Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali katika Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Mwanne Ismail Mchemba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Tabora Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali katika Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. MWANNE I. MCHEMBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi na mimi nichangie machache kuhusu mapendekezo ya Mpango kwa kazi tuliyokuwa nayo mbele yetu ya Kitaifa ya maendeleo.
Awali ya yote nichukue nafasi hii kwanza kabisa kuwashukuru wapiga kura wangu walionichagua baada ya kunipa likizo kwa miaka mitano tena. Kwa hiyo, nawashukuru mama zangu wameweza kunipa nafasi mbili nikiwa kama Mwenyekiti wao wa Mkoa, lakini si hilo tu wakanipa na nafasi ya Ubunge, nawashukuru sana. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nachukua nafasi hii kumpongeza sana Mheshimiwa Waziri, kwa taarifa na Mapendekezo ya Mpango aliotuletea. Wakati nasoma nimeona amegusa sekta zote na hizi sekta kubwa ambalo tunamwombea ni utekelezaji, hilo ndilo kubwa, lakini Mpango, Maelekezo, itakavyokuwa, lakini kitabu hiki kinakidhi maeneo yote.
Mheshimiwa Mwenyekiti, niende moja kwa moja bila kupoteza muda kwenye upande wa viwanda. Viwanda hapa nchini amezungumzia kwenye ukurasa wa 24, viwanda twende kwa kufuata jiografia. Viwanda vingi vimefungwa, maeneo mengine hayana viwanda kabisa na sehemu nyingine viwanda vilikufa. Kwa mfano Mkoa wa Tabora, Mkoa wa Kigoma, Mkoa wa Katavi, tunalima tumbaku, lakini mpaka sasa kiwanda kiko Morogoro. Kwa hiyo, tunaiomba Serikali katika Mpango huu iangalie ni jinsi gani ya kuweka kiwanda cha uchakataji katika Mkoa wa Tabora ile ni center Mheshimiwa Mwenyekiti, si hilo tu kulikuwa na Kiwanda cha Nyuzi, kiwanda hiki kilikuwa kinachakata nyuzi kama nyuzi, nyuzi hizo ni za pamba. Wazalishaji wa pamba wakuu ilikuwa ni Tabora, Shinyanga, Mwanza na Kigoma, lakini pamba hizi zinasafirishwa badala ya kuzalisha kwenye Kiwanda cha Nyuzi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, niiombe Serikali katika Mpango unaoletwa iangalie ni jinsi gani ya kuweka kiwanda kizito kama kile katika eneo hilo, kwa sababu lazima tutafute center, jiografia yetu inasemaje. Si hilo tu, kuna viwanda ambavyo vimefungwa na vinatarajiwa kufungwa kutokana na mafuta yanayokuja, kwa mfano, kutoka nje au viwanda ambavyo vinazalisha nchini kukosa malighafi. Pia kuna viwanda ambavyo mpaka hivi sasa, kwa mfano, Viwanda vya Mafuta, vingi vinategemea kufungwa kwa sababu mafuta yanaletwa kutoka nchi za nje. Hawa wanalipa kodi kubwa, lakini viwanda vinapofungwa ni athari kubwa kwa nchi yetu kwa sababu ajira inakuwa haipo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo nimwombe Mheshimiwa Waziri wa Fedha na Serikali kwa ujumla, watusaidie kuhakikisha kwamba wanalinda viwanda vyetu vya nchini ili kuweza kupata ajira ya kutosha. Pia kutoa elimu kwa vijana wetu ili waingie katika soko la ushindani. Kwa hiyo, tunaomba wenye viwanda pia waweze kutoa mafunzo kwa wale wafanyakazi wao ili tuweze kwenda nao pamoja.
Mheshimiwa Mwenyekiti, miaka ya nyuma kulikuwa na viwanda vya SIDO. SIDO ni mkombozi mkubwa wa viwanda vidogo vidogo, hiyo nayo isisahaulike, SIDO ni mkombozi, akinamama wengi, vijana wengi wamejitokeza kupata mafunzo kwenye viwanda vidogo vidogo vya SIDO. Hata hivyo, si hilo tu, niombe Serikali yangu ni sikivu, haina wasiwasi, tena haya tunayoyazungumza asiwe na wasiwasi mtu yeyote kwamba hayatachukuliwa, yatachukuliwa na yatafanyiwa kazi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunapoathiri viwanda vya ndani na tusipoviwezesha viwanda vya ndani nchi yetu tunaikosesha mapato, kwa sababu asilimia kubwa ya mapato inategemea sana viwanda. Kwa hiyo, kubwa ambalo ningeishauri Serikali, walinganishe, waoanishe, sera ya viwanda na sera ya biashara. Hivi vitu viwili vinakinzana na kama vinakinzana vinatuathiri sana. Nimwombe Waziri wa Viwanda aliangalie hilo, ashirikiane pia na Baraza la Mawaziri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, niende tena kwenye suala la reli, limezungumziwa kwenye ukurasa wa 53, lakini halikukaziwa, limewekwa juu, juu. Niombe kwa niaba ya wenzangu na wenyewe watachangia, tusilete mzaha kwenye suala la reli ya kati. Reli ya kati itatutenga sana. Hatuwezi tukaidharau kwanza kwa mambo mawili, wapiga kura wetu na wananchi wetu wa Tanzania wanategemea sana reli ya kati, wanategemea sana TAZARA, lakini si hilo, ubebaji wa mizigo barabara zote zinaharibika kwa sababu ya magari mazito.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tutakapoweza kuimarisha reli, ingawa wamesema latiri 80 kwa kipande, kwa mfano, wamesema kati ya Igalula, Tabora, Lolangulu, jamani tuizungumzie yote ili ifike Kigoma, ifike Mpanda, ifike Mwanza ili wabebe mizigo yote, hata hao nchi za nje wanategemea reli hii iwaunganishe kutoka Dar es Salaam kwenda huko. Unaposema kwamba nyingine ianzie huku kwa kweli niombeā€¦
(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)
MHE. MWANNE I. MCHEMBA: Bado dakika zangu.
MWENYEKITI: Kengele hiyo.
MHE. MWANNE I. MCHEMBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ukarabatiā€¦ Bado ni ya kwanza.
MWENYEKITI: Ya pili.
MHE. MWANNE I. MCHEMBA: Ya pili? Hapana Mwenyekiti ni ya kwanza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nisibishane na wewe naunga mkono hoja, lakini ni ya kwanza, ahsante sana. (Makofi)