Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Rashid Mohamed Chuachua

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Masasi Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. RASHID M. CHUACHUA: Mheshimiwa Mwenyekiti, binafsi nampongeza Mheshimiwa Waziri kwa weledi wake katika kuhakikisha juhudi za kujenga Tanzania ya Viwanda zinafanikiwa. Kusini mwa Tanzania ni eneo ambalo viwanda vya korosho vilijengwa kwa kuwa ndiko mali ghafi hii inakozalishwa kwa wingi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni wazi kuwa juhudi za Serikali zinahitajika katika kufufua viwanda hivi kwa ajili ya kuinua uchumi wa nchi yetu pamoja na wakazi wa maeneo husika. Jimbo la Masasi lina kiwanda cha kubangua korosho ambacho hakifanyi kazi kwa muda mrefu sasa. Naomba majibu ya Serikali kuhusu mpango wa kuhakikisha kuwa kiwanda hiki kinafanya kazi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakusudia kutoa shilingi kwenye mshahara wa Waziri ikiwa katika majumuisho Serikali haitatoa kauli kuhusu suala hili.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.