakapokuja na nina uhakika, watalii wengi watatokea Bukoba kwenda kwenye Hifadhi ya Burigi Chato, tuhakikishe upande wa Muleba tunakuwa na gate kubwa la kuhakikisha kwamba watalii watakapotoka Bukoba kwenda Burigi Chato wanapata sehemu ya kuingilia, badala ya kuzunguka kwenda Biharamulo kwenda sijui Chato, waingilie eneo la Muleba. Mheshimiwa Waziri atatupa maneno yakeo atakapokuja kuhitimisha hoja yake.

Mheshimiwa Naibu Spika, la mwisho, wakati nachangia Wizara ya Mifugo, niliongelea hili suala la kuchukua mifugo. Bahati nzuri wewe mwenyewe ni Mwanasheria, Waziri ni Mwanasheria, wanajua maana ya sheria. Inapokuja katika Wizara hii, mifugo imeingizwa kwenye Hifadhi mwananchi wangu nilimwongelea katika Wizara ya Mifugo…amekamatwa, amefunguliwa kesi ya kuingiza mifugo kwenye hifadhi, ameshinda. Siku hiyo hiyo amekamatwa kwa kosa lingine eti ameharibu uoto wa asili. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kama mahakama imesema arudishiwe mifugo yake kwa nini watu wa Wizara hii wanakaa na mifugo ya wananchi jamani! Wanafanya wananchi wachukie Serikali yao kana kwamba Serikali imewaibia mifugo yao, lakini ni watu wachache. Tunaomba Mheshimiwa Waziri atusaidie wanatupatia wakati mgumu kwenye majimbo. (Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

NAIBU SPIKA: Ahsante sana.

MHE. OSCAR I. KIKOYO: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana na naunga hoja
mkono. (Makofi)