Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Viwanda Na Bishara

Hon. Zuberi Mohamedi Kuchauka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Liwale

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Viwanda Na Bishara

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, viwanda vyetu vinashindwa kwenda kwa faida kwa kuwa na mamlaka nyingi za usimamizi zinazofanya kazi zinazofanana kama vile OSHA, TBS, TFDA NEMC na zingine mfano wa hizi. Kwa nini mamlaka hizi zisiunganishwe zikafanya kazi chini ya taasisi moja?

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunahitaji Serikali yote iongee kwa pamoja kwani ni Serikali ni moja, mfano kuna mazao ya kimkakati, je, vipo viwanda vya kimkakati vinavyokwenda sambamba na mazao hayo ya kimkakati?

Je, Wizara ya Miundombinu inayo miundombinu inayolingana na viwanda, au mazao hayo ya kimkakati, miundombinu ya barabara, bandari na uchukuzi kwa ujumla wake? Je, ni rafiki sawa na mikakati ya Wizara ya Viwanda? Je, Wizara ya Mazingira nayo inaitambua mikakati ya Wizara ya Viwanda na Biashara, kwani kwa uzoefu unaonesha Wizara ya Mazingira inaongoza kukwamisha uwekezaji nchini kwa hoja ya uharibifu wa mazingira.