Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Nishati

Hon. Amb. Dr. Pindi Hazara Chana

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Nishati

MHE. DKT. PINDI H. CHANA: Mheshimiwa Spika, awali ya yote, naunga mkono hoja.

Mheshimiwa Spika, naomba kukumbushia baadhi ya Kata katika Wilaya ya Ludewa ambazo hazina umeme, kama Kata ya Ibumi, vijiji 28 Wilaya ya Ludewa havina umeme. Kata ya Milo, Ibumi, kilondo, Ludende, Lumbila, Mkongobaki na Munford Wilaya ya Ludewa hakuna umeme. Tarafa ya Mangali Ludewa kwa baadhi ya maeneo hakuna umeme.

Mheshimiwa Spika, tunaomba Serikali ilione hili, ituletee umeme Ludewa maeneo yote. Wilaya ya Ludewa Kata ya Lugarawa vijiji 20 havina umeme; na Kata ya Mawengi vijiji vinane havina umeme. Tunaomba umeme.

Mheshimiwa Spika, ahsante, naomba kuwasilisha.