Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Nishati

Hon. Zuberi Mohamedi Kuchauka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Liwale

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Nishati

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Spika, naomba pia kuchangia kuhusiana na gesi ya Mtwara, Baada kuanza kwa mradi wa kuchimba gesi Mkoani Mtwara ni matumaini ya watu wa mikoa ya Mtwara na Lindi wawe wa kwanza kunufaika na mradi huu, lakini sasa ni kinyume chake. Mfano, mradi wa gesi majumbani unaanza kutekelezwa Mkoani Dar es Salaam na Pwani na kuiacha mikoa ya kusini Lindi na Mtwara inakotoka gesi. Jambo hili siyo jema hata kidogo.

Mheshimiwa Spika, Kata ambazo hazina umeme kabisa katika Wilaya ya Liwale ni pamoja na Kata za Mpigamiti, Mlembwe, Lilombe, Ngongowele, Mkutano, Kimambi, Mbaya, Barikiwa, Miriwi na Nahoro. Ningetamani kwa awamu hii Kata ya Mpigamiti ingekuwa ya kwanza, Kata anakotoka Mbunge kuko kiza, ni aibu isiyovumilika.

Mheshimiwa Spika, naanza mchango kwa kuwapongeza Mheshimiwa Waziri pamoja na Naibu Waziri kwa kazi kubwa ya kusimamia majukumu ya Wizara hii hasa kwenye Mradi wa REA. Hata hivyo, hakuna mafanikio pasipo na changamoto. Ziko changamo kadhaa katika utekelezaji wa mradi huu wa REA.

Mheshimiwa Spika, mfano katika Jimbo langu la Liwale bado umeme huo haujafika katika vijiji vingi. Wilaya ya Liwale yenye Kata 20 na Vijiji 76 kuna Vijiji 34 tu vilivyofikiwa. Tatizo kubwa ni Wakandarasi, wamekuwa wakitoa visingizio vya kushindwa kufikisha vifaa kutokana na ubovu wa barabara. Jambo ambalo halina ukweli, kwani ziko taasisi nyingi zinafanya kila siku na kupeleka bidhaa mbalimbali. Hapa naomba Mheshimiwa Waziri atembelee Liwale kuona uhalisia wa miradi ya REA katika Jimbo langu, bado mahitaji ni makubwa sana.

Mheshimiwa Spika, umbali wa kutoka Nachingwea hadi Liwale ni zaidi ya kilometa 230. Hivyo basi, line ya umeme imekuwa na changamoto nyingi sana kama vile nguzo kuanguka na kuungua moto. Pia kutokana na umbali uliopo, unahitaji pia substation kwa ajili ya kuongeza nguvu ya umeme. Kwani umeme unaofika Liwale tayari unaonekana kuwa na nguvu ndogo.