Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Esther Nicholus Matiko

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Naomba nami kuchangia Wizara hii muhimu katika uchumi wa Taifa letu. Kama nchi tumejiwekea malengo kwamba tufikie watalii milioni tano lakini ukiangalia trend kuanzia hata mwaka 2016 kwa takwimu za Wizara yenyewe walikuwa na watalii milioni 1.28; mwaka 2017 wakawa milioni 1.3; wakaja milioni 1.5; na sasa hivi 2020 waka-drop mpaka 620,000.

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba sisi ni wa pili kwa vivutio vingi duniani, lakini hatujaweza kuvitumia vizuri kuhakikisha kwamba utalii unatuingizia fedha nyingi za kigeni. Sasa nitakwenda kushauri machache tu kwa sababu ya uchache wa muda, kama Taifa na hili tumekuwa tukilisema, tuhakikishe katika balozi zetu tunaweka Maafisa Utalii ambao wanaujua utalii per se, ambao wanajua vivutio vyote tulivyonavyo Tanzania. Wakiwa kule kwenye zile nchi, watatumika kutangaza utalii wetu katika maeneo mbalimbali kwenye nchi husika. Hii itaenda kuongeza utalii na watu kutembelea nchi yetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, kingine utalii wa ndani kama sisi Watanzania tunakuwa mpaka unamaliza chuo, unaenda, wengine wanaenda mpaka nchi za nje, lakini hawajui hata vivutio tulivyonavyo Tanzania. Kwa hiyo tuki-promote utalii wa ndani kuhakikisha kwamba entry fee inakuwa ni ndogo, Mtanzania wa kawaida akiingia pale, basi hata yale mahoteli yawe accommodated kwa hawa Watanzania. Unakuta mahoteli ya mle ndani bei zao ni juu sana dola 200, 300 mpaka 1,000 huko, Mtanzania wa kawaida hawezi ku-afford kwenda pale.

Mheshimiwa Naibu Spika, inatakiwa hata wanafunzi wetu wa Shule za Msingi, Sekondari wanapata fursa ya kwenda kule, wanajifunza ili wanapokuwa wakubwa baadaye wakienda nchi za huko wanatangaza. Wakija watalii wa nchi zingine hapa kama ni watalii wa kibiashara wakikutana na mimi Esther Matiko nakuta nimeshajifunza, najua mbuga zetu, najua vivutio vyote, kwa hiyo nikiongea naye, akitoka akienda huko nje atatangaza na utalii utaongezeka.

Mheshimiwa Naibu Spika, kingine ni kuweza kuboresha miundombinu ya barabara hasa kwenye maeneo ambayo yako mipakani ili hata watalii ambapo wako nchi za jirani wanavyotaka kuja huku waweze kuwa vizuri, mathalani kule Tarime, tunapokea watalii ambao unakuta wameingia nchi ya Kenya, wanatoka Nairobi wanaingia Sirari, lakini wakishafika pale Tarime kwenda Serengeti, barabara ni mbovu na tumekuwa tukiongea kwa muda mrefu, irekebishwe ile barabara.

Mheshimiwa Naibu Spika, Marais wote wa Awamu ya Tatu, ya Nne na ya Tano waliahidi kutengeza barabara ile. Barabara tukitengeneza kwa kiwango cha lami watalii wakitoka kule ni wengi sana kuingia Serengeti tunaweza kukuza uchumi wetu. Serengeti imetajwa kuwa ni mbuga ya kwanza duniani na hata kwa Taifa letu ndio inaongoza kuleta mapato kwenye nchi yetu. Kwa hiyo ile barabara lazima iwekewe lami na maeneo mengine hata zile barabara za ndani ya mbunga.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sababu ya uchache wa muda, niendelee kuzungumzia mgogoro wa hifadhi na wananchi wetu. Tumekuwa tukizungumza hili Watanzania wetu wanauawa na hawa maaskari game mathalani kule Tarime, kuna Watanzania wameuawa Manga wa Kijiji cha Kenyamusabi; kuna ndugu John wa Kijiji cha Nyandage; kuna ndugu Mangenyi wa Kijiji cha Kegonga; hawa walikuwa ni wakulima tu wako mpakani. Ikasikika tu risasi wamepigwa wananchi wale hawajaonekana mpaka leo, lakini kuna wengine ni wafugaji zikasikika tena risasi ng’ombe hawajaonekana na hao wananachi hawajaonekana mpaka leo.

Mheshimiwa Naibu Spika, sio Tarime tu, Mbunge wa Mbarali alisimama juzi kati hapa akawa na statement na wananchi wengi hapa kama hatuwezi tukathamini wanyama huku tukawa tumewaua ndugu zetu, ichukuliwe hatua stahiki, kama askari game walinde hifadhi vizuri, wakiwakamata wawapeleke kwenye sheria, Mheshimiwa Waziri na Katibu Mkuu wake na Naibu Waziri najua haw ani watu ambao hawataki kuona haya mambo yanatokea, lakini watendaji kule chini wanafanya ndivyo sivyo. Hii haikubaliki kabisa.

Mheshimiwa Naibu Spika, la mwisho ni vile wanavyotaifisha ng’ombe. Hata wakienda mahakamani, mahakama ikaruhusu kwamba hawa watu warudishiwe ng’ombe wao, bado hawarudishiwi. Mathalani kuna Ndugu Hamisi wa Chato alinitafuta sana, ng’ombe wake walikamatwa kwenye Pori la Kigosi huko Kibondo mwaka 2018, walikuwa ng’ombe 420, lakini hawa askari wakasema walikuwa ng’ombe 216, wale wakawapekeleka mahakamani wakasema walipe tozo ya shilingi 500,000 wale ndugu wakalipa, lakini hawakurudishiwa ng’ombe wao.

Mheshimiwa Naibu Spika, wale watu wakaendelea kufuatilia.wakakata rufaa kwenda mkoa wakashindwa, kwenda Kanda ya Tabora wakashindwa, wakawa wanaamuriwa warudishiwe ng’ombe wao, wakashindwa kurudishiwa. Wakampigia aliyekuwa Waziri wa Maliasili na Utalii, Mheshimiwa Dkt. Kigwangala, walivyopiga simu kule wakaitwa wakapewa ng’ombe 73 tu. Hii ni dhuluma, kama wanaweza wakawakamata Watanzania wengine wakasema ni uhujumu uchumi, ina maana na wao wanafanya uhujumi uchumi dhidi ya Watanzania. Kama yule mtu tangu mwaka 2018 alikamatiwa ng’ombe wake 420, waka-declare wenyewe ni ng’ombe 216, yet wanaipa ngombe 73 wengine wanaenda wapi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, hii haikubaliki, mpaka hukumu tatu zote na wakiomba nitazi-table hapo, tunaomba hii ni just a single case study, wako wengi sana wamezungumza hapa. Kuna juzi kati nilimwona hata yule wa Longido kule alikuwa analia, yule baba na familia yake, ng’ombe wanataifishwa, tuna sheria tumejitungia ng’ombe wakiingia wapige faini inajulikana, kwa nini wanawataifisha, yet hawawarudishii ng’ombe wao. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, mwisho kabisa matumizi bora ya ardhi; kuweza kuondokana na hii sijui mara mara ng’ombe wametaifishwa, wananchi wanauawa, sijui tembo wanaingia kwa raia, sasa hivi hifadhi tulizokuwa nazo kama tunataka tuzichukue kwa matumizi bora ya ardhi tutenge, lijulikane kabisa hili eneo ni kwa ajili ya hifadhi, hili eneo halitakiwa kuwepo, ili hata vile vijiji ambavyo vipo kwenye hifadhi basi Wizara iweze ku-declare waondoe wale wananchi, kuliko hiki wanachowafanyia wanawaua.

Mheshimiwa Naibu Spika, ni bora ijulikane, kama wameamua kuondoa hivyo vijiji zibaki hifadhi waondolewe, wawape alternatives ardhi waende wakakae. Hatuwezi kuvumilia kama nchi kuona Watanzania wanauawa. Nina majina zaidi ya Watanzania 30 ndani ya Mkoa wa Mara ambao wameuawa kwenye ile Mbunga ya Serengeti, hatuwezi kukubali kitu kama hiki.

Mheshimiwa Naibu Spika, upande wa Bunda, Serengeti na Jimbo la Tarime Vijijini haikubaliki. Kwa hiyo tunaomba sana Waziri na watendaji wote hawa askari game ukinikamata kama nimeenda kinyume, nichukue nipeleke kwenye vyombo vya sheria, why are you killing our people? Ni Tanzania pekee ambapo mtu anaweza akauawa then inachukuliwa easy tu, yaani maisha ya Mtanzania hayana thamani dhidi ya tembo, fisi, simba na mambo mengine. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, hii is unbecoming kabisa, hatuwezi tukathamini wanyama dhidi ya Watanzania. Naomba sana naongea very bitterly, tunataka tujue hatma ya hawa Watanzania wa Tarime. Kama waliwauwa watupe maiti tuzike, tunasubiria kama wapo hai, wako wapi wapelekwe kwenye vyombo vya sheria ili ndugu wale waweze kujua, hawa walikuwa ni baba wa familia, walikuwa ni baba ambao wanatunza wazazi wao. Ahsante. (Makofi)