Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Kilimo

Hon. Santiel Eric Kirumba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Kilimo

MHE. SANTIEL E. KIRUMBA: Mheshimiwa Spika, wote ni mashaidi kwa muda mrefu ushirika umekuwa ukikabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo kukosekana kwa viongozi wa ushirika wenye uwezo wa kusimamia kikamilifu utekelezaji wa majukumu ya vyama kwa unafanisi. Hali hiyo imesababisha kukithiri ubadhirifu wa fedha na mali za wanaushirika hivyo kuwakatisha tamaa wakulima kujiunga na vyama hivi.

Mheshimiwa Spika, naomba Serikali kuweka mazingira rafiki wezeshaji kwa ajili ya upatikanaji wa masoko ya mazao ya uhakika ndani na nje ya nchi. Najua Serikali ilianzisha Kitengo cha Masoko (Agricultural Marketing Unit) katika Idara ya Maendeleo ya Mazao inayosimamia utafutaji wa masoko na tafiti za masoko na bei za mazao pamoja na kufuatilia mifumo ya uuzaji, pia Serikali inapaswa kuweka bajeti ya kutosha kufanya haya majukumu ili kusaidia hawa wakulima wetu wanapata shida.

Mheshimiwa Spika, naomba Serikali ya Awamu ya Sita kuendelea na utekelezaji wa programu ya kuendeleza kilimo awamu ya pili (ASDP II) hii itasaidia sana sekta ya kilimo. Serikali inapaswa kuboresha mifumo ya taasisi, bodi na sheria za kilimo kwa ajili ya usimamizi wa maendeleo ya mazao ya kilimo.

Mheshimiwa Spika, Serikali inapaswa kuunganisha wakulima wadogo na mashamba makubwa ili kuendeleza kilimo biashara, kupata ujuzi na maarifa ya kilimo. Wizara inapaswa kuharakisha upatikanaji pembejeo na masoko.

Mheshimiwa Spika, naiomba Wizara pia kuwekeza nguvu katika ukarabati wa miundombinu ya umwagiliaji, maghala, masoko na miundombinu bora ya kuhifadhi mazao ya kilimo. Pia naiomba Serikali kuimarisha uzalishaji wa mbegu bora na upatikanaji wa pembejeo nyingine za kilimo na kuzisambaza kwa wakulima.