Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Viwanda Na Bishara

Hon. Lucy Thomas Mayenga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Viwanda Na Bishara

MHE. LUCY T. MAYENGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipatia nafasi ya kuweza kuchangia Wizara hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze kwanza kabisa kwa kumpongeza sana Mheshimiwa Rais wetu Mama yetu mama Samia Suluhu kwa kweli kwa jinsi alivyoweza kubadilisha taswira ya biashara katika Taifa letu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunapokaa, watu wanapokaa kila kona kuzungumzia masuala ya kipato au kuweza kulalamikia kipato, hakuna njia yoyote inayoweza kusaidia wananchi hawa wakaja kuridhika zaidi ya biashara. Ninasema hivyo kwa sababu biashara zote duniani utakuta inagusa kilimo, biashara zote duniani utakuta inagusa mambo ya Liganga, Mchuchuma, biashara zote duniani kuna sehemu ambapo mwananchi atafaidika kwa njia moja au nyingine.(Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini ambacho wasiwasi wangu, ambacho nakiona ni kwamba mitazamo ambayo wanakuwa nayo viongozi wetu wakubwa na hasa niseme Marais wetu na hawa viongozi wengine wakubwa Waziri Mkuu, Makamu wa Rais wakikaa kuongea na wafanyabiashara, wakikaa kuongea kisiasa, ni vitu havifanani kabisa na mawazo ambayo yapo huku chini kwa watendaji. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi ninachokiona ni tatizo la sisi Watanzania hasa huku kwenye watendaji tubadilishe mindset na siyo kitu kingine. Tumekaa kwa muda mrefu sana tunazungumzia changamoto zilizopo kwenye biashara, baada ya hizi changamoto wakasema tuje na kitu kinaitwa blueprint, lakini blueprint hii ni karatasi, blueprint hii ni kitu ambacho kimeandikwa, kinataka mtu aje sasa aseme kwamba hiki tutakitekeleza kwa aina gani. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kingine hata kwenye kuchukua hizi hatua tuwe basi tunachukua hizi hatua haraka haraka, niwapeni mfano, kwa mfano, sheria zetu sisi hapa Tanzania kwa muda mrefu hazifungamani, yaani sheria za kodi na sheria za kibiashara zipo tofauti sana. Mtu akija hapa kwa mfano mtu akitoka popote una mtaji wako hata wa dola laki moja, dola laki mbili, ukisema nataka kwenda kufanya biashara fulani, yaani mchakato jinsi utakavyokuwa na jinsi utakavyosumbuliwa kwenye hicho ambacho unakifanya mpaka unakata tamaa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini yote haya viongozi na watendaji Serikalini huko wanayajua kwa nini hawachukui hatua? Ndiyo maana ninasema kwamba viongozi wanaweza wakawa na mawazo mazuri sana, lakini huku chini lazima tubadilike.

Mheshimiwa mwenyekiti, nitoe tu mfano wa mambo kama mawili, matatu hapa Tanzania kuna viwanda viwili tu vya mabati, viwanda hivi ndivyo ambavyo vinafanya kazi ya kuzalisha mabati hapa Tanzania, lakini wafanyabiashara ambao wana mawazo au wanamitaji ya kufanya biashara hii wapo wengi sana. Sasa kinachofanyika ni kwamba kunakuwa na kama kautaratibu kaku-monopoly biashara, mtu anakuja anakaa anakwenda kuongea na watu anaowajua mwenyewe huko akienda kuongea nao ninyi ambao mnataka kufanya hiyo biashara kila mkijitahidi kufanya mnashindwa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa ndiyo maana nimesema tubadilishe mindset, sasa matokeo yake wafanyabiashara hivi sasa wameamua badala ya kuzalisha bidhaa hapa Tanzania wanaamua kwenda Kenya na Uganda kwa sababu kule walipi kitu, wanakuja wanaingiza hapa Tanzania ndiyo wanafanya biashara. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, viwanda hivi tunavyokaa kupiga makelele viwanda vitawezaje kuanzishwa kwa utaratibu huu. Kodi hizi kwa nini haziwi na mwingiliano yaani kwamba tukisema kwamba tunamfutia kodi hii, import duty, tukisema tunafuta import duty tunaacha VAT tufanye haya mambo kwa sababu ya kuweza kusaidia watu waanzishe viwanda na mambo mengine yaendelee. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine, mtu leo hii ukisema kwamba mimi nataka nifanye biashara, mfano labda kama dawa za minyoo, dawa za mifugo, nataka niingize hapa Tanzania, ukiwa na kiwanda hapa Tanzania ile dawa ni ghali kuliko ambayo inatoka nje kwa sababu ya changamoto ya kodi, sasa mtu anafikiria mimi namtaji wangu hakuna mfanyabiashara ambaye hataki faida. Mimi ninamtaji wangu nasema nataka nifanye biashara ya aina fulani halafu nikipiga mahesabu naona kwamba kuanzisha kiwanda hapa Tanzania, najiona kwamba kiwanda kile sawa kuna faida kitaingiza, kitaajiri watu na kadhalika, lakini faida yangu itakuwa ndogo tofauti na ile faida ambayo utaipata kwa kuagiza kutoka nje.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ndiyo maana changamoto licha ya kwamba sijui kuna mazingira biashara, jamani wawekezaji mje mfungue viwanda, siyo rahisi mtu kuja kuanzisha kiwanda hapa Tanzania kwa mazingira haya yaliyopo ya hizi sheria, kanuni, taratibu na haya masuala ya kodi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini vilevile sheria hizi hizi leo mimi nimekaa nataka nianzishe kwa mfano labda kiwanda, mimi naomba niwaulize Wizara hii ya Viwanda na Biashara hivi hivi viwanda tu vilivyopo wanavitembelea kwenda kuangalia kinachozalishwa? Kwa sababu huku chini kwa wananachi mwananchi leo hii, Mheshimiwa Subira amesema pale kwamba kuna viwanda vingi sana kwenye Mkoa wa Pwani, kuna viwanda vya tiles na kadhalika. Lakini zile bidhaa ambazo zinazalishwa kwenye hivi viwanda wakati hawa wawekezaji wanakuja, walikuwa wanaamini kwamba watumiaji wa bidhaa hizi mtu analenga soko la lile eneo ambalo anaanzisha ile biashara. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kinachofanyika kwenye Wizara hii ya Viwanda na Biashara hawaendi kukagua hizo bidhaa, wala kwenda kuangalia nini kinaendelea kwenye uzalishaji, wala kwenda kuthibitisha kwamba hiki kinachozalishwa kina ubora, hivi mnafanya nini ofisini? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kinachotokea sasa watu wanakuja wanaanzisha biashara, wakianzisha biashara, mtu anaanzisha biashara let’s say kiwanda cha tiles, wanunuzi wanakosekana kwa sababu mnunuzi anaangalia quality, akishaangalia quality anasema hivi hapa nilipo nikinunua box moja la bidhaa labda let’s say ya tiles za Tanzania na tiles za China nikiongeza shilingi 10,000 tu, napata hii ya China ambayo fundi anamthibitishia kwamba bora ununue hii itadumu zaidi kuliko hii ambayo inatengenezwa Tanzania. What is this? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa nini Wizara ya Viwanda na Biashara haiendi kuangalia ubora wa bidhaa ambazo zinazalishwa? Hii ni hatari kubwa sana kwa sababu mwisho wa siku hivi viwanda vita-collapse, watu watakaa wanasema karibuni tutawahamasisha kwa njia nyingi sana, Mheshimiwa Mama Samia ameweka mazingira mazuri sana. Lakini kama sisi wenyewe hatutakuwa serious kwenda kuangalia mambo ambayo yanafanyika huko, tusikae mwishowe Mbunge mmoja hapa ameelezea, hapa Tanzania tatizo letu ni kama vile kila mtu yaani kwamba elimu ni huyu, wa elimu ndio kinamuhusu peke yake, huyu mwingine wa maji kinamuhusu peke yake, kwenye viwanda huku mambo ya fedha, mambo ya kodi ni mwingine yaani hatushirikiani, hakuna co- ordination. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, haya mambo tukiendelea kuyafanya namna hii tutakuwa tunaongea, viongozi wetu watakuwa wanahubiri haya mambo sana, wananchi wetu watakuwa wanalalamika kwamba pesa hatuna mifukoni, wakati sisi ambao tuko kwenye nafasi hizi za kufanya utendaji huu wa kuthibitisha na ni vitu vya kukaa tu na watu tukawasikiliza na kuthibitisha. Mwisho wake tumekaa hapa tukazungumza sheria ya TIC, na namshukuru sana Mheshimiwa Rais pia ali-mention hili, mtu anakuja na mtaji wake anasema kwamba, mimi nimekuja. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, maana tunamkaribisha mwekezaji, tunamuambia kwamba ukija Tanzania utaingiza wafanyakazi moja, mbili, tatu na kadhalika, lakini huku unampa unamnyang’anya kwa mlango wa nyuma. Sheria ya TIC na yenyewe pia kwanza ni ya muda mrefu sana mwaka 1972 inatakiwa kubadilishwa, lakini mpaka leo ni mambo yale ya Serikali mambo yanakwenda hivi na nini tunatumia muda mrefu sana. Mtu anakuja na mtaji wake, mimi nina mtaji wangu wa dola 500,000 au dola 1,000,000 nimekuja hapa Tanzania baada ya kufika hapa nakaa naanza kuwekeza kwenye masuala labda pengine kwenye biashara fulani. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nasema kwamba kwa mimi kwa pesa yangu namuamini dada yangu Esther huyu akinisimamia hapa, yaani hatakuwa na mambo ya ajabu ajabu, namuamini aidha ndugu yangu au ni mtendaji wangu. Halafu sheria inakuambia kwamba umeshafika umeshawekeza mtaji wako, lakini inabidi kwa kweli hapa kwasababu kuna mtanzania mwingine ana elimu kama hiyo kwa nini huyu asifanye. Mwisho, vitu vingine mtu anaangalia kwamba, yeye na huyu mtu wana historia gani, wana ukaribu gani, wako pamoja kwa kiasi gani, uaminifu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwentekiti, mwisho, lakini naunga mkono hoja. (Makofi)