Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

Hon. Shabani Hamisi Taletale

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Morogoro Kusini Mashariki

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

MHE. HAMISI S. TALETALE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Kwanza kabisa nashukuru, leo kwa mara ya kwanza na mimi nachangia kwenye Wizara ambayo imenilea. Ni Wizara ambayo upande wa sanaa najua madudu wanasema kindakindaki. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nianze na COSOTA. Naomba kumuuliza Mheshimiwa Waziri sisi tunafahamu wenzetu wa michezo wanaongoza michezo, mpira alikuwa kocha, alikuwa mchezaji lakini huku kwenye COSOTA sijui msomi kaoka wapi huko anakuja anaongoza COSOTA, hajui sheria yeye yuko busy tu kutung’ang’aniza wananchi tuseme tunafuata sijui utamaduni. Sawa, hakuna mtu asiyetaka kuufuata utamaduni wa nchi yetu, lakini COSOTA tumewekewa mapolisi ambao wanakwenda kuua utamaduni wa nchi, wanakwenda kuua muziki wetu.

Mimi nina mfano mmoja ambao mwaka jana, hapa kidogo na-declare interest, mwanamuziki wangu Diamond Platinum wimbo wake wa Hallelujah ulizuiliwa usipigwe na COSOTA, mwaka huo huo mwishoni waandaaji wa filamu ya Coming to America wakauchukua ule wimbo kama wimbo bora. Sasa wimbo umeenda kuwa bora nje ya nchi, nchi yenyewe yenye wimbo imeikataa. HaPa kuna walakini kwenye BASATA. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kingine ambacho naomba nizungumzie, wasanii wamekuwa wakilia sana sijui mirabaha, nini, hawalipwi. Leo hii media inalipa ili wasanii walipwe lakini COSOTA hawalipi. Mimi zamani nilikuwa napata pesa kutoka kwenye taasisi ya MCSK ipo Kenya na taasisi nyingine ya SAMBRO iko South Africa, COSOTA walipoenda kujiunga na SAMBRO, MCSK wasanii nchini hawalipwi. Hivi vitu viwili leo namwambia Waziri, nitamshikia shilingi mpaka nijue wasanii wanaanza kulipwa lini. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lingine ambalo mimi kiukweli linaniuma kwa sababu sisi ambao tunafanya burudani za viwanjani tumekuwa tukipigia simu sana kwa babu zetu vijijini, leo ziba mvua, zuia mvua. Katika hotuba ya Mheshimiwa Waziri, sijaona aseme kwamba kuna sports arena inakwenda kutengenezwa. Tumechoka kufanya event za wazi, tunahangaika kuwapigia simu mababu vijijini wazuie mvua. I am from Africa bro! (Makofi/Kicheko)

Mheshimiwa Spika, leo hii Rwanda ni nchi ambayo mpya tu leo hii wana sports arena yao, watu wa NBA wanakuja. Sisi hapa hatuna sports arena, sio tu hivyo wasanii wa Tanzania ni moja ya wasanii wakubwa East Africa, tunaongoza kwenye kila kitu. Tunapokosa kuwa na sports arena tunategemea kwenda kufanya show viwanjani, tunakosa kukuza sanaa yetu.

Leo hii nchi yetu Tanzania, hakuna asiyejua Afrika kama sisi ni corona free, wananchi wanaingia, tunakusanyika, hakuna tuzo za MTV South Africa kwa sababu watu hawakusanyiki. Wamekuja wanatuomba waje Tanzania lakini sisi tunawaambia hatuna sports arena. Wanashangaa, hee, hiyo nchi gani? Ni nchi ambayo ina uhuru, ina amani, viongozi wake tumekuwa tukiahidiwa tu tutajenga sports arena. Leo hii tumeenda kutafuta wawekezaji jamni twendeni tukatengeneze sports arena nchini kwetu. Lakini hivyo vigingi vilivyotokea hapo katikati. Sasa sijui ni Waziri hutaki tupate na sisi sehemu yetu ya kujistiri au samahani ingawa sio mtani wangu, lakini sijui na wewe unapenda tukakae vilingeni tuzuie mvua bila sababu. Kwa sababu kama unafanya show Dar es Salaam, Morogoro na kadhalika.

Mheshimiwa Spika, unakumbuka tulifanya show hapa uwanjani mwanzo mwisho ilikuwa ni mvua. Sasa inakuwa shida. Mimi nikumbushe kitu kimoja, mwaka juzi tulifanya show Sumbawanga, nakumbuka Mkuu wa Mkoa alinipa mganga wa mkoa, huyo mganga wa mkoa akaniambia hapa mvua itafungwa usiwe na wasiwasi. Ndani ya uwanja kulikuwa kuna wananchi 7,000; nje nina watu kubao. Sasa tukitaka kutoka na wasanii kwenda uwanjani ile mvua inatufuata shiiiiii, tukitaka kurudi inarudi. (Makofi)

Mheshimia Spika, tuliingia uwanjani kama unakumbuka ile show ambayo wasanii wangu walidumbukia, watateleza, wakadondoka. Hivi ni vitu ambavyo vinatuumiza sisi, naongea kama natania, lakini Mheshimiwa Waziri umezungumza bajeti yako yote sijakuona ukizungumzia sports arena. Mimi ni mmojawapo ambao nitakataa kuunga mkono bajeti yako kwa sababu naona hauungi mkono maendeleo ya muziki wa Tanzania. Kwa sababu hatuwezi, leo muziki umekua. Tunatoka hapa wasanii wanakwenda kufanya show nje…

MHE. AIDA J. KHENANI: Mheshimiwa Spika. Taarifa.

SPIKA: Kuna Taarifa. Endelea.

T A A R I F A

MHE. AIDA J. KHENANI: Mheshimiwa Spika, nataka kumpa mzungumzaji kwamba Sumbawanga hatuna shida hiyo, siku nyingine akija, afuate utaratibu tu mambo yatakwenda sawa. (Makofi)

MHE. HAMISI S. TALETALE: Mheshimiwa Spika, Taarifa nimeipokea na kweli, shida hawana ila balaa lilikuwepo. (Makofi/Kicheko)

SPIKA: Mheshimiwa kule Sumbawanga wake za watu tu, basi! Endelea. (Kicheko)

MHE. HAMISI S. TALETALE: Mheshimiwa Spika, hivi ni vitu ambavyo vinatokea kwenye sanaa yetu. Kama Serikali inakosa kutufikiria kwenye suala zima la kuwa na ukumbi na Serikali inaandaa bajeti inakuja kutusomea bajeti mpaka inamaliza haijatamka wala haijaonesha dhamira ya kwamba leo hii tutakuwa na sehemu ya sisi wasanii kwa ujumla kupata sehemu ya burudani, hii inasikitisha sana Mheshimiwa Waziri. Mimi nikuombe, nashindwa kukuambia uende ukajipange tena, ila jipange na Wizara yako tunahitaji kupata sports arena nchini. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini pia, kuna kipindi nilizungumza na Katibu Mkuu wa Wizara yetu akaniambia wanapigania kuwa na sports arena Dodoma, Hee! Mheshimiwa siiombei hata Morogoro Kusini Mashariki wala Morogoro, iko wazi kabisa mji wa burudani na starehe ni Dar es Salaam. Kwa hiyo, tunatakiwa kama tunawaza kuwa na sports arena, Ikakae Dar es Salaam. Isiende Morogoro, isije Dodoma ikakae Dar es Salaam. Lakini ikitokea leo hii tunakaa hapa, Mheshimiwa Waziri amesimama, amezungumza mpaka amemaliza bajeti yake sijaona azungumzie hicho kitu. Mimi inaniumiza, hakuna msanii asiyejua kama mimi ndiye ninayeongoza kufunga mvua. Kwa sababu ya mila zetu za Kiluguru, mimi ni mziwanda, mziwanda ndiyo mfunga mvua sio uchawi wa ushirikina, I am from Africa! Hilo liko wazi. (Makofi)

Naomba unipunguzie hii kazi Mheshimiwa Waziri, naomba unipunguzie hii kazi, inatuchosha. Mpaka unamaliza bajeti yako unazungumza sijaona ukizungumza kuhusu viwanja. (Makofi/Kicheko)

Tunaomba tupate kiwanja na sisi wasanii wawepo indoor, wafanye burudani zao na usituletee kiwanja cha watu sijui 20,000/30,000 ikiwa tunakwenda nje ya nchi kama Mali na kadhalika tunajaza viwanja vya mpira leo hii tunataka kiwanja kikubwa cha burudani nchini. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, cha mwisho kabisa hawa Marais wetu, kuna sijui Rais wa Ngumi, sijui Rais wa nini. Nchi yetu ina Rais mmoja tu, R ni moja tu, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Samia Suluhu Hassan. Mheshimiwa Waziri naomba hawa Marais, sijui wa Shirikisho, sijui TFF, zitoke wawe na vyeo vyao. Wanapunguza heshima ya neno Rais na wanaitoa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, mtu unamuona Rais kabisa Rais ana vumbi. Rais hawezi kuwa na kiatu kina vumbi. Tunatakiwa tuheshimu neno Rais. Eti Rais wa Wasafi! Hawezi kuwa Rais! (Makofi)

MHE. HUSSEIN N. AMAR: Mheshimiwa Spika, Taarifa.

SPIKA: Mheshimiwa Amar nimekuona.

T A A R I F A

MHE. HUSSEIN N. AMAR: Mheshimiwa Spika, naomba nimpe Taarifa mzungumzaji, kwa kweli, hili suala la Rais, hata sisi kule tuna Rais wa Wachimbaji, hili linakera sana. Nilikuwa nampa Taarifa hiyo. (Makofi)

SPIKA: Kwa kweli jambo hili linakera. Mheshimiwa Waziri Mkuu, hawa Marais, hata Yanga wana Rais wa Yanga, hii haiwezekani! (Kicheko)

Mheshimiwa Babu Tale endelea bwana! (Makofi)

MHE. HAMISI S. TALETALE: Mheshimiwa Spika, hili suala la Marais kwa kweli linakera. Tuache maana ya Rais ibakie kuwa moja, nchi ina R moja tu. Tuna Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Rais Samia Suluhu Hassan. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, anatokea Rais anasimama eti yeye ni Rais, ana kiatu kina vumbi, ina maana Rais! Tuheshimu majina tunayopeana, ndiyo maana mimi nimejiita babu, kwa sababu nikijua kabisa kama babu ni mzee, mimi ni mzee kwenye industry yangu ya bongo fleva, ni mzee kwenye industry ya music in general.

Mheshimiwa Waziri, milango yangu iko wazi, nakukaribisha ukihitaji ushauri wowote, ila nitakuonea huruma sana na wewe ukiwa katika watu ambao eti wasanii wakifanya kiki zao ninyi mkaziingilia mkazitamka. Nilimuona Mheshimiwa Naibu Waziri akizungumzia kiki ya mmoja wa wasanii wangu. Ilinisikitisha sana na nilikuambia kama nisingekuwa Mbunge angeona rangi ya pili ya tabia yangu. Lakini kwa sababu naona ah! Marekani kuna msanii anaitwa Sixnine Tekashi, ni mmoja ya wasanii kichaa, lakini moja ya msanii ambaye anatengeneza pesa kuliko wasanii wengine wote kwa kipindi hiki. Lazima tujue kutofautisha kiki ambayo inatengeneza pesa, kiki ambayo isiyotengeneza pesa.

Mheshimiwa Spika, kikubwa wasanii wetu wanatuletea heshima, kikubwa wasivunje maadili. Ukiwa kama Waziri au Naibu Waziri ukawa wewe sasa unakwenda kumzuwia msanii asifanye kile ambacho kinamtengenezea faida yake, wewe upo busy kama mtu unaonekana kama sasa unapinga maendeleo ya sanaa nchini. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, niwaombe, nikuombe Mheshimiwa Waziri, hakuna kitu ambacho kinawaliza wasanii kama hiyo system yenu ya BASATA ya kumuona kila msanii kumfungia. Hii ni taasisi, tunaomba ipewe watu ambao wanahusiana na sanaa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nashindwa kuunga mkono hoja mpaka ninapoona uwanja, arena. Ahsante. (Makofi)