Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Nishati

Hon. Bernadeta Kasabago Mushashu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Nishati

MHE. BERNADETHA K. MUSHASHU: Mheshimiwa Spika, nampongeza Mheshimiwa Waziri, Naibu Waziri na Katibu Mkuu kwa hotuba nzuri na kazi nzuri wanayoifanywa Wizarani.

Mheshimiwa Spika, Mkoa wa Kagera bado una vijiji vingi ambavyo havina umeme. Je, ni lini Miradi ya REA III, Mradi wa ujazilizi na wa Peri-urban itakamilishwa au kuanzwa lini Mkoani Kagera?

Mheshimiwa Spika, Wilaya nyingi hazikuunganishwa kwenye grid ya Taifa. Tunatumia umeme wa Uganda. Umeme huu umekuwa kero kwa wananchi kwani unakatika katika kila mara. Je, ni lini Serikali itarekebisha hayo matatizo ili wana Kagera wapate umeme wa uhakika?

Mheshimiwa Spika, Rais wa Serikali ya Awamu ya Tano, akiwa kwenye mkutano wa hadhara pale Bukoba Manispaa, alisema anampatia jukumu Naibu Waziri wa Nishati ahahakikishe matatizo ya umeme yanaisha kabisa Mkoani Kagera. Je, ni lini ahadi hii itatekelezwa?

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja.