Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Martha Nehemia Gwau

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. MARTHA N. GWAU: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi hii ili niweze kuwa mmoja wa wachangiaji katika Wizara hii muhimu kabisa ya Maliasili na Utalii.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kwa moyo wa dhati kabisa na kipekee nipongeze Wizara hii kuanzia Waziri mwenye dhamana, Naibu Waziri na wataalam wote waliopo katika Wizara hii, kwa jitihada madhubuti wanazozichukua kuhakikisha kwamba suala la utalii Tanzania linatangazwa vilivyo na pia tunapata watalii wa kutosha. Naomba nitoe pongezi hizo za dhati. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, pia, naomba nijikite kwenye utalii; utalii ni sekta muhimu sana kwa nchi yetu ambayo inatuingizia pato, lakini pia vijana wetu wanapata ajira, lakini pia pesa za kigeni, kwa hiyo unaweza kuona umuhimu wa sekta hii ya utalii nchini kwetu ilivyokuwa kubwa sana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nijikite kuelezea watalii wanaotoka nje kuja Tanzania. Mikakati ya Serikali kutokana na hotuba ya Mheshimiwa Waziri ni kujitahidi kuhakikisha namba ya watalii wanaotoka nje kuja Tanzania inaongezeka kwa miaka mitano ijayo. Mikakati hii ni mizuri na naomba nimpongeze Mheshimiwa Waziri. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, mikakati hii itafanikiwa tukifanya mambo matatu; cha kwanza lazima tukubali kuwa creative na innovative. Lingine, tukubali kuwa competitive, lazima tukubali kushindina na wenzetu na la tatu lazima tukubali ku-learn from others, waliofaulu walifanyaje na sisi tunafanyaje, kwa nini tunakwama hapa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ukizingatia Tanzania ni ya pili kuwa na vivutio vingi duniani, lakini kwa nini Tanzania siyo ya kwanza au ya pili au tatu, au ya tano kwa namba ya watalii wanaoingia Tanzania, ina maana hapa kuna shida ambayo hatujaitatua vizuri na ndiyo maana tunashindwa kufikia ile idadi ya watalii kuwa wengi kwetu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, tunaweza tukajifunza kutoka kwa wenzetu wa Comoro, Egypt na South Africa, wamefanya nini, kwa nini wenyewe wanapata namba kubwa ya watalii wanaokuja nchini mwao na sisi Tanzania hatupati namba hiyo, lazima kuna shida ambayo inabidi tujifunze na tukubali kubadilika. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kingine, napenda kuongelea sana quality of service inayotolewa baada ya wageni kuja Tanzania. Mheshimiwa Waziri na timu yake wanaweza wakatangaza matangazo yote ya promotion za utalii watu waje Tanzania. Wanaweza wakatumia wacheza mpira, ma-celebrity tofauti tofauti, lakini, je, wameshawahi kujiuliza swali mtalii akifika hapa anapata huduma inayostahili? The quality of service is it equal to value of money? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sababu kama anakuja kuangalia tembo Tanzania na hapati huduma nzuri na tembo huyo huyo yupo Kenya ina maana ata-opt kwenda kwenye service nzuri ya Kenya na asije Tanzania. Kwa hiyo tukitoa quality service tutamvutia huyu mtu aseme Kenya kuna tembo mfano, Uganda kuna tembo na Tanzania kuna tembo na opt kwenda Tanzania because I will get a quality service na nitapata huduma nzuri inayotakiwa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nime-highlight mambo machache ambayo naona kama ni tatizo na of course tumesafiri sana unakutana na watu kwenye ndege popote huko duniani, wanakwambia Tanzania mnavivutio vizuri, lakini kuna shida kwenye huduma zenu. Kwa hiyo naomba Wizara wavi-note; cha kwanza, service provider wetu waiter, waitress, guide, chefs na receptionist hawa ni face ya watalii wote wanavyoingia nchini. Hawa watu ni lazima wapewe mafunzo mbalimbali, training mbalimbali ya kuhakikisha kwamba mtalii anapofika hapa yeye ndiyo kioo cha kumpokea. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya Waziri na Naibu na Waziri na timu yake kumtangazia kuna Ngorongoro Tanzania, akishafika anakutana na nani, anakutana na service provider atahitaji kulala, anahitaji kula, anahitaji kutembezwa hawa watu Wizara inawaangaliaje, ili wao watoe huduma nzuri, huyu mtalii aridhike, aseme badala ya kwenda Kenya nataka niende Tanzania kwa sababu nitapata huduma nzuri. Hilo ni tatizo (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, tatizo la pili ni lugha, watoa huduma wengi Tanzania wanaongea Kiswahili na Kiingereza, lakini wangeongeza lugha ya tatu kwa mfano, Wachina wengi wanapenda kwenda kutembea Thailand kwa nini? Ina maana kule wanaongea Kichina, kuna mtu anaye-guide anaongea kachina, anavutika kwenda kule, lakini barabara zetu ni mbovu za kwenda na ndani ya utalii. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kingine network, communication network, siku hizi kuna kitu wanaita live, mtu akiwa kule kwenye mbuga za wanyama ataonyesha live nipo na simba kwa hiyo network communication iboreshwe…(Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

NAIBU SPIKA: Haya ahsante sana.

MHE. MARTHA N. GWAU: Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kusema haya, naomba kuunga mkono hoja. Ahsante sana. (Makofi)