Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Viwanda Na Bishara

Hon. Condester Michael Sichalwe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Momba

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Viwanda Na Bishara

MHE. CONDESTER M. SICHALWE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa fursa na mimi kwanza nianze kwa kupongeza wasilisho kutoka kwa Mheshimiwa Waziri wa Viwanda na Biashara. Na mimi naomba kutoa mchango wangu katika maeneo matatu kama muda utakuwa rafiki.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sehemu ya kwanza kabisa nataka kutoa mchango wangu kwa kuishauri Serikali ni kwa namna gani iweze kutusaidia wananchi wa Tanzania kuendesha biashara zake, lakini kwa kuangalia na kasi halisi ya teknolojia ambayo iko duniani ili iweze kutusaidia kuendana na mataifa mengine na kukimbizana sawasawa na wenzetu ambavyo wanakimbizana huko kwenye mataifa ambayo yameendelea ambayo yanatumia teknolojia katika kufanya vizuri kwenye biashara. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mchango wangu wa pili ni kuomba ni kwa namna gani Serikali inaweza kuwekeza nguvu kubwa kwenye maeneo ya mipaka maana kuna fursa nyingi sana ikiwa ni pamoja na kufungua viwanda kwenye maeneo ya mipaka, lakini pia hata kuboresha mazingira mazuri ya biashara kwa sababu panapatikana ajira nyingi, kuanzia vijana, wazee, watu waliosoma na ambao hawajasoma.

Mheshimiwa Mwenyekiti, na eneo la tatu, nitataka kuchangia na kuishauri Serikali kwamba vijijini akina mama wengi wameonekana ndio ambao wanatengeneza pombe za kienyeji na pombe hizi za kienyeji kwa kule vijijini zimeonekana zikipendwa sana. Basi kwa nini Serikali isitafute namna nzuri ya kuwasaidia akina mama hawa kuboresha ujuzi wao ili itusaidie kutoku-import pombe nyingi kutoka mataifa ya nje, tutumie ujuzi wa akina mama hawa ili kuendelea kutengeneza pombe zetu hapahapa kwa watu ambao ni watumiaji wa pombe waendelee kutumia vitu vyetu halisi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikienda kwenye teknolojia za biashara ambazo ziko duniani, naomba kuanza na namna gani ambavyo toka dunia ilivyokuwa imeanza kuna mifumo mbalimbali ambayo ilikuwepo ya biashara. Mfumo wa kwanza wa biashara uliokuwepo ni mfumo wa barter trade. Barter trade ilikuwa inafanyika katika mfumo kwamba kulikuwa hakuna means of exchange, kwa hiyo, biashara zilikuwa zinafanyika kwa kubadilishana bidhaa na bidhaa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini baada ya hapo, mfumo huo ulikuja ukapita baada ya dunia kuendelea tukaja kwenye metal au coin ambapo vito au dhahabu vilitumika kama means of exchange. Baada ya hapo dunia ikaondoka tukaingia kwenye paper (cash) ch currency, maana yake hapa tunaangalia Tanzanian Shilling, Kenyan Shilling, Zambian Kwacha, Nigerian Naira, Pula na pesa mbalimbali kutoka kwenye mataifa mengine.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya hapo tunaendelea tuko kwenye huu mfumo, lakini tukaja kwenye mfumo mwingine ambao tunaita credit card ambao hata sasa hivi bado tunatumia, kwamba watu hawataki kubebeshana pesa nyingi, lakini mtu unapokuwa na kadi unaweza ukafanya transaction mahali popote pale.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mfumo wa nne uliofuata ambao sasa dunia ipo na ndipo mahali ambapo dunia inatengeneza pesa nyingi sana, ndipo mahali ambapo hata matajiri wengi ambao wamepata kutokea katika kipindi cha miaka 15, ninapowaongelea Bill Gates, Alibaba, wametokana na mfumo huu wa teknolojia ambao umegawanyika katika phases mbalimbali. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hapa naongelea fourth industrial revolution ambayo ndani yake kuna block chain technology. Kwenye block chain technology kuna teknolojia nyingi; watu wa sheria wanaweza wakaitumia block chain technology, watu wa ardhi wanaweza wakaitumia block chain technology, lakini hapa nataka niongelee kwenye mambo ya fedha namna gani block chain technology inatumika, na zaidi ya hapo nataka kuongelea kwenye digital currency.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hapa kwenye digital currency, hii ni teknolojia ambayo ni kubwa sana lakini kwa bahati mbaya tafsiri ambazo tunazipata sanasana kwenye Nchi kama Tanzania na nyingine za Afrika, tunashindwa kuitafsiri vizuri teknolojia hii. Na hakuna namna tunaweza tukaizuia teknolojia hii isije kufanya kazi, na tayari huko duniani kuna watu ambao wametokea matajiri wengi sana kwa kupitia block chain technology ambayo ndani kuna digital currency.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hapa kwenye digital currency nataka kuziongelea baadhi ya currencies. Mfano naziongelea bitcoin, ethereum, theta, bitcoin cash, litecoin na ripple, na zipo coin mbalimbali. Lakini hapa nataka kuiongelea zaidi coin ya bitcoin. Coin hii mpaka sasa Tanzania hatufahamu kwa upana namna bitcoin inavyofanya kazi, na Watanzania wengi wamekuwa wakiendelea kupoteza fedha zao kwa sababu wanadanganywa, hawajui. Lakini kama Serikali ingekuwa imeamua kulivalia njuga jambo hili wakaamua kuwekeza kwenye elimu kuna vijana wengi wa Kitanzania ambao wanaulewa mkubwa na wimbi kubwa sana la vijana ambao wapo wengine wanafanya na wanatengeneza hela, lakini pia Serikali inapoteza mapato yake kwa kiasi kikubwa sana kupitia hili eneo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mfano leo nikiongelea, jana bei ya bitcoin ilikuwa milioni 92 za Kitanzania, nachukulia mfano mtu kwa mfano South Africa kuna ATM ya bitcoin, Kenya kuna ATM ya bitcoin lakini sasa hivi tuchukulie mtu anatuma hela kutoka South Africa anamtumia Mtanzania aliopo hapa, hakuna namna yoyote ambayo BOT wanafuatilia transactions hizi kwa sababu mambo yote yanafanyika online, mambo yote yanafanyika kwenye internet.

Mheshimiwa Mwenyekiti, na hata ilipotokea wakati ambapo Serikali iliamua kuzifunga zile bureau nyingi ambazo zilikuwa zipo Arusha na sehemu zingine, bureau nyingi ziliamua kuhamia kwenye online kwa mfano Serikali haijui kuna kitu kinaitwa remitano, Serikali haijui local bitcoin, Serikali haijui kuna kitu kinaitwa e-wallet huko kwote Watanzania wapo ambao wanatengeneza hela na wanatengeneza hela wakati mwingine naweza kusema hata hela zinaingia nchini kinyume na taratibu kwa sababu hakuna connection kati ya teknolojia, Serikali na taasisi za fedha. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa ombi langu kwa sababu ya ku-serve muda, Serikali tuamue kujifunza hata kwa nchi za wenzetu, tunaweza kujiuliza South Africa wanafanyaje mpaka wana ATM ya bitcoin, Kenya wanafanyaje mpaka wana ATM ya bitcoin? Kwa nini wanaweka zile ATM, wananufaika na nini.

MWENYEKITI: Malizia sentensi yako ya mwisho.

MHE. CONDESTER M. SICHALWE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, kwa hiyo kwa kumalizia ni kwamba tunaiomba Serikali iwekeze sana mahali hapa kwa sababu wimbi kubwa la vijana ambao wanatumia teknolojia wanaweza wakapata ajira kwa kupitia mahali hapa na Watanzania wengi wasiendelee kupotoshwa na kuibiwa kama ambavyo lilikuja hata wimbi la D9 watu wengi wakaibiwa ni kwa sababu Serikali ilikuwa haijaweka mikono yake namna gani ikusanye mapato na namna gani iwalinde Watanzania hawa. (Makofi)