Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Zaynab Matitu Vulu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. ZAYNABU M. VULU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze kwa kumpongeza Mheshimiwa Waziri kwa uwasilishaji wake wa hotuba ya bajeti. Viwanda vidogovidogo vilivyokuwepo kwa tathmini ya mwaka 2012 imeonesha kulitolewa ajira milioni 5.2 na kuchangia Pato la Taifa (GDP) ambapo ajira hizo zilisaidia kuwezesha familia kujiendesha na kupunguza uzururaji.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimalizie kwa kusema kwamba, kiasi cha shilingi bilioni 81, kilichoombwa kwa mwaka 2016/2017 kinashabihiana na kasi ya Mheshimiwa Rais John Pombe Joseph Magufuli cha kutaka kujenga Tanzania ya viwanda kwa sababu asilimia 49.3 ya pesa zote zinaenda kwenye shughuli za maendeleo na asilimia 50.7 iende kwenye matumizi ya kawaida. Ili tuwe na viwanda ambavyo vitazalisha kwa uhakika, suala la miundombinu ya umeme, barabara na reli iwe imeimarika zaidi tuweze kusonga mbele.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.