Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Zainab Athuman Katimba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. ZAINAB A. KATIMBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na jitihada na mikakati mbalimbali ambayo Serikali imechukua kufufua viwanda na kujenga viwanda vipya nchini bado naona kuna changamoto ambazo ni vema Mheshimiwa Waziri akazifahamu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni vema kwanza kujifunza kwa nini viwanda vya zamani vilikufa?
Ni vema kujifunza wapi tulikosea kama Serikali na kama nchi mpaka viwanda vikafa
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni vema tukajifunza changamoto zinazokabili viwanda vilivyopo sasa na namna ya kuzitatua. Sambamba na kukaa vikao vya kimkakati na wamiliki wa viwanda waliopo saa hapa nchini na kupata mawazo na ushauri wa uhalisia wa hali ya uendeshaji wa viwanda hapa nchini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, je, viwanda vilivyopo vinakabiliwa na changamoto zipi?
Kimasoko ya bidhaa zizalishwapo nchini?
Upatikanaji wa nishati ya umeme ya kutosha na uhakika?
Gharama za umeme?
Sheria mbalimbali, rushwa na urasimu na kadhalika
Mheshimiwa Mwenyekiti, ushauri wangu ni lazima Wizara hii ishirikiane kwa karibu sana na sekta za kimkakati kama Wizara ya Nishati na Madini, Wizara ya Kilimo, Wizara ya Elimu na ofisi nyingine wezeshi ili kuweza kufanikisha dhamira hii ya Rais.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni vema kuwa na mpangokazi unaonesha ratiba ya utekelezaji wa kila hatua kuanzia sasa mpaka 2025. Pia ni vema Waziri atupe majibu ya changamoto zilizopo na namna atakavyozitatua na Wabunge tuko tayari kumpa ushirikiano kutafuta ufumbuzi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lazima tuongeze bidii ya kuvutia wawekezaji wa ndani na nje ya nchi na kupunguza urasimu na vikwazo visivyo vya lazima ili kuhakikisha maendeleo ya uchumi wa viwanda nchini, sekta binafsi kuwa nguzo muhimu katika kufikia lengo hili.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho ni lazima Serikali isimamie taasisi za kifedha nchini kwa kufunga sera wezeshi ili Watanzania waweze kushiriki kikamilifu kwenye uwekezaji ni lazima kuwe na upatikanaji wa mitaji yenye masharti nafuu toka kwenye benki zetu nchini ikilinganishwa na benki za nje yanayokopesha wawekezaji wa nje ambao wanashindana na wawekezaji wa ndani kwenye soko moja.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana na naunga mkono hoja kwa asilimia mia. Ahsante sana.