Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Constantine John Kanyasu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. CONSTANTINE J. KANYASU: Mheshimiwa Mwenyekiti, Nyanza Cooperative Union wameshindwa kuendesha viwanda vya pamba kutokana na kuwa na madeni makubwa Benki. Pia kutokana na kupitwa na teknolojia ya viwanda walivyonavyo ambavyo sasa haviwezi kushindana katika soko kutokana na gharama za uzalishaji, kwa kuwa Serikali hivi sasa inataka kufufua viwanda vyote. Napenda kushauri Serikali kwanza kuwasaidia Nyanza kupata mbia ambaye atasaidia mitaji na teknolojia mpya katika ginneries.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Geita tunalima mananasi bora kabisa hapa Tanzania. Kwa muda mrefu zao la nanasi halijatumika kama kivutio cha uwekezaji na hivyo kupunguza uzalishaji kwa kuwa wakulima hawana soko la uhakika. Naiomba Serikali kupitia agenda ya Tanzania ya viwanda kutupatia mwekezajiwa Kiwanda cha Nanasi Geita na soko la nje la zao hili.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa Tanzania inataka kuwa nchi ya viwanda, nashauri kila Mkoa upewe maelekezo ya kupima maeneo maalumu ya viwanda, yaani industrial area. Maeneo haya yatengenezewe hati na yamilikiwe na Halmashauri ili mwekezaji akifika usiwepo usumbufu wa kupata maeneo. Maeneo haya yapewe miundombinu ya umeme, barabara na maji ili kumfanya mwekezaji kuvutika na hali hiyo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu upatikanaji wa mitaji, naomba kushauri kwamba Serikali mara itakapokuwa imefanya utafiti katika eneo fulani na kuona panafaa kiwanda, lakini hakuna wawekezaji, utumike mtindo uliotumika Rwanda ambao ni kwamba watu wenye mitaji ya wastani wanaunganishwa kwa hisa na kupewa access ya kukopa kwa collateral kwenye Benki maalumu kama TIB na kuwafanya wazawa kadhaa kumiliki kwa pamoja kiwanda. Haya yamefanyika Rwanda na viwanda vingi vinafanya kazi.