Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki

Hon. Kenneth Ernest Nollo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bahi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki

MHE. KENNETH E. NOLLO: Mheshimiwa Naibu Spika, na mimi nikushukuru kwa kunipa nafasi ya kuchangia kwenye Wizara hii ya Mambo ya Nje. Nchi yetu imekuwa inaheshimika katika sura ya kimataifa kwa muda mrefu sana. Lakini heshima ambayo tumekuwa nayo tangu enzi ya awamu ya kwanza ni kutokana na nchi yetu kuwa na misimamo thabiti katika kutetea haki na unyanyasaji wa aina yoyote katika nchi mbalimbali hapa duniani. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, hatukujipambanua tu kwa kutetea haki kwa kutetea waafrika wenzetu wanavyosanyanyaswa au kuonewa lakini tumeenda nje kabisa ya Afrika na kutetea kokote duniani ambako tunaona haki inabinywa. Nataka niseme hili kwa kuangalia kwamba nchi yetu sawa inaingia kwenye uchumi wa dipomasia, lakini tunafika mahali sasa tunaanza kwenda kama watu wanaotaka kujiuza, tunapoteza heshima yetu, tunapoteza sisi tusema maskini ambaye sasa hana aibu.

Mheshimiwa Naibu Spika, maana sasa unaweza ukawa maskini, lakini aibu unayo, una heshima yako unalinda heshima yako. Nalisema hili kwa sababu moja, wiki mbili zilizopita dunia nzima imeona namna Palestina ilivyoshambuliwa kwa kiasi kikubwa ambacho binadamu yeyote hawezi akasema hiki ni kitu gani kinatokea. Nchi yetu hatujatoa hata tamko la kulaani, hata kusikitika. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, na mwingine anaweza aka-justify akasema mbona nao Hamas walikuwa wanarusharusha mawe upande ule, lakini ukiangalia kulichofanyika pale nchi yetu tulitakiwa tuweze kufanya condemnation kwa namna gani Palestina walivyofanyiwa. Hata Mwalimu alikuwa na msimamo thabiti kuhusu Palestina na msimamo wa nchi yetu ilikuwa ni kwamba pale inatakiwa mataifa mawili na juzi Rais wa Amerika huyu mpya amesema pale panatakiwa mataifa mawili. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa nataka nisema ni kwa nini tunaanza kupoteana, Waziri atuambie msimamo wetu kuhusu Palestina ni nini? Anachofanyiwa Palestina sisi msimamo wetu Tanzania ni nini? Hili Waziri atuambie na ikiwezekana basi leo alaumu kilichotokea juzi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, tulikuwa na msimamo mkali kuhusu Morocco, alijitangazia kwa west sahara anaitawala na sisi Tanzania tukawa wakali hata tukatoa influence yetu kwenye Umoja wa Afrika na Morocco akajaribu kuingia pale akazuiwa, lakini hili nalo tumepoteana kwanza tumefungua ubalozi wetu Algeria ambao ulikuwepo, lakini tume-extend na Morocco sasa tuna ubalozi ambao tunautumia ule wa Algeria. Lakini na hili nalo Waziri atuambie msimamo wetu kuhusu West Sahara ni nini? Tumekubali kwamba tunakuja kujengewa kiwanja basi imekuwa give and take tunawaacha West Sahara ambako ulikuwa msimamo wetu tangu awali. Hili nalo Mheshimiwa Waziri atuambie msimamo wetu kuhusu West Sahara ni nini sasa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nataka niseme kuhusu economic diplomacy ambayo wengi wameisema kwamba sisi tuangalie nchi yetu tunapata nini, ndio maana nikasema sasa ile ni maskini anayejirahisisha na nchi yetu imekuwa na heshima kubwa na watangulizi wetu walitumia damu na nguvu zote kutetea hili, lakini hatuwezi tukatumia kitendo cha uchumi wa diplomasia tuweze sasa kusema hili sisi walau kwa vile tunapata pesa basi hili tuliruhusu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, balozi zetu tunazifungua, lakini ni lazima tuangalie kwamba tunapata nini pale. Economic diplomacy isichukuliwe kwamba sasa tumekubali ubeberu ututawale tunavyotaka na vyovyote itakavyoenda lakini lazima tuseme hapana kwa imperialism, ni nchi yetu lazima iseme bado kuna shida ya ubeberu na ubeberu wa namna yoyote ile nchi yetu lazima isema hapana, tusipoangalia tutakuwa ma-purpet wa mabeberu na tutasema kila kitu tutakabiliana.

Mheshimiwa Naibu Spika, nataka niseme hili kwa sababu moja wakati corona inaingia nchi yetu watu waliishangaa na tulionekana hatufai kwa nini atufungii watu wetu ndani, na hili tulisimama kidete, lakini majirani zetu na Afrika wakaanza kuwaambia sasa chukueni package ya kujinusuru na ya kunusuru uchumi wenu na majirani zetu wamekopa IFM, World Bank, nani hela nyingi sana, lakini sisi msimamo wetu tulisema kwamba kwenye hili hapana kama wanataka kutusaidia basi watupunguzie riba ya madeni haya. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, na ninataka niseme na wizara waelewe tunakoelekea tunajipeleka kwenye chanjo, sawa, lakini kwenye jambo hili tuangalie tuwe na msimamo thabiti kwamba chanjo ile bado inazungumzwa kwa tofauti. Mheshimiwa Rais ameunda Kamati na imeshauri lakini ni lazima ndugu zangu wa Tanzania tuendelee kuliangalia hili. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, bado twendeni kwa kushtukastuka, tusiingize miguu yote, kama tulivyostuka hatua za awali za kufungia watu wetu bado na hili lazima twende kwa kustukastuka.

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo lingine ni kuhusu balozi zetu kama nilivyogusia tusipekele tu watu ambao wamesoma international relations, tupeleke watu mbalimbali wenye ujuzi, wataalam wa masoko, biashara, wa uwekezaji, lakini kwamba balozi anakuwa na afisa mmoja tu pale halafu mnategemea mpate chochote. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, unateuwa balozi kwenda Lubumbashi unamchukulia kwa minajili kwenda kusuluhisha tu migogoro, lakini bado tunanaangalia kwamba balozi wetu huyu atuletee nini Tanzania. Kinachotushinda ni kwamba tunashindwa sasa kuangalia potential zilizopo za kibiashara tuweze kuzileta hapa kwetu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lingine nilitaka nishauri, nchi yetu inavutia wawekezaji lakini tutaweza kupata wawekezaji wengi, lakini baadae tunaweza tukasema hawa watu wamekuja kutuibia kwa sababu moja tu, ukienda Malaysia kwamba mwekezaji lazima awe na mzawa, hapa kwetu tunasema lakini hatulifanyi, hata mzawa akiwepo anakuwa na ka-minor share na anakuwa diluted. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo hili tuliwekee mkazo kwamba ni lazima Mtanzania awepo kwenye kampuni ile na ashiriki kikamilifu, lakini kingine tuzalishe na sisi matajiri wa kwenda kuwekeza nje, Dangote yupo kwetu hapa ametengenezwa, lakini mkakati wa kumpeleka Bakhresa nje upo wapi, matajiri wetu mkakati wao huko wapi? Nataka nishauri kwamba Wizara ya Fedha na ninachukulia mfano wa nchi ya Ufaransa ina department ya Private Sector for Overseas Investiment na sisi tuwe na hicho na kitengo.

Mheshimiwa Naibu Spika, ndugu zetu wa China wakija hapa wawekezaji wao wanakopa hela kwenye Exim Bank ya China ndio maana inakuwa rahisi kuwekeza hapa kwetu. Sasa na sisi ni lazima tuwe na Overseas Department kwa ajili ya private sector ambayo itaweza kuwatafutia masoko, oppotunities na hata kuangalia namna gani Serikali iweze kufanya business negotiations badala kuwaacha waende namna hiyo walivyo.

Mheshimiwa Naibu Spika, tukifanya hivi tutasaidia nchi yet una kwa maana hiyo tutakuwa washindani katika biashara, katika shughuli za uwekezaji zinazofanyika na namna hiyo tutaweza kweli kusema tunatekeleza economic diplomacy.

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kusema hayo nashukuru sana na naunga mkono hoja, ahsante sana. (Makofi)