Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Nishati

Hon. Selemani Jumanne Zedi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukene

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Nishati

MHE. SELEMANI J. ZEDI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi hii ili niweze kuchangia kwenye hotuba hii muhimu sana ya wizara muhimu sana ya Nishati. Awali ya yote nianze kwa kumpongeza Mheshimiwa Waziri na Naibu Waziri kwa kuiongoza Wizara ya Nishati na mwezi wa tatu uliopita, Mheshimiwa Waziri alikuja jimboni kwangu kuzindua mpango wa REA Awamu ya tatu na alifanya kazi kubwa sana hongera sana Mheshimiwa Waziri. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, na niseme tu kwa kipindi ambacho nimekaa Bungeni, Mheshimiwa Waziri wa Nishati ndugu yangu Kalemani ni Waziri ambaye ni msikivu na niwaziri ambaye anafikika ni approachable ni waziri ambaye unamfikia kirahisi na anasikiliza Wabunge kwa kina, hongera sana Mheshimiwa Kalemani. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nianze kwa kuzungumzia bomba la mafuta na nina interest la bomba la mafuta kwa sababu pale kwenye jimbo langu, Jimbo la Bukene, Kijiji cha Sojo ndipo ambapo itajengwa karakana kubwa ambayo mabomba yote ya kilometa 1,400, kutoka Hoima mpaka Tanga yote kabla ya kufukiwa chini pale ndipo yataandaliwa kwa hiyo, karakana ambayo Mheshimiwa Eng. Ezra itajengwa kwenye Kijiji cha Sojo ambacho kipo ndani ya jimbo la Bukene.(Makofi)

Mheshimiwa Spika, Serikali pale imechukuwa hekta 400 na sasa hivi wananchi wanasubiri tu fidia ili kazi ya ujenzi wa hiyo inaitwa courtyard ianze pale. Sasa angle yangu itakuwa ni namna gani Watanzania watanufaika na huu mradi wa bomba la mafuta. Pamoja na faida nyingine ambazo tunazijua za bomba la mafuta ambazo sina haya ya kuzungumzia, lakini kuna faida kubwa sana ambayo Watanzania wanaweza kuipata kama wizara itajipanga vizuri na kuweza kuainisha shughuli zote zitakazofanyika kwenye ujenzi wa bomba la mafuta na kuwaandaa watanzani ili Watanzania washiriki kikamilifu kwenye hizo shughuli na kuweza kupata manufaa yatakayo patikana. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, mradi huu unakuja na fedha nyingi sana pale tu kwenye Jimbo la Bukene kwenye courtyard, bajeti yake Serikali iko kampuni inayojenga pale itaingiza bilioni 600 ambazo zitakuja kwa ajili ya mfumo wa activities mbalimbali. Sasa as we speak now sasa hivi Serikali haijaweka wazi ni kazi gani zitakazofanyika pale kwenye bomba hilo la mafuta na kazi hizo zinahitaji ujuzi gani? Zinahitaji technical capacity ipi? Kwa sababu, Watanzania hatuwezi kunufaika kama hatujajiandaa mapema kwa sababu hatuwezi kusubiri wakati wa implementation ukifika tu alafu na sisi ndiyo tujitokeze obvious tutashindwa ku- compete na makampuni mengine. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, ushauri wangu kwenye hilo ni kwamba wizara iandae desk maalum ambalo litaainisha activities zote zitakazofanyika zinahitaji technical capacity gani? Zinahitaji administration capacity gani? Ili kampuni za kitanzania zianze kujipanga, yanahitajika maandalizi Watanzania wanahitajika kuunda hizi kampuni nyingine inabidi ziundwe ziajiri technical fulani, ziwe na uwezo fulani ili kuweza ku-compete kupata hizo kazi, haya mabilioni ya shilingi yatakayoletwa na maradi huo kama hatujajipanga tutayaangalia tu na yatachukuliwa na makampuni nyingine za nje. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nikiendelea pale pale kwenye bomba la mafuta ni kwamba kama tulivyokubaliana mwanzoni mwaka jana Mheshimiwa Kalemani na Waziri wa Ardhi walikuja pale kwenye Kijiji cha Sodo kukagua eneo lile ambalo courtyard itajengwa ninaomba hapa msisitizo kabla, shughuli hazijaanza basi wananchi wale wote walipwe fidia, zile heka 400 ambazo Serikali imechukua zimeshafanywa uthamini kamishna wa ardhi ameshaizinisha, wananchi wanasubiri fidia na kabla shughuli yoyote haijaanza, ushauri wangu ni kwamba wananchi wale walipwe fidia ili kuondoa migongano inayoweza kuwepo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini pale ambako courtyard inajengwa as we speak now hakuna umeme, hakuna maji, lakini tulifanya mazungumzo ya mwanzoni mwaka jana, kwamba kampuni ya EACOP ndiyo italeta umeme pale na ndiyo itale maji pale, kwa hiyo it right time now kwa wizara kuisimamia na kuifuatilia kampuni ya EACOP ili umeme ulietwe pale na maji yaletwe pale. Na angalizi hapa ni kwamba umeme utakapoletwa siyo uletwe kwenye point two ambako coating yard itajengwa, lakini vijiji vyote ambavyo vinazunguka pale kwenye Kambi ya Sojo viweze kunifaika na umeme huu na maji ambayo yatafika pale. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ninzungumzie kidogo mradi wa REA awamu ya tatu, mimi tatizo ninaliona kwa mradi wa REA scope hiyo inayoitwa wigo. Sasa hivi kwenye vijiji vyetu utakuta kijiji fulani kinatajwa kwamba kimepata umeme, lakini ukienda kiundani kuangalia unakuta kijiji kinavitongoji sita, kitongoji kilichopata umeme ni kimoja vitano havina umeme, lakini kijiji chote kinatajwa kwamba kimepata umeme. Kwa hiyo, Mheshimiwa Waziri kuna haya ya kuangalia scope ule wigo wa umeme kufika kijijini la sivyo tutakuwa tunahesabu vijiji lakini kumbe ni kakitongoji kamoja tu kwenye kijiji ndiko kana umeme. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, wilaya yetu imepata mkandarasi ambaye ni Sillo Power ni matumaini yangu kwamba yale makosa yaliyokuwa yamefanywa na mkandarasi wa mwanzo hayatarudiwa tena, kuna vijiji vilikuwa vimerukwa lakini kulikuwa na ucheleweshaji mkubwa na ninaimani kwamba Mheshimiwa Kalemani anauwezo mkubwa wa kusimamia eneo hilo na ataweza kusukuma. (Makofi)

SPIKA: Ahsante sana.

MHE. SELEMANI J. ZEDI: Mheshimiwa Spika, baada ya kusema hayo naunga mkono hoja. (Makofi)