Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Nishati

Hon. Boniphace Mwita Getere

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bunda

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Nishati

MHE. BONIPHACE M. GETERE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi nichangie hoja hii ya Wizara ya Nishati, binafsi nimefurahi kumuona Senator wetu Mheshimiwa George Mkuchika kwa kweli tuwe wakweli mwanadamu ni roho tu kama roho zetu zipo salama tunatakiana mema humu ndani, tunatakiana mema kwenye roho, roho tu ndio Mungu anaitaka iendelee kuwepo hiki kiwiliwili ni cha hapa hapa duniani lakini roho ni ya Mungu ikiendelea kuwepo tunashukuru. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naomba niipongeze Wizara ya Nishati wanafanya kazi nzuri sana sana. Wizara hii sisi ambao tulikuwa wabunge wa CCM tulikuwa tunatekeleza ilani ya Chama Cha Mapinduzi kusema kweli sehemu kubwa ya vijijini ya utekelezaji wa Ilani hii Wizara ndio imetekeleza, kura nyingi tulizozipata katika CCM kwa utekelezaji wa Ilani ni pamoja na hii Wizara ya Nishati, na hasa mradi wa REA vijijini kwa hiyo mradi wa REA vijijini ni muhimu sana Wizara imefanya kazi lakini Waziri wake na watumishi wengine wote na Naibu, ila tunamfahamu Waziri zaidi kwa sababu tumekaa naye muda mrefu kidogo nidhamu yake haina mfano. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, haina kabisa katika watu wanaotaka kupewa nidhamu baadhi ya Mawaziri wanaotaka kupewa nidhamu kwa utendaji na kwa kumpigia simu na kupokea na kunyenyekea na kufanya kazi huyu bwana anafanya kazi kweli sio utani. Anafanya kazi nzuri sana. Sasa niombe, kwamba huko tunakokwenda huko mbele mimi naona kama Wizara imekuwa na shughuli nyingi mno na hili unaweza kulisimamia hii Wizara inapokwenda nimesikia juzi tunatafuta mafuta, kutafuta mafuta ya kuchimba baharini ashughulike Mheshimiwa Dkt. Kalemani Bomba la kutoka Uganda lije Tanzania Mafuta ashughuliye huyo huyo, gesi inayotoka NLG aende yeye sun NLG wanaiita aende yeye wewe msukuma acha, bwawa la Mwalimu Nyerere aende yeye ashughulike sijui na vinasaba na mafuta kutoka Bandarini yeye. (Makofi/Kicheko)

Mheshimiwa Spika, naona tufanye kama wenzetu tuwe na Wizara mbili Wizara ya maendeleo ya Nishati na Wizara ya Maendeleo ya Petrol kwani kuna shida gani kama hizi Wizara zina fedha za kutosha mambo ya mafuta ni mabilioni ya fedha, mambo ya umeme yajitegemee hivi leo umeme unakatika kila mahali, umeme wa REA hauendi Kalemani ataendaje Bunda, ataendaje Kongwa ataendaje huko wakati wamembana kwenye mikataba ya kwenda Uganda, kusaini Mikataba, tukubaliane Mheshimiwa Rais alione hili tutenganishe hii miradi ya kimkakati iwe na mtu mwingine na hii mradi ya umeme ibaki na watu ambao tunashughulika nao kila siku.

Mheshimiwa Spika, wananchi wanataka kuona umeme habari ya kuchimba mafuta, habari sijui ya gesi inatoka kwenye mabomba ipewe mtu mwingine kuna shida gani, tuliangalie hilo naona sasa tukiliona hilo vizuri nchi yetu itaenda kwenye jambo la namna hiyo. Nimshukuru Mheshimiwa Rais, Mheshimiwa Rais anafanya kazi nzuri jana nimemuona kule Sokoni anahangaika na matatizo ya wananchi, amesimamia vizuri bomba la mafuta la kutoka Uganda ule ni mradi wa kimkakati wa muda mrefu lakini wenye faida. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, wamezungumza Wabunge wengi hapa ushauri wangu kwenye huu mradi Wabunge tuelimishe kuhusu huu mradi, huu mradi una mikataba mitatu mimi leo nikiambiwa mradi ule unafanyaje nitasema utapata ajira nyingi, utafanya nini lakini sijaelewa mikataba ya miradi hiyo ikoje. Kwa hiyo, Wabunge tuelimishe juu ya mikataba mitatu ya huu mradi ukoje, unafanyaje tupate Semina ya kutosha ili na sisi tueleze faida ya mradi huu itaendaje kwenye shughuli za kila siku huko mbele tunapokwenda.

Mheshimiwa Spika, kuna suala la vinasaba sasa ninashindwa kuelewa wakati fulani ukisoma hadithi au ile tips za wakubwa wale watu waliokuwa wanatafuta uhuru akina Stephen Biko, anakwambia akili ya mwanadamu, akili ya mtu anayedhulumiwa yaani mtu anayedhulumiwa ili ajielewe anafanya kazi gani ya kudhulumiwa umpe akili wala usimpe silaha. Sasa ninashindwa kuelewa vinasaba ni nini, vinasaba ni vitu ambavyo mtu ameleta ili kutibu tatizo na nchi hii inaweza kuendeshwa bila vinasaba lakini leo kuna watu wamejipanga vinasaba vinasaba vinasaba.

Mheshimiwa Spika, nataka kusema jambo moja vile vinasaba sasa hivi vinatozwa shilingi 14,000 mafuta yanayoingia nchini, mafuta tunayotumia sisi ni mafuta yanayotumika hapa nchini ni bilioni 14 ukizidisha na 14 ni bilioni 56 matumizi yake yakitoka super profit ni bilioni 40.

Mheshimiwa Spika, kwanini watu wasiseme kwanini wati doubt bilioni 40 unaipeleka wapi? Kwa hiyo niseme kwamba TBS inauwezo wa kupima ubora wa mafuta lakini haina uwezo wa kuweka vinasaba mambo ya ajabu duniani hapa ubora wa mafuta TBS inauwezo wa kupima lakini kupima kuweka vinasaba haiwezekani vitu vya ajabu sana hapa duniani. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ninajiuliza madawa yanayotumika hapa nchini, madawa ya wanadamu sisi tunatengeneza hapa si tunaagiza yaani kuagiza madawa ya kutibu wanadamu hapa nchini ni jambo dogo kuliko kuagiza vinasaba, mambo ya ajabu hapa duniani hapa, mambo ya ajabu sana hapa tunaagiza mbolea tunaagiza madawa tunaagiza kila kitu tunafanya operation za binadamu vinasaba ni kitu gani. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo niombe nishauri niombe vinasaba visimamiwe na TBS na TBS wachukue shilingi saba kwa sababu vile vinasaba ni shilingi nne unaweza ku-handle, shilingi saba nyingine ije TARURA tunahangaika hapa na mambo ya TARURA mambo ya Barabara na mambo ya nini tuna hela zipo hapa…

SPIKA: Mheshimiwa Getere nilichokielewa so far kwa sababu niko nawasikiliza wote wanasema hawa waliochangia kuhusu kinasaba mpaka sasa wanasema kuipa TBS sio tatizo ila tunajukumu sisi Wabunge wa kuirekebisha sheria ya TBS kwa kuwaongezea hilo jukumu ndani ya sheria, ili wafanye kisheria jambo ambalo nafikiri tumuhimize Waziri endapo linakubalika ili sasa lifanyike hilo ili TBS wafanye ndicho nilichoelewa endelea tu lakini kuchangia. (Makofi)

MHE. BONIPHACE M. GETERE: Mheshimiwa Spika, ahsante, nadhani hii suala la sheria hivi ngoja nikuulize sisi wote ni Wabunge hapa na wewe ni Mbunge hapa hivi tulipoamua kununua ndege tulileta sheria gani? Si tulileta ndege zikawepo,

Mheshimiwa Spika, mimi ninachokisema umezungumza vizuri sheria ziletwe wakati huo TBS iendelee ku-handle kwa sababu wale watu hawana mkataba TBS iendelee kuwa nalo hilo eneo wakati sheria zinafanya nini, zinaletwa shida iko wapi? Tusiwe watu wa kunyonywa mimi mambo ya kunyonywa ndio siyapenda humu ndani, tuhangaike kwamba hili neno linaendaje ili liweze kuleta mahusiano yetu kwenye mambo kama haya. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nadhani umeshauri vizuri sheria iletwe haraka, lakini wakati huo huo TBS iendelee kufanya hiyo kazi kwa sababu jamaa wale hawana Mkataba. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nilikuwa ninazungumza kukatika kwa umeme wa REA sasa mimi nashindwa kuelewa ni umeme wa REA ndio unakatika au Umeme mwingine ya mjini haukatiki, kwasababu vijijini umeme wa REA unakatika mara 10 kwa siku shida ni nini kama sisi tunaumeme wa kutosha wa megawatt za kutosha katika nchi hii leo shida ni nini umeme unakatika mara kumi kuna watu hawafanyi kazi shinda inatokea wapi kwenye jambo kama hili. Kwa hiyo, ndio maana nimesema hii Wizara tuiangalie upya tuweze kuigawanya ili iweze kufanya kazi vizuri. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, jambo jingine nililotaka kuzungumza ni suala la mradi wa mikakati tuna bwawa la Mwalimu Nyerere tuna mradi SGR suala zuri duniani ambalo Marehemu Dkt. Magufuli tutamkumbuka miaka nenda rudi ni kwamba bwawa la Nyerere mradi ule unaendeshwa kwa Mkopo ambao hautulazimishi kuchukua bwawa wenzetu wa nchi jirani miaka ya karibuni hivi inayokuja miradi mingi ya mikakati itakuwa ya watu Zambia tayari na maeneo mengine tayari, lakini bwawa letu la Nyerere na niombe kwa style mliyotumia ya kukopa kwa fedha ya hiyari tusiingie tena watu waje kuleta uhifadhi yaani kufadhili ile Rambo lile bwawa la Nyerere halafu liwe la watu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, hilo ndio jambo, marehemu amefanya jambo kubwa sana kwamba mradi ule sasa hata ukiisha madai yake sisi hatudaiwi kwa nguvu, tutadaiwa kwa hiyari, na hivyo hivyo kwenye reli wenzetu wanaojua miradi ya namna hiyo ya mikakati huko mbele sio yao itakuwa ya watu kwa hiyo ninafikiri kwamba tuendelee kufanya na mimi naona Mama amejitahidi sana kuwa karibu na Miradi ya Mikakati tumuombee Mungu aendelee kuilinda miradi ya mikakati ili nchi yetu iende salama, ahsante. (Makofi)