Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Nishati

Hon. Deodatus Philip Mwanyika

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Njombe Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

3

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Nishati

MHE. DEODATUS P. MWANYIKA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa nafasi. Nianze kwa kumpongeza Mheshimiwa Waziri kwa kazi nzuri ambayo amekuwa akifanya.

Mheshimiwa Spika, katika bajeti ya Mheshimiwa Waziri tunaambiwa sasa ni vijiji karibu 1,952 ndiyo bado havijapata umeme na katika REA III round II ndiyo vitapata umeme. Kwa Jimbo letu la Njombe tuna tatizo na nilishaonana na Mheshimiwa Waziri kumueleza matatizo ambayo tunayo. Njombe ni vijiji vinne tu ndiyo ambavyo vimeingia katika mradi wa REA III round II. Mheshimiwa Waziri alinihakikishia kwamba kulikuwa na makosa na kwamba vitajumuishwa.

Mheshimiwa Spika, Waziri ametushauri hapa kwamba tuwasiliane na wakandarasi ili tuweze kujua scope ya kazi yao na wanafanya nini. Nimewasiliana na wakandarasi kama Waziri alivyosema lakini cha kusikitisha ni kwamba wakandarasi mpaka sasa scope yao ya kazi inafahamu hivyo vijiji vinne tu.

Mheshimiwa Spika, naelewa pengine kuna mchakato wa kubadilisha hiyo scope lakini nimuombe Waziri kwa niaba ya wananchi wa Njombe awahakikishie kwamba vijiji vile 20 vyote vitaingizwa katika mpango huu.

Tunaomba sana asitupeleke kwenye Peri-Urban Project maana vijiji hivi ni vijijini kabisa siyo maeneo ya mjini kwa vile Jimbo la Njombe linaitwa Njombe Mjini. Vijiji hivyo ni kama vifuatavyo; Makoo, Ngelamo, Mamongolo, Lugenge, Kisilo, Kiyaula, Idihani, Utengule, Ngalanga, Uliwa, Igoma na kijiji ninachokaa mimi vilevile kina matatizo cha Makanjaula nacho hakina umeme. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nimuombe sana Waziri atuangalie kwa jicho la huruma. Njombe program nzima ya REA I, II, III zote hizi kwa kiasi kikubwa sana zimekuwa propelled na Mkoa wa Njombe kwa sababu sisi ndiyo supplier wakubwa wa nguzo karibu zote ambazo zinakwenda katika project hizi zote. Kwa hiyo, tuna kila sababu ya kuona Mheshimiwa Waziri na sisi anatuangalia.

Mheshimiwa Spika, lakini kwa namna ya pekee nimuombe Waziri, tuna Shule ya Sekondari Yakobi, REA III round I uli-target taasisi mbalimbali za afya na za elimu lakini kwa bahati mbaya sana shule hii ambayo ina watoto karibu 600 mpaka leo wako gizani. Tunamuomba sana Mheshimiwa Waziri ajaribu kuiingiza shule hii nayo ili iweze kupata umeme katika kipindi hiki.

Mheshimiwa Spika, naomba niongelee suala la nishati jadidifu. Sekta madhubuti ya nishati ni ile ambayo ina mchanganyiko wa vyanzo mbalimbali vya umeme. Kwetu hapa tunaona kabisa kwamba kwa kiasi kikubwa umeme wa maji na umeme wa gesi ndiyo unachukua sehemu kubwa lakini tuna potential kubwa ya kuwa na umeme tofauti na huo au wa kuongezea kama umeme wa upepo au solar. Wawekezaji siyo kama hawapo lakini majadiliano na wawekezaji hawa yanachukua muda mrefu sana. Njombe tuna potential ya kuzalisha mpaka megawatt 150 kwa umeme wa upepo kama vile wenzetu wa Singida. Mheshimiwa Waziri ametuambia wanakwenda kufanya majadiliano na ni kweli wawekezaji tunajua wameshaitwa kwa majadiliano lakini majadiliano haya yafike mwisho basi ili na umeme wa upepo nao uingie katika mpango wetu wa umeme. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kama muda utaniruhusu niongelee kidogo kuhusu mradi wa kusindika umeme wa gesi. Kwenye vitalu Na.1, 2 na 4 ndipo ambapo tunategemea kwamba mradi huu mkubwa wa LNG utajengwa au utapata resource yake ya umeme. Tuseme wazi Tanzania ina bahati kuwa na endowment kubwa sana ya gesi 57 tcf ni umeme mkubwa, ukiu-put kwenye context ni umeme ambao unaweza uka-power nchi ya UK kwa miaka 20 bila wasiwasi, kwa hiyo, ni umeme mwingi mno. Hata hivyo, suala siyo kuwa na resource ni namna gani resource hii sasa tunakwenda kuifanya ifanye kazi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini niseme kimoja katika global scale bado Tanzania hatupo hata katika top twenty wenye resource kubwa ya gesi. Kwa hiyo, wawekezaji ambao tunao kwenye sekta hii ni vizuri tukakamilisha mazungumzo hayo. Tunafahamu siyo kitu cha kukimbilia au cha kufanya haraka lakini tuseme kama alivyosema Mbunge mmoja hapa kwamba kwa kweli hatuna muda mwingi wa kupoteza.

Mheshimiwa Spika, naomba niunge mkono hoja, ahsante sana. (Makofi)