Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Yahaya Omary Massare

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Magharibi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. YAHAYA O. MASSARE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ili nichangie katika Wizara hii ya Maliasili na Utalii.

Mheshimiwa Naibu Spika, nichukue fursa hii kuishukuru Wizara hii kwa kuniteua kuwa Balozi wa Utalii wa Ndani, lakini pia nipongeze utendaji mzuri wa Waziri Mwalimu wangu Ndumbaro na Naibu wake kwa utendaji mzuri sana katika Wizara hii. Vile vile niwapongeze zaidi kwa hili ambalo wameliona juzi tarehe 2 kwa kuruhusu export ya mti wa mkurungu ambao ulikuwa barned pasipo sababu ya msingi.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imefanya maamuzi haya mazuri, lakini baada ya maamuzi haya kuna changamoto ambazo mimi naziona na naomba niishauri Serikali yangu ya Chama Cha Mapinduzi, lakini bahati nzuri zaidi kwa TFS ambao wapo hapa chini ya Wizara hii, kuna jambo ambalo sidhani kama wanaliona; tunapoamua sasa kufanya export ya mbao ngumu tunahitaji ma-saw doctors. Vyuo vyetu vya FITI bado havijatengeneza ma-saw doctors ambao wanafaa kufanya kazi maeneo yetu. Viwanda vilivyopo maeneo ya Mufindi na maeneo mengine ya mbao laini bado wanatumia ma-saw doctor ambao hawana elimu ya kutosha, ndio maana uchakataji wa magogo umekuwa na tatizo kubwa kwa maana mbao hazinyooki sababu ya kufanya hata export hizi zinakuwa na shida katika masoko ya dunia ni kwa sababu mbao zetu hazinyooki kwa sababu hatuna ma-saw doctors.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sababu Serikali ni moja, naomba Ofisi ya Waziri Mkuu ikubali wanapowadau wa misitu hasa wawekezaji wanapowekeza katika mazao ya misitu kwenye viwanda vya misitu, Serikali ikubali kuajiri ma-saw doctor wa kigeni ili kusaidia ku-train watu wetu baada ya muda nao wataweza kuchukua nafasi zile ambazo zinafaa.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuna jambo ambalo hapa limekuwa na changamoto kubwa sana, wananchi wengi hasa sisi wawakilishi wao wametutuma tuwazungumzie kuhusu sakata hili la mkaa. Gunia moja mtu anatakiwa kulipia sh.12,000, bado nchi hii hatujawa na mbadala wa nishati, sasa ni namna gani tunajipanga. Kwa kuwa Serikali ni moja labda ingefanya utaratibu basi gesi hii ambayo tunayo itapakae nchi nzima mabomba ya gesi yatoke kule Dar es Salaam yaje mpaka Mwanza, yaende mpaka Tanga na Mbeya kwako kule ili wananchi waweze kutumia hii gesi ya asili lakini matumizi mbadala leo ya mkaa hatuna.

Mheshimiwa Naibu Spika, niiombe sana Serikali iangalie namna bora hasa TFS watafute species za miti ambazo ni nyepesi kama alivyosema jana ndugu yangu hapa Mheshimiwa Profesa Kishimba, miti ambayo inaweza kupandwa kwa haraka na ikaota kwa ajili ya kupata mkaa kwa haraka.

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana, naunga mkono hoja hii ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa asilimia mia moja.