Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki

Hon. Vita Rashid Kawawa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki

MHE. VITA R. KAWAWA: Mheshimiwa Spika, na mimi nashukuru kwa kunipa fursa hii niweze kutoa mchango wangu kwenye Wizara yetu hii ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki. Naomba nianze kumpongeza Mheshimiwa Rais kwa kufanya teuzi nzuri za mabalozi hawa wawili, Mheshimiwa Liberata Mulamula kuwa Waziri wa Mambo ya Nje na Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk kuwa Naibu wake.

Mheshimiwa Spika, mimi naimani sana na mabalozi hawa, kubwa, kwani nawafahamu. Na ninamfahamu Mama Mulamula kuwa yeye ni mbobezi katika eneo hili la diplomasia. Na kwa muda mfupi tu ametuonesha kwa ku-stimulate diplomasia ya uchumi kati yetu na nchi zetu za Afrika Mashariki kwa kumshauri vyema Mheshimiwa Rais na kutembelea nchi hizi na kufanya mikutano ya kibiashara na hasa Kenya na kufanya kufungua biashara ya mazao baina ya nchi yetu ya Tanzania na Kenya.

Mheshimiwa Spika, mimi napenda kuishauri Serikali tuendeleze na kukazania sana diplomasia hii ya uchumi kwani wote tunafahamu nchi ikiwa na mahusiano mema ya kiuchumi naamini kabisa tutaweza kuuza biashara na bidhaa zetu nje kwa wingi na tukiuza nje kwa wingi tutapata fedha za kigeni, lakini pia tuta-stabilize uchumi wa nchi yetu.

Mheshimiwa Spika, hivyo nilikuwa napenda sana kuishauri Wizara ya Fedha iangalie diplomasia ya uchumi nayo ina gharama yake, mahusiano yana gharama yake kwa hiyo, tuangalie sana kupeleka fedha kwa wakati; kama ni OC tusipeleke OC za mishahara tu, tupeleke OC pia za kugharamia mahusiano haya ya diplomasia ya uchumi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwani tunaweza tukalaumu wakati mwingine tunaweza tukafika mahali tukalaumu ma-diplomat wetu waliokuwepo nje kwamba, wanachelewa kutekeleza majukumu yao ya diplomasia ya uchumi, sababu tu wanaweza wakawa wanakosa hata gharama ya kugharamia ile round coffee table ya kuweza kuwaita na kuwashawishi potential investors kwa kukaa nao na kunywa nao kahawa na kuwaelezea hali halisi ya kwetu na kushawishi waweze kufika huku. Kwa hiyo, ni muhimu sana Wizara ya Fedha kutenga na kusambaza fedha zile zinazotakiwa kwa ajili ya mabalozi wetu nje ya nchi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini lingine napenda sana kuishukuru Wizara kwa kutekeleza ushauri wa Kamati ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama ya kuona kuna umuhimu wa kuongeza watumishi katika balozi zetu hasa wanaohusiana na wenye utaalam wa kufanya kazi hii ya diplomasia ya uchumi. Tunawapongeza sana kwanza wameshatekeleza jukumu hilo na sasa wako katika uratibu nadhani wa kupeleka hawa ma-diplomat wetu katika maeneo hayo.

Mheshimiwa Spika, lakini pia naipongeza Wizara kwa kutambua na kushirikiana nao mabalozi wetu wastaafu, tumewaona leo wamekuja hapa. Mabalozi wastaafu hawa ni encyclopedia ya Wizara hii ya Mambo ya Nje na Waziri umedhihirisha mahusiano mema ya diplomasia kuwakumbuka na kuwatambua mabalozi hawa na leo kuwaleta hapa na kushirikiana nao. Mabalozi hawa ndio walifanya kazi kubwa sana katika nchi hii kipindi cha nyuma wakati wakiwa kazini kwa hiyo, ni vema wana uzoefu mkubwa sana. Wizara iendelee kuwatumia mabalozi hawa ili kutoa ushauri wao na experience yao katika Wizara hii na mahusiano ya kimataifa, lakini pia katika dilpomasia ya uchumi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, mimi nilikuwa na hayo tu machache, naomba nikushukuru na ninaunga mkono hoja. (Makofi)