Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Viwanda Na Bishara

Hon. Dr. Charles Stephen Kimei

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vunjo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Viwanda Na Bishara

MHE. DKT. CHARLES S. KIMEI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninapongeza hotuba nzuri ya Waziri wa Viwanda na Biashara, nampongeza yeye mwenyewe Waziri, Naibu Waziri, Katibu Mkuu na uongozi mzima wa Wizara kwa kazi nzuri na ubunifu katika kutekeleza Sera na Ilani ya chama tawala.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kinachosikitisha sana ni Wizara hii inayobeba dira ya Taifa letu kwa sehemu kubwa kutokupewa kipaumbele cha kufikishiwa fedha zilizoidhinishwa kwenye bajeti ya maendeleo. Kwa mwaka 2020/2021 ilipata chini ya asilimia 50 ya bajeti na hivyo kushindwa kutekeleza miradi ambayo ingewezesha kujenga misingi bora ya kuwezesha wananchi wajasiriamali kuanzisha shughuli za uzalishaji na kutengeneza ajira.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ujenzi wa majengo/ mabanda ya kuwapangishia wajasiriamali wadogo wadogo na wa kati ni falsafa nzuri kwani inawezesha pia kuwafikishia wajasiriamali hawa huduma na mafunzo mbalimbali, na pia kuwasimamia wale wanaopewa mikopo na SIDO kutumia mikopo hiyo vizuri. This be Serikali ikubali kutenga fedha nyingi zaidi kwa utekelezaji wa mkakati huu na kwa Mfuko SIDO wa kuwezesha wajasiriamali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mashirika ya TIRDO, CAMARTEC, TEMDO yanafanya ubunifu mzuri na unaozingatia uwezekano wa kupeleka kwenye soko letu teknolojia sahihi kwa mazingira yetu na kwa bei nafuu. Hata hivyo taasisi hizi hazipati bajeti za kutosha kujitangaza na kupeleka taarifa sokoni kwa walengwa ili wazijue na wazinunue. Kwa namna hii zinapoteza tija. Wapewe rasilimali fedha na watu wa kueneza kile walichobuni.

Mheshimiwa Mwenyekiti, aidha, mashirika mengi yaliyo chini ya Wizara hii hayana bodi. Hii inapunguza kiwango cha utawala bora. Tuiombe mamlaka husika ifanye uteuzi kwa wakati.

Mheshimiwa Mwenyekiti, utekelezaji wa blueprints unastahili kuongozwa na Wizara hii licha ya kwamba Wizara nyingine zina maeneo yao. Blueprint inatekelezwa kwa kasi ndogo, lakini kuna haja ya kufanya tathmini mpya kuhusu kero mpya zilizoibuka kwa wafanyabiashara na wawekezaji. Kero zilizoorodheshwa miaka mitatu iliyopita zimepitwa na uhalisia wa sasa.