Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Edward Olelekaita Kisau

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kiteto

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. EDWARD O. KISAU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana. Kwasababu ya muda nitatoa tu hongera ya jumla hivi, mnielewe. Nitawapongeza baadaye. (Kicheko/ Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Ilani ya Chama cha Mapinduzi, ukurasa wa 113 unasema hivi, naomba sana wataalam wetu waisome sana: “Kuimarisha mahusiano kati ya maeneo ya hifadhi na wananchi.” Mahusiano ya wananchi na hifadhi ni mabovu sana. Hilo moja. Ilani inaendelea kusema hivi, ili Sekta hii iwe endelevu, lazima mjali haki na maslahi ya wananchi. Hamwangalii sana maslahi ya wananchi wakati mwingine.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nilikuwa nasoma vitu vingi tu hapa, nilichogundua ni kwamba, kama walivyosema wasemaji wengine, utalii tangu tumepata uhuru mambo yote bado yapo kikoloni zaidi; ni boots and guns, fences, fines, mnaanza kuua watu, mnachukua ng’ombe wa watu; hiyo siyo sustainable. Mwache! Uhifadhi ili uwe endelevu, ni lazima ushirikishe wananchi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumeambia kwenye data hapa kwamba sasa tunaongelea asilimia 32 mpaka 40 ya nchi hii, iko kwenye hifadhi, it may not be enough, lakini lazima mfahamu tumeongezeka. Ni dhana ya kikoloni ambayo ni exclusion, expansion, removable, nature, then people later, haiwezi kuwa sustainable. Nchi nyingine zimeshabadilika, wameanzisha model ambazo zina-accommodate watu na uhifadhi. WMA ni classic example, inawezekana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, haya mambo ya kukaa na kuanza ku-characterize ardhi za watu, eti corridor, eti buffer zone, eti wildlife or pastoral area, I mean! Mheshimiwa Waziri, kuna tangazo laki hapa nililisoma asubuhi hapa. Umewaelekeza watu wako wachaji ng’ombe 100,000 kwa kichwa cha ng’ombe. Miaka miwili iliyopita ilikuja sheria hapa ya kutaka kulishawishi Bunge lilete faini ya shilingi 100,000 kwa kichwa na Bunge lilikataa, hongereni sana. Sasa limeanza kurudi kwa mlango wa nyuma.

Mheshimiwa Waziri, this is illegal, haiendani na sheria zetu, nawe ni Mwanasheria, Wakili tena Dokta kabisa. Nakushauri sana, please rethink kuhusu hili, it is illegal, it is unlawful. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, ndiyo maana kuna wengine walikuwa wanasema hapa hatufuati sheria. Sheria haijasema hai-punish ng’ombe, inam-punish mwenye ng’ombe, ndiyo logic ya sheria. Sasa ninyi mkianza kuleta; na sheria iko hapa, haisemi hivyo. Fine kwa group minimum imetolewa na sheria na maximum. Kwa hiyo, mna-range pale. Hii idea ya kuleta sheria ya kichwa cha ng’ombe it is illegal, haipo! Kesho nataka nisikie hii inakuwa supported na sheria gani? Kama hamtasema, nitashika shilingi kwa mara ya kwanza. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tuache. Nchi hii sasa tusipofikiria kuleta model zinazotuchanganya Pamoja, huu uhifadhi utafeli. Suala la mifugo, mimi nina mwananchi wangu Kijiji cha Warkyushi kuna pori linaitwa na Mkungunero. Pori la Mkungunero by GN liko Kondoa, Dodoma; lakini wanatuambia eti beacon ziko Kiteto, how? Kwanza kisheria ukishakuwa na GN ambayo ina-conflict na GPS points maana yake kisheria ni kwamba you can’t enforce, lakini wewe unakamata ng’ombe kila wakati. Mheshimiwa Hayati Rais Magufuli…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MWENYEKITI: Ahsante.

MHE. EDWARD K. OLELEKAITA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. (Makofi)