Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Pascal Yohana Haonga

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Mbozi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. PASCAL Y. HAONGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa, nchi hii ina matunda mengi kama vile maembe, mananasi, machungwa, zabibu na mengineyo, Serikali haina sababu ya kuagiza juice na wine nje ya nchi kwa kuwa uwezekano wa kuanzisha viwanda vya juice na wine hapa nchini ni mkubwa, kuagiza juice nje ya nchi ni upotevu wa fedha.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia mafuta ya kupikia ambayo ni ya pili kuingizwa nchini yakitangulia mafuta ya magari, Serikali ipige marufuku uingizaji wa mafuta ya kupikia kwa kuwa mazao ya kutengenezea mafuta kama vile karanga, alizeti na mawese vinapatikana hapa nchini. Alizeti inalimwa katika Mikoa ya Singida, Iringa, Mbeya, Rukwa, pamoja na Mikoa mingine.
Mheshimiwa Mwenyekiti, vivyo hivyo, uagizaji wa toothpick ungepigwa marufuku kwa kuwa tuna miti mingi inayoweza kutengenezea toothpick. Serikali ikizingatia haya yote tutaokoa fedha nyingi sana, lakini pia tutatengeneza ajira kwa wananchi wetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha.