Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Viwanda Na Bishara

Hon. Amb. Dr. Pindi Hazara Chana

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Viwanda Na Bishara

MHE. DKT. PINDI H. CHANA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuunga mkono hoja ya Viwanda na Biashara.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu Mchuchuma na Liganga; je, Mradi wa Mchuchuma na Liganga utaanza lini? Mbona umetengewa fedha chache sana Mchuchuma na Liganga.

Kuhusu diplomasia ya uchumi (economic diplomacy) taarifa mbalimbali za biashara na viwanda ziende katika Balozi zetu ili waweze kuwajibu haraka wawekezaji huko huko Ubalozini.

Katika Balozi zetu tupeleke trade attaches na tuwape link kila Balozi ili wawasiliane na Wizara ya Viwanda kupata taarifa muhimu kwa ajili ya masoko ya korosho, chai, pamba parachichi na kadhalika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, parachichi Njombe; parachichi inahitaji muuzaji wa kuuza nje aje na accreditation registration na registration hii hufanyika kwa gharama kubwa sana. Wizara ina mpango gani wa kusaidia wakulima wa Njombe wa zao la parachichi.

Kuhusu mahindi; zao la mahindi Wizara iweke mkakati wa masoko ya uhakika, hivi sasa bei ya mahindi kwa debe ni shilingi 4000; pembejeo ni gharama sana, Wizara isaidie bei ya mbolea na pembejeo ishuke.