Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Innocent Lugha Bashungwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Karagwe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. INNOCENT L. BASHUNGWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninamshukuru sana Mheshimiwa Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa hotuba yake nzuri na iliyosheheni mipango mizuri ya uchumi wa viwanda hapa nchini. Katika hii ninapenda kusisitiza Serikali ihakikishe uchumi wa Viwanda unajielekeza kwenye kuongeza mnyororo wa thamani (value chain) kwenye shughuli za asilimia 70 ya Watanzania ambazo ni kilimo, mifugo, uvuvi na Biashara ndogo na kati (SMEs) The focus should be at the bottom of the population pyramid ndipo kuna asilimia 70 ya wananchi au zaidi. Kwa kufanya hivi uchumi wa wananchi hawa ambao karibu wote ni maskini utakuwa na malengo ya nchi yetu wa kufikia uchumi wa kati (MIC) ifikapo 2025 yatafanikiwa. Aidha, tutakuwa tumepata uchumi wa viwanda wenye tija na weledi kwa Watanzania walio wengi. Ninaomba sana Serikali izingatie ushauri huu. Ninashukuru Mheshimiwa Waziri Mwijage kwa kutambua hili katika hotuba yake.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Karagwe ni moja ya Wilaya nchini ambazo zinazalisha mazao mengi na kusaidia kulisha Watanzania hasa wanaoishi Mjini. Pamoja na mchango huu mkubwa wa kuzalisha kwa wingi mazao mengi hasa maharage na kahawa, sijaona Serikali ikileta wataalamu kuwapa mafunzo wakulima kuhusu namna ya kulima kwa tija na kuwasaidia mikakati ya kuwaunganisha na masoko. Kushindwa kufanya hivi kwa Serikali kumesababisha mazao kuharibika mashambani, (Post harvest loss) kwa miaka mingi kwenye Wilaya ya Karagwe na kwingineko Nchini. Je, kwa nini Serikali haijatenga bajeti ya kuwasaidia wakulima wa Karagwe na mafunzo ya kufanya kilimo cha biashara na kuwapa mikakati ya kuwaunganisha na masoko.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli aliahidi wananchi wa Kagera kwamba Mkoa utajengwa uwanja wa Kimataifa kwenye eneo la Omukajunguti lakini katika hotuba ya Mheshimiwa Waziri Mwijage sijaona wala kusikia fedha zilizotengwa kwa ajili ya kutekeleza ahadi hii ya Serikali ya Awamu ya Tano.
Aidha, sambamba na hii ahadi ya Mheshimiwa Rais, pia wananchi wa Kagera waliahidiwa na Mheshimiwa Rais Special Economic Zone (SEZ) sambamba na mipango ya uwanja wa ndege wa Kimataifa. Mkoa wa Kagera kijiografia umezungukwa na Miji mikubwa ya Afrika Mashariki ambayo kuwepo kwa SEZ na Uwanja wa Ndege wa Kimataifa utakuza biashara za Mkoa wa Kagera na kusaidia kukuza uchumi wa Nchi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba Mheshimiwa Waziri atakapo simama kujibu hoja za Wabunge name nijibiwe katika SEZ na uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Omukajunguti.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imewaahidi wananchi wa Kagera Kiwanda cha kusindika nyama kwa miaka mingi sana. Kuna eneo kubwa lililotolewa kwenye Ranch ya RAHCO ya kitengule takribani hekta 36,000 kwa mwekezaji huyu ila hakuna uwekezaji wa kiwanda cha nyama mpaka hivi sasa. Hii haikubaliki na ni mfano mzuri wa matumizi mabaya ya ardhi. Je, kwanini Serikali inatoa maeneo kwa wawekezaji ambao ni waongopaji na wakati kuna Watanzania wanakosa maeneo ya kufanya uwekezaji katika sekta ya mifugo? Naomba tamko la Serikali juu ya uwekezaji wa Kiwanda hiki cha kusindika nyama kwenye Ranch ya Kitengule. Aidha, Mkoa wa Kagera tuna maziwa mengi sana. Tunaiomba Serikali ituletee Wawekezaji wa kujenga kiwanda cha kusindika maziwa. Jirani zetu wa Rwanda wana ardhi na hali aya hewa inayofanana na Kagera.
Rwanda inasindika Maziwa yanaitwa Nyamo UHT na yanauzwa Afrika Mashariki nzima, Iweje Kagera ambayo ina ardhi kubwa kuliko Nchi ya Rwanda na tuna rasilimali ya ardhi na hali ya hewa ya kuwezesha uzalishaji wa maziwa mkubwa tusipate wawekezaji wa kusindika maziwa? Tunaiomba Serikali iweke diary zone Mkoa wa Kagera na miundombinu stahiki iwekwe ili kuvutia uwekezaji huo. Ninaomba tamko la Serikali kuhusu hoja hii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, gharama ya saruji Mkoa wa Kagera ni mara mbili ya gharama ya saruji Mkoa wa Dar es Salaam. Je, Serikali ina mpango gani wa kuvutia uwekezaji wa saruji kwenye Kanda ya Ziwa ili wananchi wa Mikoa ya ukanda huu wapate saruji ya bei nafuu kama wenzao wa Kanda ya Pwani?
Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.