Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Nishati

Hon. Cosato David Chumi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Nishati

MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Spika, nawapongeza kwa kazi nzuri mnayofanya, lakini zaidi usikivu wenu. Binafsi kila nilipoomba kuonana na Mawaziri au Watendaji kuanzia Katibu Mkuu, DG wa REA na TANESCO kwa kweli nimepata nafasi na nimesikilizwa na shida za wananchi wa Mafinga zimepata walau suluhisho,

Mheshimiwa Spika, hata hivyo nina ushauri na mambo kadhaa kwa Wizara. Hoja yangu ya siku zote ni kuhusu kuona uwezekano wa kuwa na Wilaya mbili za Kitanesco katika Wilaya ya Mufindi kutokana na umuhimu wake, hasa katika dhana nzima ya uchumi wa viwanda.

Ushauri wangu ni kwamba tuwe na ofisi kwa ajili ya Mafinga ambako kuna viwanda vingi vya mazao ya misitu na tuwe na Ofisi Mufindi ambako kuna viwanda vingi vya chai pamoja na Kiwanda cha Karatasi Mgololo. Ninaamini hata mapato, Mufindi inazidi baadhi ya mikoa. Hivyo kusogeza huduma hii haitakuwa mara ya kwanza. Kwa mfano, Ilala ina zaidi ya Wilaya moja ya Kitanesco.

Mheshimiwa Spika, transfoma zinazofungwa Mafinga za KV 50 ni ndogo ukilinganisha na uhitaji hasa wa viwanda vya mazao ya misitu. Maombi yangu; umeme ni huduma na ni biashara/mapato, ni kwa ajili ya uzalishaji, hivyo kuwekeza nguvu kwenye maeneo kama Mafinga itasaidia kuongeza mapato ambayo yatatumika kusambaza umeme maeneo ambayo umeme ni kwa ajili ya huduma zaidi. Kwa hiyo, iwe ni ujazilizi au REA III awamu ya pili, ipo kila sababu maeneo kama Mafinga kuyaangalia kwa macho mawili na kwa jicho la uchumi wa viwanda.

Mheshimiwa Spika, lingine ni kuhusu taa za barabarani. Tayari Halmashauri ya Mafinga Mji, imeshawasilisha andiko kadri ambavyo DG wa REA alituelekeza. Hivyo kwa umuhimu ule ule ambao Serikali ilikubali mazao ya biashara ikiwa ni pamoja na nguzo za umeme kusafirishwa masaa 24, tunaomba taa za barabarani katika maeneo ambayo ni junction za kibiashara.

Mheshimiwa Spika, lingine ni Luku. Sina utaalam wa masuala ya IT, lakini nashauri kwamba kama teknolojia inaruhusu, basi mtu anaponunua umeme asilazimike tena kwenda kwenye mita kuingiza token. Iwe kama ving’amuzi ambapo ukinunua tu inaji-update. Naomba kuwasilisha.