Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Viwanda Na Bishara

Hon. Priscus Jacob Tarimo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Moshi Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Viwanda Na Bishara

MHE. PRISCUS J. TARIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nikushukuru sana kwa nafasi ya kuweza kuchangia lakini pia nianze kwa kuwapongeza sana Mheshimiwa Waziri, Naibu Waziri, Katibu Mkuu na watendaji wote kwa uwasilishaji mzuri na uandaaji mzuri wa bajeti ya Wizara yao. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi nitaenda haraka haraka ili niweze kuongelea mambo mengi zaidi. Nianze kwa kuunganishwa kwa TBS na TFDA pamoja na marekebisho ambayo yametajwa kwenye hotuba ya Mheshimiwa Waziri kwenye ukurasa wa 18. Nia ya kuunganisha taasisi hizi za TBS na TFDA ilikuwa nzuri sana ili kuboresha utendaji. Lakini badala yake imeleta vikwazo, shida katika utendaji. TBS sasa imekuwa ndiyo mamlaka ya ku-standardize na ku-regulate majukumu ambayo kikawaida yasingetakiwa yafanyike na taasisi moja. Badala yake sasa kumesababisha kuwepo kwa bidhaa fake sokoni, hasa bidhaa zinazotoka nje. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaweza kutoa mfano; kwa mfano, maziwa ya watoto wachanga, sheria inasema yale ambayo yameshakubaliwa sasa ambayo yamepiwa yanaonekana yana vigezo yawe na maelezo kwa Kiswahili kwa maana ya kwamba ingredients na vitu kama hivyo. Lakini sasa hivi ukitoka tu hapo nje ukienda supermarket yamejaa maziwa ambayo hayana vigezo na yapo sokoni.

Kwa hiyo, TBS ilipounganishwa na TFDA, badala ya kuleta kheri imeleta tatizo. Ni vizuri sheria ile iliyopitishwa basi iweze kutofautisha majukumu ndani ya TBS kwamba yale ya ku-standardize yasimamiwaje na haya ya ku-regulate yaweje kwa sababu ya kuiunganisha…

MHE. NEEMA K. LUGANGIRA: Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa.

MWENYEKITI: Taarifa Mheshimiwa Neema.

T A A R I F A

MHE. NEEMA K. LUGANGIRA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru, ningependa kumpa Taarifa mzungumzaji hiki anachokisema cha jukumu la kuangalia ubora na usalama wa chakula ilivyoondolewa kutoka TFDA kwenda TBS inahatarisha sana maisha ya Watanzania. Unakuta wengi wetu tunanunua labda boksi ya juice ya machungwa tukijua kwamba lile ni chungwa halisi, lakini kihalisia ndani yake kunakuwa na concentrate, ladha na rangi. Kitu ambacho ni hatarishi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, naomba kumpa taarifa kwamba TBS na Wizara lazima iangalie namna gani ya kuandaa kanuni zitakazomlinda mlaji na kutoendelea kuweka maisha ya Mtanzania rehani. Ahsante. (Makofi)

MWENYEKITI: Mheshimiwa Priscus.

MHE. PRISCUS J. TARIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naipokea na ni ufafanuzi mzuri wa hiki nilichokuwa nasema kwamba haya majukumu yalivyopelekwa pamoja yameleta matatizo badala ya kuleta heri. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, niende moja kwa moja kwenye viwanda. Wakati viwanda, hasa vile vilivyokuwa vinamilikiwa na Serikali vinabinafsishwa kulikuwa kuna taasisi mbili zinahusika; viwanda vilivyopitishwa kwenye LAT na vile vilivyopitishwa kwenye PSRC. Vile vilivyopitishwa kwenye LAT ni vile ambavyo vilikuwa liquidated. Yaani vilikuwa vinauzwa, na ile ilikuwa ni discretion ya mnunuaji afanye nini. Lakini vile vilivyopitishwa PSCR ilikuwa ili viweze kuboreshwa, viongezewe mtaji, teknolojia, vitoe ajira na vilipe kodi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pale Moshi Mjini vipo viwanda vingi amevitaja Mheshimiwa Ndakidemi sasa hivi. Kiwanda cha Kibo Match, Kibo Paper na viwanda vingine. Vile vilibinafsishwa ili viendelezwe, lakini vimefungwa havifanyi chochote. (Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha muda wa Mzungumzaji)

MHE. PRISCUS J. TARIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.